Mchina aweka wazi kwamba Uganda na Rwanda lazima watii ili wapate mkopo

MK254

JF-Expert Member
May 11, 2013
31,529
47,777
Kwamba lazima wawe tayari kuunga kwenye reli ya Kenya ili wapate mkopo. Haya yaliwekwa bayana na waziri mkuu wa China, ifahamike Mchina anataka kuhakikisha miundo mbinu yake ndio inatamalaki ukanda wote huu na hataki uchakachuaji maana anawekeza kwa ajili ya miaka ya baadaye.
Ni wazi kwamba Afrika ndio iliyobaki na raslimali na fursa nzuri za kuwekeza, pia ukanda wa EAC ndio unaongoza katika ukuaji.

---------------------------------------------------------------------------------------------------
China has said it is ready to finance the construction of the standard gauge railway from Kisumu in Kenya to Uganda and Rwanda as long as the three countries agree to handle the project jointly.

According to Beijing, such an agreement among the three countries would minimise political risks and plug missing links.

There have been fears that the viability of the SGR within Kenya and beyond could be undermined by failing to link landlocked countries to the Mombasa port because of financial or other considerations.

Chinese Prime Minister Li Keqiang told Kenyan President Uhuru Kenyatta at the China Africa Summit in Beijing two weeks ago to discuss the extension of the railway line from Kisumu to Kampala and then Kigali with Presidents Yoweri Museveni and Paul Kagame.

Kenya State House spokesman Manoah Esipisu said Mr Li was clear that China would fund those sections as a regional project.

“The president already spoke with the leaders of Uganda and Rwanda on the possibility of sending a joint team to negotiate for financing of the remaining portion,” said Mr Esipisu. He said Kenya was now waiting for Kampala and Kigali’s response before planning an SGR beyond Kisumu.

“The viability of the (Nairobi to Kisumu) the line is okay. One feature of the SGR investment to Kisumu is the building of a modern port there. Kisumu to Malaba is viable with Uganda and Rwanda on board,” Mr Esipisu said.

Difficult terrain

On May 31, President Uhuru Kenyatta launched the operations of the first phase of the railway from Mombasa to Nairobi that cost $3.27 billion. He also announced a feasibility study for Phase 2B of the 350km line from Naivasha to Kisumu, for which China has committed a $3.6 billion loan. China is also funding the section from Nairobi to Naivasha at $1.5 billion.

Kenya Transport Cabinet Secretary James Macharia said the terrain in the Rift Valley is the reason it costs more from Nairobi to Kisumu (350km) than Mombasa-Nairobi (472km).

“We have to dig tunnels and construct more bridges across the landscape. That will obviously cost more,” he said in a briefing to journalists.

Sources said a joint project was appealing to the three countries. Uganda has been negotiating a $2.9 billion loan deal for the 293km section from Malaba to Kampala.

“We have to wait for our neighbours to decide on the plans for the last phase of this project before we can get the funds. China really doesn’t want to fund a white elephant project,” Uganda Finance Minister Matia Kasaija said in an interview with Bloomberg.

He said the China Export-Import Bank was only willing to fund the project if it was linked to the Kenya line at Malaba.

A Uganda government report released in April concluded that the Kenya SGR had the most potential to spur growth in the landlocked country. It said an SGR linked to Mombasa was shorter and more dependable because of the ongoing expansion of the Kenya port. Rwanda said last year it would link its SGR to the one proposed in Tanzania.

China plan raises hope for East African SGR project
 
Mchina mjanja sana aahhhh haaah all she wants is access to rich Congo,nakasema atawajengea bunge bure la usd 50 ml,Magu slowly but surely we reach there without Chinese, naamini tukipata what is ours kwny madini na mitandao ya simu mbona reli inajengeka vizuri tu.
 
Mchina mjanja sana aahhhh haaah all she wants is access to rich Congo,nakasema atawajengea bunge bure la usd 50 ml,Magu slowly but surely we reach there without Chinese, naamini tukipata what is ours kwny madini na mitandao ya simu mbona reli inajengeka vizuri tu.

Lazima ukubali kuliwa ili ule, hilo lipo tena kwa mataifa yote ya dunia, tatizo ni pale unaliwa hadi mifupa kama jinsi nyie huliwa kwenye shamba hilo la bibi. Nchi mna kila kitu madini zaidi ya mataifa yote Afrika, ardhi kubwa, vivutio bora zaidi ya mataifa bora Afrika, kwanza mpo nchi mbili ndani ya muungano yaani orodha ni ndefu ya kila sababu za nyie kuongoza Afrika kiuchumi na kila kitu, lakini mnatajwa kwenye orodha ya mataifa maskini wa kutupwa Afrika.

Leo hii baada ya zaidi ya miaka hamsini ya uhuru ndio mnagundua eti mnaliwa kwenye mchanga wa dhahabu, aisei tatizo lenu mna uzembe wa kusoma, hampendi kusoma kabisa hivyo inabidi mpigwe chenga kwenye mikataba, Kingereza huwa kinawapa chenga pia. Ukitaka Mtanzania atie saini chochote mpe mkataba ulioandkwa kwa kingereza chenye misamiati na maneno mengi, ataishia kuuliza wapi pa kutia saini, basi.

Mnafaa kwanza mnajifungia ndani na hiyo mikataba, mnasoma neno kwa neno, herufi kwa herufi kabla ya kutia saini. Bure mtaliwa hadi muikimbie nchi. Nyerere naskia alizuia madini yasiondoke hadi pale mtakua na elimu ya kutosha, sasa leo hii mnajinadi kuwa na elimu lakini mnaliwa balaa.
 
Kwa hili, nawapongeza Wachina...Sasa hebu Museveni ajaribu kuiasi project hii ya Northern Corridor kama alivofanya kwenye oil pipeline deal ndio atashangaa akikosa hata shillingi ya kujenga kilomita moja ya reli......I wont be surprised if this is one of the issues that Kenyatta discussed with China during the Belt and Road forum...Ukiwa unashirikiana na watu kama hawa ambao hawatabiriki, ni lazma uwe mwangalifu wasije waka vunja dili huku umewekeza hela nyingi mno..
 
MK254
Mathalani u sahihi kabisa lakini usidhani kwamba umasikini wa watanzania unasababishwa na elimu ndogo ya watanzania au kiwango cha kuongea kiingereza,
LA HASHA,
Watanzania wana elimu sana tena kubwa ila ukiritimba, ubinafsi, uchoyo, ulafi, wizi na kutojali maslahi ya mamilioni ya watu kwa ajili ya matumbo ya watu wasiozidi hata elfu ndo sababu ya umasikini wetu.
ila uzuri hatulii njaa
 
Ninawashauri Kenya waachane na outdated Mchina's train system just becasuse its free for now. (They must be sure that in the end they will have to pay for the loan)... Nimesikia jinsi hiyo train invayoenda utadhani fundi karai wanagonga nyundo. Yani ukitoka Mombasa mpaka ufike Nairobi, kichwa lazima kiume, au la sivyo ubebe Panadol!
Hiyo railway in the worst case scenario inafaa kuwa reli ya kubeba mizigo, not passengers!
 
Ninawashauri Kenya waachane na outdated Mchina's train system just becasuse its free for now. (They must be sure that in the end they will have to pay for the loan)... Nimesikia jinsi hiyo train invayoenda utadhani fundi karai wanagonga nyundo. Yani ukitoka Mombasa mpaka ufike Nairobi, kichwa lazima kiume, au la sivyo ubebe Panadol!
Hiyo railway in the worst case scenario inafaa kuwa reli ya kubeba mizigo, not passengers!
umepanda wewe mwenyewe ukaumwa na kichwa ama umeskia tu? pili, kama abiria wote walitoka wakiumwa basi kuna shida ila kama ni wachache, sioni shida...treni hii ina umuhimu sana hasa kwa mambo ya cargo...sasa issues za kelele dogo sana...wacha hata kama treni zingekuwa zinafanana kama zile za miaka 100 iliyopita lakini zinaenda kwa mwendo wa kasi na kusafirisha abiria na mizigo kwa mpigo, bado ningeipa heko!..issue sio treni inavokaa ama inavopiga kelele...issue ni kasi na ufanisi...
 
049cdd0882cd73091441ed67e2bfe3a9.jpg


Mchina ni nyoko, inaonekana kabisa kaishatutosa baada ya kupunch hizo projects zake za Mbegani port na SGR ya wizi. Hapa Museveni akitereza tu Kagame hapindui alafu reli yetu inakuwa white elephant project. Hapa ni kuhakikisha tunapata funds za haraka ili kujenga hii reli mapema iwekezanavyo. JPM akishundwa kufanya hivyo kamwe watanzania hatutamsamehe. Swali ni atapata wapi hela? Wazungu kawatibua, Wachina ndio hawamsomi? Balozi Maiga ana kazi sana.
 
049cdd0882cd73091441ed67e2bfe3a9.jpg


Mchina ni nyoko, inaonekana kabisa kaishatutosa baada ya kupunch hizo projects zake za Mbegani port na SGR ya wizi. Hapa Museveni akitereza tu Kagame hapindui alafu reli yetu inakuwa white elephant project. Hapa ni kuhakikisha tunapata funds za haraka ili kujenga hii reli mapema iwekezanavyo. JPM akishundwa kufanya hivyo kamwe watanzania hatutamsamehe. Swali ni atapata wapi hela? Wazungu kawatibua, Wachina ndio hawamsomi? Balozi Maiga ana kazi sana.
naona unaelewa sana jambo hili...umegonga ndipo..yaani ndio reli yenu isiwe tembo mweuoe, itabidi muharakishe sana ya Kenya isifike Kigali kabla ya kwenu...
 
Lazima ukubali kuliwa ili ule, hilo lipo tena kwa mataifa yote ya dunia, tatizo ni pale unaliwa hadi mifupa kama jinsi nyie huliwa kwenye shamba hilo la bibi. Nchi mna kila kitu madini zaidi ya mataifa yote Afrika, ardhi kubwa, vivutio bora zaidi ya mataifa bora Afrika, kwanza mpo nchi mbili ndani ya muungano yaani orodha ni ndefu ya kila sababu za nyie kuongoza Afrika kiuchumi na kila kitu, lakini mnatajwa kwenye orodha ya mataifa maskini wa kutupwa Afrika.

Leo hii baada ya zaidi ya miaka hamsini ya uhuru ndio mnagundua eti mnaliwa kwenye mchanga wa dhahabu, aisei tatizo lenu mna uzembe wa kusoma, hampendi kusoma kabisa hivyo inabidi mpigwe chenga kwenye mikataba, Kingereza huwa kinawapa chenga pia. Ukitaka Mtanzania atie saini chochote mpe mkataba ulioandkwa kwa kingereza chenye misamiati na maneno mengi, ataishia kuuliza wapi pa kutia saini, basi.

Mnafaa kwanza mnajifungia ndani na hiyo mikataba, mnasoma neno kwa neno, herufi kwa herufi kabla ya kutia saini. Bure mtaliwa hadi muikimbie nchi. Nyerere naskia alizuia madini yasiondoke hadi pale mtakua na elimu ya kutosha, sasa leo hii mnajinadi kuwa na elimu lakini mnaliwa balaa.
Mkuu hii comment yako imeniliza, siyo kwamba Tanzania hakuna vichwa, vichwa vipo sana tu, na watu waliosoma shule vizuri wapo wengi tu tatizo ni kupewa fursa ya kufanya kazi independently.
 
Lazima ukubali kuliwa ili ule, hilo lipo tena kwa mataifa yote ya dunia, tatizo ni pale unaliwa hadi mifupa kama jinsi nyie huliwa kwenye shamba hilo la bibi. Nchi mna kila kitu madini zaidi ya mataifa yote Afrika, ardhi kubwa, vivutio bora zaidi ya mataifa bora Afrika, kwanza mpo nchi mbili ndani ya muungano yaani orodha ni ndefu ya kila sababu za nyie kuongoza Afrika kiuchumi na kila kitu, lakini mnatajwa kwenye orodha ya mataifa maskini wa kutupwa Afrika.

Leo hii baada ya zaidi ya miaka hamsini ya uhuru ndio mnagundua eti mnaliwa kwenye mchanga wa dhahabu, aisei tatizo lenu mna uzembe wa kusoma, hampendi kusoma kabisa hivyo inabidi mpigwe chenga kwenye mikataba, Kingereza huwa kinawapa chenga pia. Ukitaka Mtanzania atie saini chochote mpe mkataba ulioandkwa kwa kingereza chenye misamiati na maneno mengi, ataishia kuuliza wapi pa kutia saini, basi.

Mnafaa kwanza mnajifungia ndani na hiyo mikataba, mnasoma neno kwa neno, herufi kwa herufi kabla ya kutia saini. Bure mtaliwa hadi muikimbie nchi. Nyerere naskia alizuia madini yasiondoke hadi pale mtakua na elimu ya kutosha, sasa leo hii mnajinadi kuwa na elimu lakini mnaliwa balaa.
umegonga ndipo bro!!!
 
MK254
Mathalani u sahihi kabisa lakini usidhani kwamba umasikini wa watanzania unasababishwa na elimu ndogo ya watanzania au kiwango cha kuongea kiingereza,
LA HASHA,
Watanzania wana elimu sana tena kubwa ila ukiritimba, ubinafsi, uchoyo, ulafi, wizi na kutojali maslahi ya mamilioni ya watu kwa ajili ya matumbo ya watu wasiozidi hata elfu ndo sababu ya umasikini wetu.
ila uzuri hatulii njaa

Kaka kingereza ni muhimu sana na hauwezi kukikwepa, haswa kwa nchi zetu hizi ambazo tunaagiza hadi sindano. Kwenu hapo mikataba, sheria na stakabadhi nyeti zimeandikwa kwa kingereza. Hivyo mtakiponda kila uchao kwa dhana ya 'sizitaki mbichi' lakini kimewazunguka na kuwalea. Lazima mkubali kuikabili hii lugha ya mabwana zetu Afrika, maana ndio inatumika kuwatafuna kwenye mikataba.

Hilo la nyie kuwa na elimu halina mashiko ni 'neither here nor there' maana elimu hiyo kama hamuitumii kulinda vya kwenu, basi haina umuhimu. Nafuatilia mijadala yenu ya mchanga wa madini hadi nahisi kujificha chini ya meza kwa aibu, kama kweli mumekua mkiliwa miaka yote hii kijinga hivyo pamoja na elimu yenu hiyo ni aibu kubwa Afrika na sio kwenu tu.
Wenye elimu huitumia kwa maslahi ya nchi, wanahoji balaa, na kukatalia chochote kisichoendana na misimamo yao, hata kama watapitia kibano sio kusubiri hadi mtafunwe mifupa ndio mnaanza kukurupuka.

Soma taarifa za profesa Wangari Maathai ndio uelewe nini maana ya elimu.
 
Wote mnaogonganishwa vichwa na huyu mkenya ni mazuzu

Ukifuata hii hoja kitaalam na kwa kutumia akili utajua kwamba hugonganishwi, maswali yanayoulizwa leo huko kwenu yalifaa kuulizwa kitambo, na ndio maana huwa unaskia historia inahukumu watu. Maamuzi ya leo yatahojiwa na vijana wa kesho. Rais wenu Magufuli amefanya maamuzi magumu hadi hata kumfuta waziri Muhongo ili kulinda nchi kwa kizazi cha kesho.
 
Ukifuata hii hoja kitaalam na kwa kutumia akili utajua kwamba hugonganishwi, maswali yanayoulizwa leo huko kwenu yalifaa kuulizwa kitambo, na ndio maana huwa unaskia historia inahukumu watu. Maamuzi ya leo yatahojiwa na vijana wa kesho. Rais wenu Magufuli amefanya maamuzi magumu hadi hata kumfuta waziri Muhongo ili kulinda nchi kwa kizazi cha kesho.
Hakuna jipya zaidi ya ujinga mtupu. What's so special with Kenyans anyway ? Kuwa mtumwa mwaminifu - A loyal slave. Achaneni na ropo ropo na maneno meengi kama watu wa Arusha, as blacks we have got a long way to go.

- Ukiangalia wanaoshikilia uchumi wa Kenya, ukaangalia na maisha ya kawaida ya mkenya ni SIMANZI tupu, leo badala ya kukaa ukafirikia namna mtakavyoweza kujinanasua kwenye huo mkopo wa mchina, mko busy na propaganda zisizo na maana. Msipoangalia mnaelekea kutumia YUAN ili msamehewe deni. Pathetic
 
Hakuna jipya zaidi ya ujinga mtupu. What's so special with Kenyans anyway ? Kuwa mtumwa mwaminifu - A loyal slave. Achaneni na ropo ropo na maneno meengi kama watu wa Arusha, as blacks we have got a long way to go.

- Ukiangalia wanaoshikilia uchumi wa Kenya, ukaangalia na maisha ya kawaida ya mkenya ni SIMANZI tupu, leo badala ya kukaa ukafirikia namna mtakavyoweza kujinanasua kwenye huo mkopo wa mchina, mko busy na propaganda zisizo na maana. Msipoangalia mnaelekea kutumia YUAN ili msamehewe deni. Pathetic
kawaida ya mdanganyika...kuropokwa tu kila upande....Kenya haitakuwa nchi ya kwanza kuwa na deni wala haitakuwa ya mwisho...afadhali nchi inayopiga hatua ka deni kuliko nchi stagnant wanaokimbizana kila uchao na sijui kina Bashite...yaani mkatae kutawaliwa na vyama vya kikoloni ndio mkomae kisiasa na kiuchumi..sasa hivi chama cha KANU kenya kiko kwa coma kinasubiri tu kifo...
 
Hakuna jipya zaidi ya ujinga mtupu. What's so special with Kenyans anyway ? Kuwa mtumwa mwaminifu - A loyal slave. Achaneni na ropo ropo na maneno meengi kama watu wa Arusha, as blacks we have got a long way to go.

- Ukiangalia wanaoshikilia uchumi wa Kenya, ukaangalia na maisha ya kawaida ya mkenya ni SIMANZI tupu, leo badala ya kukaa ukafirikia namna mtakavyoweza kujinanasua kwenye huo mkopo wa mchina, mko busy na propaganda zisizo na maana

Jifunze kusoma mada kuanzia mwanzo hadi mwisho sio kudandia tu bila kujua kichwa kiko wapi na inaelekea wapi. Mimi nilimjibu Mtanzania mwenzio aliyetutahadharisha kwamba tutaliwa na Mchina. Nikamkumbushia kama ni suala la kuliwa basi huo ushauri bora angeutumia kwa nchi yake kwanza maana nafuatilia mijadala yenu ya mchanga hadi aibu, mlivyotafunwa kwa miaka yote hiyo.

Kenya tunaliwa, hiyo sio siri lakini pia tunatafuna, ni mwendo wa kung'atana hadi kieleweke. Tumebanana hivi hivi hadi tumetoka kwenye orodha ya mataifa maskini wa kutupwa Afrika. Leo hii katiba yetu bora, GDP yetu inasoma kwenye $75b pamoja na kwamba hatuna madini ya kutajwa, nchi yetu ndogo eneo kubwa ni kame, vivutio vya utalii vichache, tumechezea mabomu ya alshabaab n.k.
 
Jifunze kusoma mada kuanzia mwanzo hadi mwisho sio kudandia tu bila kujua kichwa kiko wapi na inaelekea wapi. Mimi nilimjibu Mtanzania mwenzio aliyetutahadharisha kwamba tutaliwa na Mchina. Nikamkumbushia kama ni suala la kuliwa basi huo ushauri bora angeutumia kwa nchi yake kwanza maana nafuatilia mijadala yenu ya mchanga hadi aibu, mlivyotafunwa kwa miaka yote hiyo.

Kenya tunaliwa, hiyo sio siri lakini pia tunatafuna, ni mwendo wa kung'atana hadi kieleweke. Tumebanana hivi hivi hadi tumetoka kwenye orodha ya mataifa maskini wa kutupwa Afrika. Leo hii katiba yetu bora, GDP yetu inasoma kwenye $75b pamoja na kwamba hatuna madini ya kutajwa, nchi yetu ndogo eneo kubwa ni kame, vivutio vya utalii vichache, tumechezea mabomu ya alshabaab n.k.
yaani nchi ya tz imelala usingizi wa pono...tungekuwa tu na nusu ya rasilimali ambazo watz wanazo, dah! tungekuwa wapi aisee? nchi ya Kenya ni self-made...sio kama nchi zingine za kiafrika...ukienda SA utapata dhahabu...nenda Nigeria upate mafuta almaarufu 'dhahabu nyeusi' ..nenda Egypt na Angola pia utapata mafuta...Kenya ndio, tuna wildlife ila swala la terrorism limekuwa pigo kubwa...na tunasonga mbele tu...yaani uchumi wa $75B..in the next few years tutakuwa $100B na zaidi...bado ndogo lakini ni jambo la kufurahisha..
 
Lazima ukubali kuliwa ili ule, hilo lipo tena kwa mataifa yote ya dunia, tatizo ni pale unaliwa hadi mifupa kama jinsi nyie huliwa kwenye shamba hilo la bibi. Nchi mna kila kitu madini zaidi ya mataifa yote Afrika, ardhi kubwa, vivutio bora zaidi ya mataifa bora Afrika, kwanza mpo nchi mbili ndani ya muungano yaani orodha ni ndefu ya kila sababu za nyie kuongoza Afrika kiuchumi na kila kitu, lakini mnatajwa kwenye orodha ya mataifa maskini wa kutupwa Afrika.

Leo hii baada ya zaidi ya miaka hamsini ya uhuru ndio mnagundua eti mnaliwa kwenye mchanga wa dhahabu, aisei tatizo lenu mna uzembe wa kusoma, hampendi kusoma kabisa hivyo inabidi mpigwe chenga kwenye mikataba, Kingereza huwa kinawapa chenga pia. Ukitaka Mtanzania atie saini chochote mpe mkataba ulioandkwa kwa kingereza chenye misamiati na maneno mengi, ataishia kuuliza wapi pa kutia saini, basi.

Mnafaa kwanza mnajifungia ndani na hiyo mikataba, mnasoma neno kwa neno, herufi kwa herufi kabla ya kutia saini. Bure mtaliwa hadi muikimbie nchi. Nyerere naskia alizuia madini yasiondoke hadi pale mtakua na elimu ya kutosha, sasa leo hii mnajinadi kuwa na elimu lakini mnaliwa balaa.

Mkuu hujui tu jinsi hii comment ilivyoniuma.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom