Mchimba kaburi, kaingia mwenyewe

View attachment 529472

Mtu timamu hawezi kukataa salamu, na hapa ndipo nilipogunduwa huyu siyo kiongozi bali kidudumtu cha kwenye kisamvu, na kwa vitendo vyake ndiyo aichimbia kaburi CUF, inshallah ataingiya yeye na husuda zake na hao wanamtia wazimu aso kuwa nawo.

Aiwache CUF na aanzishe chama chake kama azani chama cha siasa aeza kukimiliki kama msuli. Mtu gani, kila panapo gogoro pua yake ipo, kila penye borongo, kono lake lipo na kila penye kandagalo guu lake lipo, na aanzishe chama chake na kiwe mali yake, watu waombe duwa, wamsalie mtumi, wapike basmati wale, washibe, na kushukuru.

Wasomjuwa wanamshangaa, wasomjuwa
wanadhani aonewa, wasomjuwa wanadhani mzalendo, lakini wanaomjuwa hata mishipa ya shingo haiwachezi pindi huyu Bwana akinung'unika kama mlango wa mninga uliolegea bawaba, haiwachezi, sababu wanajuwa hana lolote isipokuwa unafiki tu na anachojali na kupigania maslahi yake tu.

Kaisaliti Zanzibar na Abdul Jumbe kwa Nyerere kwaajili ya maslahi yake, na hata sasa kwa werevu wa mambo wangali wanahoji uhalali wake kidhamira katika kuongoza au kushiriki harakati za kudai Zanzibar yenye mamlaka ikiwa yeye alikuwa kizigiti kikubwa cha Zanzibar kuwa na mmalaka ndani ya Muungano.

Hakuna asiyejuwa, UAMSHO waliwaunganisha wazanzibar wote pasina kuzingatia tafauti zao za kisiasa au kidini, wimbo wao siku zote ulikuwa Zanzibar yenye mamlaka kamili aidha ndani ya Muungano au nje ya Muungano. Mashekhe hawa wakakamatwa Maalim akiwa sehemu ya serikali, na wakaletwa bara, Maalim akiwa sehemu ya serikali. Tumeshuhudia CUF ikifanya maandamano katika mambo mengi, lakini hatukuona maandamano ya CUF wakitaka hawa mashekhe waachiliwe au warudishwe kwenye mahakama za Zanzibar.

Huu ni usaliti mwingine wa Seif kwa Wazanzibari, kwa nafasi yake ndani ya serikali angetia juhudi za kuhakikisha mashekhe hawaletwi bara kama alishindwa kuzuia kukamatwa kwao, na kubwa zaidi angejiuzulu kwa kuonesha kuwa yeye siyo sehemu ya dhuluma wanayofanyiwa wazanzibar.

Usaliti mkubwa zaidi ambao unamshushia hadhi yake ni huu ambao anaoufanya sasa.Maalim Seif anaisaliti CUF, amekiingiza chama katika makubaliano ya ovyo kabisa ya UKAWA kwa tamaa ya fedha za kampeni na urais, mbaya zaidi ananadi kuwa UKAWA umesaidia kuwapa wabunge wengi na kwamba bila UKAWA wasingepata wabunge hao, kauli hizi ni za kukisaliti chama na kauli za kusaliti na kudharau juhudi za wanachama na watendaji wa chama za kuijenga CUF kutoka 2010 kuelekea 2015.

Hivi kama UKAWA ina gawa wabunge na madiwani kama njugu, vije leo NCCR iwe na mbunge mmoja na NLD isipate mbunge hata mmoja? Kwanini CUF iwe na wabunge wengi kuzidi NCCR? Kwanini CHADEMA iwe na wabunge wengi zaidi? Jawabu liko wazi, CUF chini ya Lipumba na yeye mwenyewe Maalim ndiyo ya kupongezwa kwa idadi hiyo ya wabunge na siyo UKAWA, ingawa simaanishi ushiriki wa UKAWA katika natija hii ni wa kubezwa.

KUHUSU KUJIUZULU LIPUMBA.
Huko juu nilisema Seif kakiingiza chama katika makubaliano ya ovyo kabisa na/au kwa kwenda kinyume kabisa mpango wa CUF ndani ya UKAWA, na jambo hilo Prof alionya na kutahadharisha ndani ya vikao vya chama, lakini katibu mkuu kwa ubabe huku akidharau vikao na taratibu za chama, akafanya borongo.

Prof Lipumba aliandika barua ya kujiuzulu kwa minajili ya kutaka kuitishwa MKUTANO MKUU CUF,,,,na katika mkutano huo angeulizwa sababu ya kujiuzulu kwake kabla ya mkutano huo kuridhia au kukataaa kama katiba ya CUF inavyoelekeza.

Kwahivyo barua kwa Seif na timu yake waliona ni barua ya kujiuzulu,lakini kwa Lipumba yale yalikuwa ni mashitaka dhidi ya katibu mkuu ndani ya mkutano mkuu. Mashitaka ambayo yangemweka hatarini aidha katibu mkuu au mwenyekiti.

MWISHO.
Zamani nilidhani nyumbu ni wafuasi tu CHADEMA, lakini kumbe zipo nyumbu zingine upande wa Maalim Seif, wakati Lipumba akiweka kusudio lake wazi la kufuta barua yake ya kuomba kujiuzulu, watu wanaomuunga mkono waliambiwa na akina Mtatiro kuwa ni wafuasi wa mtu badala ya chama, lakini sasa Maalim Seif akiwa na uwezekano mkubwa aidha wa kuanzisha chama au kuhamia CHADEMA, walewale waliowaita wenzao ni wafuasi wa Lipumba badala ya chama nawo wanampango kuondoka na Maalim Seif huku wakiahidi kukichimbia kaburi CUF Zanzibar.

Nami nawaambia, waende salama, ila wajuwe fika hilo kaburi wataingiya wenyewe na husuda zao, kama usemavyo msemo wa kiswahili, " mchimba kaburi kaingiya mwenyewe"

Dotto Rangimoto Chamchua
Jini Kinyonga
Likizoni Dar es salaam.
0622845394

Ww umetumwa co bure...wengine wanahubiri amani na kupambana na wezi wa makinikia ....ww unakja na stori zako za kwenye kahawa..
 
ACT adui yenu ni CUF au CCM?

Mbona sijawahi kuona wewe mleta thread ukienda kinyume na CCM hata siku moja?

Kama wewe ni mwana ACT kweli, na kama unaamini chama chako ni wapinzani kweli, basi hupaswi kumbeza Maalim Seif hata dakika moja. Alichofanyiwa Maalim na CCM, hakikuwa haki, wala hakina afya kwa ustawi wa demokrasia Tanzania.

Kama CUF walidhulumiwa vile, kwanini wewe unayejiita mwanaACT unafurahia huu ujinga wa CCM? kwanini unaamini kuwa yaliyofanywa kwa CUF hayawezi kufanywa kwenu nyie ACT? Au mwenzetu uliona alichokifanya JECHA ni sahihi?

Kama una macho usome uelewe.
 
Sidhani kama ni sheria au lazima kupokea Salam ya kila mtu
Maalim Seif ni muislam na kwenye uislam kusalimia ni sunna na kuitikia salamu ni faradhi nikufafanulie unaweza kuamua wa kumsalimia usipate dhambi lakini ukisalimiwa ni sharti kuitikia, mengine ya mtoa mada naona mapichapicha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom