Mchezo (mwingine ) mchafu kumchagua DG mpya DAWASCO

Game Theory

JF-Expert Member
Sep 5, 2006
8,545
833
Wakati tuko bize na huu wa NHC kuna mwingine unaendelea kule DAWASCO (ambao kuna wakati walinipiga mkwara nisianike data za deal nzima ya Privatization yao).



Naam katika hii game ya MICHEZO ya KIFISADI na KIHUNI inaendelea kwenye ajira serikalini, kama tunavyojua ile ya NHC dili lilikuwa linachongwa na mzee LUHANJO wa IKULU, sasa kule DAWASCO main player ni waziri MARK MWANDOSYA

Nyeti ni kuwa Waziri huyu anaendeleza civil war na sasa hiviniongeavyo kuna open conflict kati yake na BODI ya shirika hili la umma ambalo tarehe 25 January, walishortlist six candidates for the post of its CEO.

Habarai zinaendelea kusema kuwa waombaji ilitakiwa wawe wamefayiwa interview mwanzoni mwa February lakini hiz interview zenyewe hazikufanyika kwa sababu tarehe 27 January kwa sababu zisizoeleweka ikaibuka shortlist nyingine yenye majina mapya 7! hivyo zoezi zima likawa kama mazingaombwe na kuwachanganya hao ma candidates na if the anything the whole thing went from farse to confusion!


Naaam, kimbembe chote hiki kilianza paleee bosi wa sasa bwana ALEX KAAYA alipofikia kikomo cha mkataba wake na baada ya hapo bodi ya DAWASCO ikamwandikia MWANDOSYA barua kumwomba aaprove mkataba wa kumwongezea muda wa miaka mingine 4 bwana Kaaya.

Mwandosya akagoma, na akawapiga mikwara bodi kuwa wamwachie yeye kazi ya kumchagua CEO mpya wa DAWASCO. Na kilichomuudh bwana mwandosya ni bodi kumu overule na kuamua kufuata sheria na wakatengeneza short-list yao wao ambayo ilikuwa na 6 candidates.

Kujibu mapigo waziri Mwandosya alitoa amri kwa vijana wake watoe short slit yake na wa Cancel ileeee ya mwanzo ya bodi. So far kinachoendelea kule DAWASCO ni total confusion btn waziri na bodi ambao wanatunishiana misuli na kila mmoja nataka kuonyesha ubosi


Na kwa jinsi mambo yanavyoeendelea tuko njiani kuona NHC deja vu!
 
tatizo si Mwandosya wala Luhanjo.....
tatizo ni Kikwete period,,,,,,,,
kila mtu serikalini anajifanyia lake kwa sababu mkuu yuko too busy
na safari na mengineyo........
 
Tatizo ni mfumo mzima na utawala, hali kama hizi zipo kila sehemu ila kuna kazi kubwa sana katika watoto wa maskini katika Taifa letu Tanzania maana kila sehemu ukienda utakuta mambo haya
 
tatizo si Mwandosya wala Luhanjo.....
tatizo ni Kikwete period,,,,,,,,
kila mtu serikalini anajifanyia lake kwa sababu mkuu yuko too busy
na safari na mengineyo........

Tatizo siyo Kikwete wala Mwandosya wala Luhanjo; tatizo ni sisi wenyewe watanzania kwa kukubali kuona serikali inaendesha mambo yake nyuma ya pazia. Hatuna hata sheria yoyote inatupa uhuru wa kupata taarifa za mambo yafanywayo na serikali, na tunasema mswano
 
..let them beat around the bush. but all that we want is a competent guy to manage DAWASCO, period!!
You know, wenyewe wanasema wako kwenye mchakato... Na wakikosea, watasema "tulikuwa hatujajipanga vizuri"
 
Siku zote kukitokea changes kuna watu wanachukua muda kuelewa!

I doubt, they may not be wrong only that we do not have full information. We only have one sided information and probably coming from loosers....
 
..let them beat around the bush. but all that we want is a competent guy to manage DAWASCO, period!!
You know, wenyewe wanasema wako kwenye mchakato... Na wakikosea, watasema "tulikuwa hatujajipanga vizuri"
huyo COMPETENT GUY hawezi kupatikana katika utaratibu kama huu, wa kuleteana vi memo, we angalia watu wameshakaa chini na kuchagua watu wao sita ili wafanyiwe final interview, sasa huyo wa saba katoaka wapi?
 
kwani nani yuko juu?waziri au bodi ya wakurugenzi?

Tatizo ni system yetu kuwa mbovu, ukiangalia kiundani Waziri sio mwajiliwa wa wizara yoyte, maana anaweza leo kuwa waziri wa mawasiliano kesho akawa waziri katika wizara nyingine, lakini kuna watendaji wakuu ambao ni waajiriwa,
sasa hapa ndio inapokuwa mchanganyiko mkuu
 
watanzania tuamke na tukubali kwamba tatizo sio waziri, bodi au nini... Tatizo ni mfumo. Its a high time ile kamisheni ya ajira ipewe muscles za kuweza kuajiri hata executive positions, ingawa na yenyewe bado... Au hata agencies za kimataifa zifanye hiyo kazi
Tusitegemee chochote kwani iwe bodi au waziri, kila mmoja anavutia kwake.

Mizegwe kama hiyo ipo kwenye upatikanaji wa DG wa MSD, mamlaka ya hifadhi za jamii, TTB, na hata bima

Tunahitaji wizara husika kubadili mfmo wa kazi
 
Kwa nini wasiandike kwa Watanzania wote kuapply baada ya hapo waangalie vigezo wanavyotaka? sasa hii ya bodi kuandika short list na wote wanabodi wakaweka majina ya ndugu zao kuna la maana hapo?
 
Kwa nini wasiandike kwa Watanzania wote kuapply baada ya hapo waangalie vigezo wanavyotaka? sasa hii ya bodi kuandika short list na wote wanabodi wakaweka majina ya ndugu zao kuna la maana hapo?
Hata wakitangaza nini, mchujo ndio huleta mfarakano... Na pia kuna wakati hata huko juu wanapofanya 'venting' huendeleza kuharibu mambo
 
Kuna tatizo gani kwa aliyemaliza muda wake? ametekeleza majukumu yake kwa kiwango gani, performance appraisal yake iko ngapi katika viwango vya asilimia?

Upande wangu.
Mimi naona kuna mabadiliko kwa kiasi fulani katika swala zima la usambazaji wa maji katika jiji letu. ingawaje kuna maeneo ambayo hali siyo njema katika upatikanaji wake.

Kuna matatizo ambayo ni utendaji wa serikali na mengine ni utendaji wa Mkurugenzi wa dawasco moja kwa moja. Hekima yangu inaniambia kama umri unamruhusu na hakuna lolote linalotufanya sisi wakazi wa DSM tulalamike basi hakuna haja ya yeye kubadilishwa kwa sababu tu Waziri Hamtaki.
 
Kwa nini wasiandike kwa Watanzania wote kuapply baada ya hapo waangalie vigezo wanavyotaka? sasa hii ya bodi kuandika short list na wote wanabodi wakaweka majina ya ndugu zao kuna la maana hapo?

Kwani utaratibu wa kupata DG wa DAWASCO unasemaje? Je bodi ina mamlaka ya kutafuta DG au ni jukumu la Waziri? Kama ni jukumu la bodi waziri hawezi kuingilia hila kama ni Waziri pia bodi haiwezi kumuingilia.

Lakini katika mashirika yetu mengi ni Waziri/Rais. Kwa hiyo waziri anaweza kuwa na mechanism za kufanya katika kutafuta DG. Kupata DG haliwezi kuwa jukumu la bodi.
 
TATIZO NI THITHI!

Sawa kabisa nakubaliana na huyu, na hali kadhalika nakubaliana na wale wanaodai ni mfumo mpaya, mpaya kabisa.

Ukitaka CEO na Deans na HoDs kwenye vyuo vikuu, mfumo wa sasa(umeasisiwa na UDSM kusema kweli), ni kuwa wanateuliwa watu watatu, wanapewa jukumu la ku-search wanaofaa!Unajua nini hao watatu wanachaguliwa na mkuu aliye madarakani, yaani Mkandala akitaka Deputy VC wake yeye ndiye anayechagua search team, itamletea nani!!!? Haya madudu yanaacha mianya mingi ya hicho kitu kitamu cha kutamanika RUSHWA! Na thithi thote hatujali tunapoona sera mpya ambayo inaweza kufungua hio mianya, uliza kule UDSM kama wamewahi hata kukohoa kuhusu anayeteua search team. Hivi vijimambo vya kukaa kimya..THITHI...

Taasisi zetu zinaendeshwa kwa mikutano kibao tena inayochukua muda mrefu (ndio ni lazima na vibahasha viwepo), lakini amini usiamini, zaidi ya 80% ya wanaohudhuria hawafungui mdomo isipokuwa wanapokula kuku, sambusa, juisi, mapapai.

Ni kwa nini Bodi ya NHC haikuachagua mtu wao! Yaani taasisi nyeti kama NHC inaweza ikathubutu kuwa na BODI Mpya, MANAGEMENT Mpya kwa wakati...ni lazima kuna vitu vinajengwa...nitaanza kupayuka niachie hapa....
 
Awali ya yote naunga mkono hatua ya Waziri Mwandosya kutoapprove extension ya mkataba wa DG juu kwa juu, ata kama mtu atakuwa amefanya vizuri ni muhimu baada ya mkataba nafasi itangazwe na kushindaniwa kwa haki.

Lakini swali ni je hiyo nafasi ilitangazwa ili watu waaply na kushindanishwa ili kupata hizo shortlists?
 
Every important post in Tanzania is Political..!!!

Politicians are Gods in our country; this really sucks.

It doesn't have to be this way.
 
Tatizo ni thithi

thawathawa umethema kweli kabitha

Every important post in Tanzania is Political..!!!

Politicians are Gods in our country; this really sucks.

It doesn’t have to be this way.

Yah! piga shule yako, soma professional yeyote at the end of the day mwanasiasa ndiye anayekuamulia maisha. nchi yetu hii ndiyo maana watu hawarudi kila kona 'umimi'
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom