Mchezaji Zana Coulibaly wa ASEC Mimosas awasili nchini kukamilisha taratibu za kujiunga na Simba SC

Ghazwat

JF-Expert Member
Oct 4, 2015
23,718
66,262
Mchezaji wa nafasi ya ulinzi Zana Oumar Coulibaly, wa ASEC Mimosas ya Ivory Coast amewasili nchini Tanzania kukamilisha taratibu za mwisho za kujiunga na Simba SC

Coulibaly ambaye ni beki mwenye uwezo uwanjani msimu uliopita alitumikia ASEC Mimosas katika michuano Kombe la Shirikisho Afrika, punde tu baada ya kuwasili nchini alikwenda uwanja wa Taifa kushuhudia Simba ikitakata kwa ushindi mnono wa mbao 4-1 dhidi ya Mbabane Swallows katika mchezo wa ligi ya mabingwa.

Zana Coulibaly, anacheza nafasi ya ulinzi upande wa kulia anakuja kuziba nafasi ya Shomari Kapombe ambaye amepata majeraha ya kuumia mguu akiwa kambini Afrika Kusini wakati timu ya Tanzania Taifa Stars ikijiandaa kupapana na timu ya Taifa ya Lesotho.

=====

Mchezaji Zana Coulibaly raia wa Burkina Faso, aliyekuwa akichezea ASEC Mimosas, amesajiliwa na klabu ya Simba baada kukamilika kwa vipimo vya afya Jana.

Leo, Novemba 30, 2018 Zana amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia Simba mbele ya Mkurugenzi Mkuu (CEO) Crescentius Magori, huku akikabidhiwa jezi namba 21.

IMG_20181128_191130_051.jpeg
IMG_20181128_191154_974.jpeg
IMG_20181128_191628_168.jpeg
 
Mchezaji wa nafasi ya ulinzi Zana Coulibaly, wa ASEC Mimosas ya Ivory Coast amewasili nchini Tanzania kukamilisha taratibu za mwisho za kujiunga na Simba SC

Coulibaly ambaye baada ya kuwasili nchini alifika moja kwa moja uwanja wa Taifa kushuhudia Simba ikitakata kwa ushindi mnono wa mbao 4-1 dhidi ya Mbabane Swallows katika mchezo wa ligi ya mabingwa.

Zana Coulibaly anacheza nafasi ya ulinzi upande wa kulia anakuja kuziba nafasi ya Shomari Kapombe ambaye amepata majeraha.

View attachment 949438View attachment 949439View attachment 949441
Kweli tunaelekea kubaya, yaani imefikia tunasajili makipa na beki wa pembeni kutoka nje ya Tanzania nafasi ambazo watanzania wapo wanao zimudu.!! Mpira wa Tanzania umesha kufa.
 
Kwani ambapo hatuchukui wachezaji kutoka nje mpira wetu umefika wapi?

Na wachezaji wetu nani amewazuia kutoka nje ya nchi?
Kweli tunaelekea kubaya, yaani imefikia tunasajili makipa na beki wa pembeni kutoka nje ya Tanzania nafasi ambazo watanzania wapo wanao zimudu.!! Mpira wa Tanzania umesha kufa.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Huenda ikawa hivyo..Huyu Niyonzima hela imepotea bure tu, siku akiingia hana mpya, aangalie Dilunga akiingia namna anavyotoa pasi za mwisho
Nani ataondoka ili huyu beki apate nafasi ya wachezaji wa kigeni ?
Ni Niyonzima ?
 
Kweli tunaelekea kubaya, yaani imefikia tunasajili makipa na beki wa pembeni kutoka nje ya Tanzania nafasi ambazo watanzania wapo wanao zimudu.!! Mpira wa Tanzania umesha kufa.
Nani anaimudu bongo mmefungwa hadi na Lesoto
 
Back
Top Bottom