UZUSHI Mchezaji Thomas Langu Sweswe alicheza mpira dakika 90 bila kugusa mpira

Baada ya tathmini, tumebaini kuwa taarifa hii ni ya uzushi
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
Thomas Lungu Sweswe ni mchezaji wa zamani wa Zimbabwe, beki wa kati anadaiwa kushikiria rekodi ya kucheza dakika 90 dhidi ya Keiza Chiefs bila kugusa mpira.

1666761379439.png
 
Tunachokijua
Kwa mujibu wa Mwandishi Oladele Emmanuel wa nigfooty.com anaeleza kuwa alifanya jitihada za kumtafuta mchezaji huo na kufanya naye mahojiano ili kupata ukweli wa madai ya yeye kucheza dakika 90 bila kugusa mpira.

Beki huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 38 aliiambia nigfooty.com kwamba habari hizo si za kweli na zaidi alisema yeyote aliyepika hadithi hiyo ana ajenda yake binafsi ya kumchafua.

Sweswe anasema "huo ni uwongo, hata kama una siku mbaya mchezoni kiasi gani hakuna namna jambo hili linaweza kutokea. Haiwezekani mchezaji yoyote anayecheza soka la ushindani kucheza dakika 90 bila kugusa mpira".

"Aliyekuwa nyuma ya jambo hili ni mtu mwenye ajenda binafsi, sijui kwanini hakutaja jambo hili wakati ule niliocheza mpira na akaja na hadithi hiyo wakati huu. Siku zote mimi hucheka wakati watu wengi hunitumia ujumbe wakiuliza ikiwa ni kweli nilicheza dakika 90 zote bila kugusa mpira.

Sasa nimerejea nyumbani Zimbabwe nikifanya kazi kama Katibu Mkuu wa Muungano wa Wanasoka wa Zimbabwe"
Thomas Langu Sweswe aliongeza.

Zaidi ya hayo, JamiiForums imefanya mawasiliano na Sweswe ili kuthibitisha habari hii ambapo Sweswe alieleza

"Taarifa hizo ni za Uzushi zinaenezwa na mtu mwenye ajenda binafsi, mwenye nia ya kunichafua. Ukitazama habari hiyo na tarehe inayodaiwa nilicheza bila kugusa mpira nilikuwa tayari nimeshastafu kucheza soka. Pia taarifa hiyo haielezi mechi hiyo nilicheza dhidi ya timu gani na ilikuwa kiwanja gani."

Hivyo, kutokana na ufafanuzi huu kutoka kwa Thomas Sweswe na kukosekana ushahidi wa jambo hili JamiiForums inapata shaka ya rekodi hii kuwa na ukweli.
Harry Maguire mwenyewe hugusa mpira atleast kila baada ya dakika 4 -5 kutokana na kasi ya soka la Ulaya.
 
Kuna game 1 hivi ilikuwa chelsea na timu 1 epl. Lukaku alikuwa na touch 8. Na kati ya hizo 4 alikuwa offside.
 
Duuuuh, yaweza kuwa kweli kulingana na timu pinzani aliyokutana nayo kwa wakati huo,Lakin Kama tumejiridhisha kwa maneno ya Mhusika na kukana habar hiyo tumziangatie(SWESWE)
 
7 Reactions
Reply
Back
Top Bottom