mchezaji huyu wa taifa stars afundishwe adabu;akome kutuzalilisha watanzania

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,722
21,775
Pamoja na wachezaji kucheza kwa kiwango cha hali ya juu hakika katika mpira nidhamu ni kitu cha muhimu sana sana;

jana kwa walioangalia mpira kuna kijana ambae leo kwenye gazeti la dar leo kapongezwa na maximo na kweli alicheza vizuri sana ila nafikiri maximo anaitajika kumfundisha awe na adabu uwanjani;mechi ya jana wacha walio uwanjani hadi watoto wadogo wanangalia;anaitwa ABDULHALIM alikuwa amesuka nywele zake,ni mchezaji mzuri sana kama mlivyokuwa mkiona alikuwa akikabana na mchezaji mmoja wa ivory coast,,

Baada ya mechi kuisha ,huyu bwana akamfwata kama anampa fairplay kwa yaliotokoea uwanjani;yule mchezaji akampa mikono miwili kwa heshima gafla jamaa akasukuma akaanza kuongea maneno ya kipumbavu mpaka refa akamfwata baadae maximo akamzuia;

Hawa ndio wachezaji tunatarajia waende kucheza hata sweden loh?shame on u.mpira ukiisha mnamaliza matatizo yenu kama unaitaji kuwa international player,kama uamini abdul subiri yatakayomkuta boban .utakumbuka ninachokwambia kakangu,kama mtakuwa na uchezaji mzuri bila nidhamu mtaishia na patririon ya kuja bongo bila police.....,

Tunaomba viongozi wetu wajue jinsi ya kuwafuundisha awa watu;wazima
 
bila nidhamu mimi kwa mtazamo wangu mafanikio huwa hayawezekani!!!
 
Weren't Tanzanians complaining about Maximo not including undisciplined players?

This kind of behaviour is exactly why Maximo was absolutely right.
 
Pdidy,

Yule jamaa alinikera hata mimi binafsi, ukiacha liletukio baada ya mpira kuisha, wakati wa mchezo ule alikuwa na confrontation za kipumbavu sana na wale jamaa wa IC...hasa huyo jamaa anaitwa Dindane.....! sijui alikuwa anataka kuonyesha nini....but kwa harakaharaka anaonekana jamaa wa ndumu sana, na anataka kuonyesha ubabe kwamba na yeye hawavumi lakini wamo....hopeful!...angalia hata alivyojieleza wakati anahojiwa na mtangazaji.......the boy is totally out of his mind & undisciplined!
 
uwanjani;
.........yule mchezaji akampa mikono miwili kwa heshima gafla jamaa akasukuma akaanza kuongea maneno ya kipumbavu......

Ndugu yangu hebu acha kumuonea mzanzibari mwenzangu...

hilo sekeseke ni wengi tulilishuhudia, wengine walikuwepo uwanjani na wengine kupitia runinga.

kwanza hayo maneno ya kipumbavu ni yepi? unaweza kuya-quote hayo maneno?

Mie nilikuwa nimekaa upande wa orange straight kulia kwa jukwaa kuu na hilo tukio nililishuhudia.

Abdulhalim hakumfanyia chochote kibaya Aruna Dindane, isipokuwa Dindane ndiye alionyesha dharau kwa abdulhalim. Na kama unakumbuka vizuri abdulhalim ndiye alimfuata Dindane kumpa mkono na kuyamaliza kutokana na purukushani iliyokuwa imetokea hapo kabla. Sasa unadai afundishwe adabu ipi?

baada ya dindane kuonyesha kumpandishia na kumsukuma ndipo jamaa nae akawa anakomaa nae, isingekuwa rahisi katika hali ile wenyewe wayamalize bila mtu mwingine kuingilia kati na ndio sabau ya refa kuingilia kati kuwatenganisha, so usimlaumu bure kijana wa watu hakufanya jambo lolote baya la kufaa kufundishwa adabu, labda utafute jambo lingine.

au unataka kumfagilia maximo kiujanja ujanja?
 
Pdidy,

Yule jamaa alinikera hata mimi binafsi, ukiacha liletukio baada ya mpira kuisha, wakati wa mchezo ule alikuwa na confrontation za kipumbavu sana na wale jamaa wa IC...hasa huyo jamaa anaitwa Dindane.....! sijui alikuwa anataka kuonyesha nini....but kwa harakaharaka anaonekana jamaa wa ndumu sana, na anataka kuonyesha ubabe kwamba na yeye hawavumi lakini wamo....hopeful!...angalia hata alivyojieleza wakati anahojiwa na mtangazaji.......the boy is totally out of his mind & undisciplined!

hivi kumbe ndo yule........that was pride hata si confidence ile!!!! majivuno ya kijinga!!!
 
Jamani wachezaji wetu walicheza vizuri sana jana. Nadhani kulikuwa na sababu ya kuwa na ari ya kucheza vizuri. Kwanza walikuwa ndio under dogs, pili walikuwa wanajua watu wengi hatukufurahia performance ya T.Stars kwenye challenge cup ya majuzi -they needed to prove they are able. Tatu walikuwa hawana cha kupoteza katika mechi hii -there was nothing at stake, hivyo naweza ku-argue kwamba Ivory Coast walicheza bila ari kubwa ya kushinda lakini hata kwa kiwango hicho cha chini bado tulishindwa kuwafunga. Ingekuwa ni mechi ya mashindano huenda tungebamizwa mengi zaidi. Mimi nina mashaka na performance ya timu yetu hasa wanapokuwa kwenye mechi muhimu kama ilivyokuwa 1/2 fainali kule Nairobi. Katika mechi muhimu naona wanashindwa kucheza vizuri. Nidhamu mbaya ni moja ya sababu inayochelewesha mafanikio ya timu yetu. Pia hatuna wachezaji wengi wanaocheza mpira wa kulipwa katika ligi kubwa duniani. Lishe nimeona pia ni tatizo kwani wale wa Ivory Coast walionekana wana nguvu sana kuzidi wa kwetu. Tusikimbilie kumchoka Maximo, huenda ndio bora kwetu kwa hali tuliyonayo. Hata akija Ferguson leo, naamini bado tutashindwa hata kuchukua kombe la Challenge. TFF lazima i-address mambo ya msingi kama kuanza kufunza mpira tangu mashuleni n.k. Kumbuka michuano ya UMISETA ya miaka ya 80 ilivyoibua wachezaji wakali kama George Kulagwa, Rahim Lumelezi na wengine wengi. Bado hatujajifunza tu??? Tunataka kocha mzuri aje kufunza watu wazima wasiofundishika kirahisi. Come on, lets be serious bwana.
 
Jamaa nilimwona toka challenge kule nairobi, alicheza vizuri sana walipocheza na uganda nilijua azima maximo amchukue, sasa km ni mbabe nidhamu hana basi tena
 
Pdidy,

Yule jamaa alinikera hata mimi binafsi, ukiacha liletukio baada ya mpira kuisha, wakati wa mchezo ule alikuwa na confrontation za kipumbavu sana na wale jamaa wa IC...hasa huyo jamaa anaitwa Dindane.....! sijui alikuwa anataka kuonyesha nini....but kwa harakaharaka anaonekana jamaa wa ndumu sana, na anataka kuonyesha ubabe kwamba na yeye hawavumi lakini wamo....hopeful!...angalia hata alivyojieleza wakati anahojiwa na mtangazaji.......the boy is totally out of his mind & undisciplined!

nahisi malaika amekuleta;nilitaaka kumwonglea alivyokuwa anajibu kihuni kama amepata ganja;nahisi atakuwa wale wale;bila ndumu game aipandi;
 
nahisi malaika amekuleta;nilitaaka kumwonglea alivyokuwa anajibu kihuni kama amepata ganja;nahisi atakuwa wale wale;bila ndumu game aipandi;


wachezaji kama wale kabla ya mechi wanaitaji kupimwa;yawezekana ganja ndio ilikuwa ikifanya kazi ,
 
Jamani hivi ni lini tutakuja kukubali kuwa Taifa stars sio Kilimanjaro stars?. Kikosi kilichocheza jana kama ni challenge mbona wangechukua bila tatizo.

Taifa stars = Kili + Karume. ndo maana timu inakuwa kali zaidi kama ya jana.
 
Yule bw mdogo akiendelea hivyo bac hata last longa....kama diof vile!!
 
Swali: Mazungumzo kati ya Aruna Dindane na huyu Abdulhalim yalikua katika lugha gani vile?
 
Ndugu yangu hebu acha kumuonea mzanzibari mwenzangu...

hilo sekeseke ni wengi tulilishuhudia, wengine walikuwepo uwanjani na wengine kupitia runinga.

kwanza hayo maneno ya kipumbavu ni yepi? unaweza kuya-quote hayo maneno?

Mie nilikuwa nimekaa upande wa orange straight kulia kwa jukwaa kuu na hilo tukio nililishuhudia.

Abdulhalim hakumfanyia chochote kibaya Aruna Dindane, isipokuwa Dindane ndiye alionyesha dharau kwa abdulhalim. Na kama unakumbuka vizuri abdulhalim ndiye alimfuata Dindane kumpa mkono na kuyamaliza kutokana na purukushani iliyokuwa imetokea hapo kabla. Sasa unadai afundishwe adabu ipi?

baada ya dindane kuonyesha kumpandishia na kumsukuma ndipo jamaa nae akawa anakomaa nae, isingekuwa rahisi katika hali ile wenyewe wayamalize bila mtu mwingine kuingilia kati na ndio sabau ya refa kuingilia kati kuwatenganisha, so usimlaumu bure kijana wa watu hakufanya jambo lolote baya la kufaa kufundishwa adabu, labda utafute jambo lingine.

au unataka kumfagilia maximo kiujanja ujanja?

This is what I saw!! Thanks
 
hilo li mchezaji ni miongoni mwa mazuzuz magic mengi tuliyonayo hata Tanzania.
Tuyakemee kwa kuyataja kwa majina hadharani ili umma uwaumbue.
 
jamani aliyeanzisha fujo ni Dindan, me sijaona kuwa yule mchezaji wetu kaanzisha fujo.
 
Hayo maneno ya kipumbavu aliyoyamwaga ni yapi, unaweza kuyaweka?
 
nahisi kama tulikuwa tunaangalia mechi tafauti. kwa sisi tilioona vizuri ni vyme hili likawekwa sawa. Abdul halim ndie aliemfata yule jamaa wa IC kwa ajili ya kuyamaliza ya uwanjani , jamaa wa IC akakataa na ku react, na hapo ndipo action ya Abdul halim ilipoaanza na ikabidi refa aingilei kati.

By the way Abdul halim alicheza vizuri sana katika mechi ile na ni vyema tukawajenga wachezaji wadogo kama wale badala ya kuwakatisha tamaaa. ni vyema tukaiangalie tena ile mechi.
 
Basi miye kweli mshamba;
Kwa kweli nilivyouangalia ule mpira, aliyenikera ni yule mkodivaa ambaye baada ya kupewa mkono (baada ya foul) alimsukuma abdulhalim... Baada ya mpira kwisha, abdulhalim alikwenda kumpa mkono tena mkodivaa na akasukumwa; nikachukia sana na sikuwa peke yangu...

kuhusu yale mahojiano, i thought the guy was fired up na majibu ya kusema kwani wao waweze wana nini na sisi tushindwe tuna nini ni inspirational kuliko majisifu ya kijinga!!

KWakweli, mimi binafsi nampongeza abdulhalim kwa kucheza vizuri sana sehemu ya kiungo na kwa kuwa fired up all the game, tukumbuke kwamba kuna wachezaji bila ule munkari mpira hauendi, akina Gazza, Gatusso, Gerrad, Roy Keane etc. Siwezi kumlinganisha abdulhalim na Nyosso au Mrwanda... hawana nidhamu

Kama mliona tofauti basi ni mtazamo na cha maana ni kiumsaidia abdulhalim kwani ana potentials zote kama walizokuwa nazo akina Gaga kwenye soka la bongo afike mbali zaidi, ana height, physique, pace, control, stamina, pace nk

Lets go positive japo kwa dakika!!
 
Dogo hakuwa na kosa jamaa wa IC walikuwa wanaringa sana na walicheza ili wasiumie.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom