Mchezaji Gerald Mdamu inadaiwa kutelekezwa na Polisi Tanzania baada ya kupata ajali; Ni aibu Tafadhali IGP ingilia kati

Mdamu anatia huruma, aomba msaada wa Watanzania​


mdamu pic


STRAIKA wa Polisi Tanzania, Mathias Mdamu aliyevunjika miguu yote katika ajali iliyotokea hivi karibuni timu yake ikitokea mazoezini mjini Moshi anatia huruma. Amewaambia Watanzania kwa uchungu mkubwa huku akilia; “Naombeni mnisaidie, hali yangu mbaya.” Mdamu alihamishiwa kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam akitokea KCMC -Moshi.

Akizungumza na Mwanaspoti kupitia simu ya kaka yake, Benedicto Mdamu(pichani kabla ya ajali) alitamka maneno mazito yaliyoambatana na kilio kisha alishindwa kuendelea kuzungumza. “Nawaomba Watanzania kwa upendo wao, huruma zao, wanione na mimi kama wanavyowaona wengine ili nisaidiwe nitibiwe, lakini kama kilio changu kitamfikia na mama yangu Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan anikumbuke mtoto wake ili nitibiwe kwa uharaka,” alisema huku akilia kwa uchungu na kaka yake akimtuliza na kumwambia amtumaini Mungu.

Awali Polisi wenyewe kupitia kwa Robert Munisi alidai kushangazwa na malalamiko yanayoibuka kila kukicha huku akisisitiza kwamba walihusika kumhamisha mchezaji huyo kutoka Moshi kwenda Dar na wanawasiliana na Mkewe kila mara kutoa msaada kwavile aliumia akiwa kazini. Mdamu ambaye ana watoto wawili Bryson (6) na Julian ambaye ni mchanga hajui hatima yao endapo kama atakosa matibabu ya haraka.

Straika huyo yupo na ndugu zake wa karibu ambao wanaweka wazi kuhitaji msaada wa hali na mali kutoka kwa familia ya soka nchini, ili atibiwe haraka kabla mambo hayajaenda kombo.

Benedicto anayemuuguza Mhimbili, ameeleza wanavyopitia wakati mgumu, huku mdogo wake akionekana kukata tamaa na kutoelewa hatima yake.

Aliliambia Mwanaspoti kwamba gharama zinazotakiwa kila siku anajikuta wakati mwingine anashindwa kuzimudu na kufanya mdogo wake awe mtu wa kulia kila wakati, huku akijiona hana thamani tena mbele ya uso wa dunia.

“Nitoe wito kwa wachezaji, makocha na wadau wa soka mbalimbali atakayeguswa na chochote amsaidie mdogo wangu ili aweze kutibiwa kwa haraka kabla ya mambo kuendelea kuwa mabaya, maana muda unavyokwenda ndivyo anavyojisikia vibaya,” alisema.

“Bora niwe muwazi ili asaidiwe, najua kuna wachezaji ambao wataguswa na kama wanataka kuamini wanaweza wakaja kujionea wenyewe, sijui hata niseme nini hata kama kuna kiongozi atasikia kilio changu naomba atusaidie na Mungu atambariki.”

MKE ATOA NENO

Mkewe Mdamu aliyejitambulisha kwa jina la Julian Marekela licha ya kuongea kwa hofu na huzuni kubwa alizungumza machache na kuwaomba Watanzania wamsaidie mumewe apone.“Naomba msaada ili mume wangu atibiwe kwa haraka maana ana hali mbaya, sijui hata nifanye nini,” kisha akakata simu na kuendelea kulia kwa uchungu.

BARAZA AMSIKITIKIA

Kocha Francis Baraz ambaye aliwahi kumfundisha Mdamu timu ya Biashara United kabla hajahamia Polisi Tanzania, alisikitishwa na hali yake.

“Nimemfundisha nikiwa Biashara United, zilinishtusha sana taarifa zake, Mdamu alikuwa na ndoto kubwa sana katika soka, naamini ipo siku zitatimia,” alisema.

Kwa yeyote ambaye atapenda kumsaidia Mdamu awasiliane kwa simu ya kaka yake namba 0714 - 716843.
Kwamba mchezaji wa ligi kuu hana bima ya afya?
Kwamba hamjui akili ZA polisi ni hamnazo
 
Kutokana na maelezo ya Ndugu yake anayemuuguza Moi, inasikitisha - yawezekana kijana si kucheza mpira tu bali anaweza hata asitembee tena.

Watanzania tumsaidie kijana huyu hata ikibidi akatibiwe nje ya nchi haraka, tusiache ndoto yake ikapotea hivi hivi.
 
Kama polisi Tanzania inawatekelezaga askari wake linapokuja suala la pesa litaacha kumtelekeza huyo raia? Majitu yaliyokaa kwenye nafasi za juu za hilo jeshi ni mabinafsi, roho mbaya, tamaa kama vile hayapokei mishahara, ukiyaona yalivyonenepeana utafikiri kitimoto
 

Mdamu anatia huruma, aomba msaada wa Watanzania​


mdamu pic


STRAIKA wa Polisi Tanzania, Mathias Mdamu aliyevunjika miguu yote katika ajali iliyotokea hivi karibuni timu yake ikitokea mazoezini mjini Moshi anatia huruma. Amewaambia Watanzania kwa uchungu mkubwa huku akilia; “Naombeni mnisaidie, hali yangu mbaya.” Mdamu alihamishiwa kwenye Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam akitokea KCMC -Moshi.

Akizungumza na Mwanaspoti kupitia simu ya kaka yake, Benedicto Mdamu(pichani kabla ya ajali) alitamka maneno mazito yaliyoambatana na kilio kisha alishindwa kuendelea kuzungumza. “Nawaomba Watanzania kwa upendo wao, huruma zao, wanione na mimi kama wanavyowaona wengine ili nisaidiwe nitibiwe, lakini kama kilio changu kitamfikia na mama yangu Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan anikumbuke mtoto wake ili nitibiwe kwa uharaka,” alisema huku akilia kwa uchungu na kaka yake akimtuliza na kumwambia amtumaini Mungu.

Awali Polisi wenyewe kupitia kwa Robert Munisi alidai kushangazwa na malalamiko yanayoibuka kila kukicha huku akisisitiza kwamba walihusika kumhamisha mchezaji huyo kutoka Moshi kwenda Dar na wanawasiliana na Mkewe kila mara kutoa msaada kwavile aliumia akiwa kazini. Mdamu ambaye ana watoto wawili Bryson (6) na Julian ambaye ni mchanga hajui hatima yao endapo kama atakosa matibabu ya haraka.

Straika huyo yupo na ndugu zake wa karibu ambao wanaweka wazi kuhitaji msaada wa hali na mali kutoka kwa familia ya soka nchini, ili atibiwe haraka kabla mambo hayajaenda kombo.

Benedicto anayemuuguza Mhimbili, ameeleza wanavyopitia wakati mgumu, huku mdogo wake akionekana kukata tamaa na kutoelewa hatima yake.

Aliliambia Mwanaspoti kwamba gharama zinazotakiwa kila siku anajikuta wakati mwingine anashindwa kuzimudu na kufanya mdogo wake awe mtu wa kulia kila wakati, huku akijiona hana thamani tena mbele ya uso wa dunia.

“Nitoe wito kwa wachezaji, makocha na wadau wa soka mbalimbali atakayeguswa na chochote amsaidie mdogo wangu ili aweze kutibiwa kwa haraka kabla ya mambo kuendelea kuwa mabaya, maana muda unavyokwenda ndivyo anavyojisikia vibaya,” alisema.

“Bora niwe muwazi ili asaidiwe, najua kuna wachezaji ambao wataguswa na kama wanataka kuamini wanaweza wakaja kujionea wenyewe, sijui hata niseme nini hata kama kuna kiongozi atasikia kilio changu naomba atusaidie na Mungu atambariki.”

MKE ATOA NENO

Mkewe Mdamu aliyejitambulisha kwa jina la Julian Marekela licha ya kuongea kwa hofu na huzuni kubwa alizungumza machache na kuwaomba Watanzania wamsaidie mumewe apone.“Naomba msaada ili mume wangu atibiwe kwa haraka maana ana hali mbaya, sijui hata nifanye nini,” kisha akakata simu na kuendelea kulia kwa uchungu.

BARAZA AMSIKITIKIA

Kocha Francis Baraz ambaye aliwahi kumfundisha Mdamu timu ya Biashara United kabla hajahamia Polisi Tanzania, alisikitishwa na hali yake.

“Nimemfundisha nikiwa Biashara United, zilinishtusha sana taarifa zake, Mdamu alikuwa na ndoto kubwa sana katika soka, naamini ipo siku zitatimia,” alisema.

Kwa yeyote ambaye atapenda kumsaidia Mdamu awasiliane kwa simu ya kaka yake namba 0714 - 716843.
Kwanza nampa pole nyingi sana Mchezaji Gerald Mathias Mdamu kwa Kilichotokea na anachokipitia sasa. Naamini Mwenyezi Mungu atampigania, atamtia Nguvu na Kumfuta Machozi na Machungu yake.

Pili nadhani pamoja Jambo Kuu na la Msingi analolihitaji Mchezaji Gerald Mathias Mdamu kuwa hiyo Tiba ya haraka lakini anahitaji upesi sana Psychological Counseling kwani nilichogundua Kinachomtesa huyu Mchezaji ni Kuambiwa kuwa anatakiwa akatwe Miguu yote Mawili kutokana na jinsi alivyoumia vibaya mno.

Tatu natambua Juhudi za Nduguze na hasa Mkewe ( pamoja na Dada yake mkubwa Rebecca ) za Kumpambania Mpendwa wao Mchezaji Gerald Mathias Mdamu ila kuna Kitu si Kizuri nimekigundua baina ya hawa Ndugu zake na Ugonjwa wa Mchezaji husika.

Taarifa nilizonazo GENTAMYCINE ni kwamba Mchezaji husika Gerald Mathias Mdamu huenda kwa Kuwajua Ndugu zake walivyo aliomba Mawasiliano yake yoyote ( hasa yahusuyo Pesa ) yapitie kwa Mkewe tu na wala si hawa Ndugu zake wengine wanaohangaika Redioni, Runingani na katika Mitandao ya Kijamii.

Nne kwa mtazamo wangu ninachokiona sasa ni kama vile Ndugu wa Mchezaji Gerald Mathias Mdamu ni kama vile wanataka Kuutumia huu Ugonjwa wa Ndugu yao sehemu Kuu ya Kujipatia Kipato na hata Mtaji wa Biashara na sasa wameshamuingiza Mke wa Mchezaji katika Mtego wao na sasa wanampelekesha watakavyo na Kuwasikiliza wao.

Tano leo hii tukisema kuwa Jeshi la Polisi limemtelekeza Mchezaji wa Polisi Tanzania Gerald Mathias Mdamu na kwamba halijatoa ( halitoi ) Ushirikuano wowote ule Kwake tutakuwa tunajitafutia Laana mbaya kwa Mwenyezi Mungu na kuwa Wazushi na Waongo.

Taarifa za uhakika nilizonazo zinasema kwamba ni Jeshi la Polisi ndiyo limetoa AMBULANCE ya Kumsafirisha Mchezaji Gerald Mathias Mdamu kutoka Hospitali ya KCMC Kilimanjaro kuja Muhimbili ( MOI ) Dar es Salaam kwa Gharama za Tsh 1,400,00/= Kamili.

Mchezaji Gerald Mathias Mdamu bado ana Mkataba na Jeshi la Polisi na hata Mshahara wake anaupokea kama Kawaida. Baada ya Kufikishwa hapo Muhimbili ( MOI ) bado Gharama za Vipimo na Chakula kwa wanaomuangalia Jeshi la Polisi linawapa ja pia kuna Daktari wa Jeshi la Polisi yupo hapo MOI ( Muhimbili ) ili kusaidia Matibabu yake.

Je, kwa huu Uungwana wa Jeshi la Polisi uliomfanyia Mchezaji Gerald Mathias Mdamu nao ( Jeshi la Polisi ) hawastahili pongezi nyingi kutoka Kwetu na badala yake tunaonyesha Chuki zetu Kwao labda kwa sababu zetu tu za Itikadi ya Vyama na Matukio ya nyuma?

Je, hawa Ndugu kuanzia Mke wa Mchezaji Gerald Mathias Mdamu ( aishiye Dar es Salaam ) huyo Kaka na Dada yake wamemsaidia lipi la Gharama Ndugu yao huyo zaidi ya Kulia na Kulaumu tu?

Na GENTAMYCINE siko hapa labda Kuwatetea Jeshi la Polisi ila nataka kama Binadamu na Waungwana tuwe 'Fair' katika hili na sasa Kipaumbele chetu kiwe ni Kushikamana na Kuhamasishana huku na kule ili Mchezaji Gerald Mathias Mdamu apatiwe Tiba na ikiwezekana apone kabisa na siyo Kulumbana kwani haisaidii ( haitosaidia ) na tukumbuke Sisi tunalumbana tu ila Mchezaji Yeye anazidi Kuumia na Kuteseka hasa Kisaikolojia.

Na bahati nzuri Baba Mzazi wa Mchezaji Gerald Mathias Mdamu ni Askari Polisi Mstaafu hivyo taratibu zote za Kipolisi na Kiserikali hasa katika Suala la Tiba na Kuuguza anazijua na nasikia ndiyo anamhangaikia zaidi Mwanae akishirikiana na Waandamizi wa Polisi pamoja na Timu yake ya Polisi Tanzania.

Namwombea Mchezaji Gerald Mathias Mdamu kwa Mwenyezi Mungu apate Msaada na Ushirikuano mkubwa kisha apone na arejee katika Majukumu yake ( kama ikiwezekana ) ila tafadhali akipewa Ushauri wa Kitabibu wa Kukatwa Miguu yote miwili ( Kitu ambacho Yeye hataki na hapendi Kukusikia ) namwomba akubali tu kwani Ulemavu siyo Kufa.
 
Hii taasisi imejaa utapeli sana,si kwa watumishi wake askari wala raia.

Ulikuwa uchaguzi mbaya sana kwa huyu jamaa kuamua kuitumikia.
 
Kuna watangazaji fulani viherehere wa vipindi vya michezo,naona kama washaanza pitisha mabakuli

Ova
 
Hayo majibu ya jeshi letu kwa raia ndg wa dada yanatosha kabisa kujua who's..!
 
Back
Top Bottom