Mchemsho wa kwanza wa Zuma

fiksiman

JF-Expert Member
May 17, 2008
402
104
Huku akionekana kuwa ni Rais mwenye kuaminika na kuleta ari mpya miongoni mwa wanyonge wa Nchi ya Afrika Kusini, hatimaye Jacob Zuma ameibuka kidedea kwenye uchaguzi mkuu na sasa anakaribia kutawazwa kuwa Rais Mpya wa Taifa lenye nguvu Afrika.

Hata hivyo, safari yake imeanza kuingiwa na dosari baada ya kutoa mwaliko kwa Rais "wanted" na Mahakama ya Kimataifa, Alhaji Omari Al Bashir wa Sudan ambaye amewekewa RB ya kukakwamata kwa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya Ubinadanu. Zuma amemwalika Bashir katika sherehe za kuapishwa kwake pamoja na kutambua kuwa anatafutwa kwa udi na uvumba na Jumuiya hiyo.

Msemaji wa Serikali ya Afrika Kusini, Bwana Themba Maseko amethibitisha kualikwa kwa Rais huyo pamoja na wakuu kadhaa wa Nchi za Afrika japo uwepo wake umeshauriwa usiwepo ili kuepusha mahusiano mabaya na Jumuyia za kimataifa

Afrika Kusini ni miongoni mwa nchi zilizotia saini makubaliano ya Rome juu ya uwepo wa Mahakama hiyo na italazimika kumkamata kiongozi huyo wa Sudan endapo atatia mguu katika ardhi hiyo. Swali je kwanini wamemualika wakijua hali halisi ya Kiongozi huyo?

Huu watoto wa uswahili huuita MCHESHO WA HALI YA JUU.
 
Zuma hawezi kuchemsha, kwani alishafikia boiling point kabla hata ya kuchaguliwa kuwa rais.

Zitakazofuata ni mbwembwe tu. I hope the Rand can stand.
 
Zuma hawezi kuchemsha, kwani alishafikia boiling point kabla hata ya kuchaguliwa kuwa rais.

Zitakazofuata ni mbwembwe tu. I hope the Rand can stand.
Binafsi siamini Zuma atafanya lolote jipya, hii ni imani tu... Kuna watu wana imani SANA naye, nimekuwa nikisoma Economist naona wadau kibao wanampa 'shavu' sana, ngoja tummulike tuone walau mwaka mmoja atakuwa na mafanikio kiasi gani.
 
Nami nawaonea huruma sana wa south africa....wanadhania kutatokea mabadiliko hasa ya uchumi wa mifukoni mwa watu wa hali ya chini...sasa akifikisha 3 yrs hakuna lolote kama muuza sura wetu utasikia.....maandamano na machafuko...mpeni muda mtamsikia atakavyotolewa...mimi namfanananisha na idd amain dada ki sera hasa za kufufua uchumi wa wazalendo wa hali chini najua hana lolotee.....ni uzawa na mwenzetu ideology ndio zinazompa kichwa atatulia mwenyewe muache
 
Nami nawaonea huruma sana wa south africa....wanadhania kutatokea mabadiliko hasa ya uchumi wa mifukoni mwa watu wa hali ya chini...sasa akifikisha 3 yrs hakuna lolote kama muuza sura wetu utasikia.....maandamano na machafuko...mpeni muda mtamsikia atakavyotolewa...mimi namfanananisha na idd amain dada ki sera hasa za kufufua uchumi wa wazalendo wa hali chini najua hana lolotee.....ni uzawa na mwenzetu ideology ndio zinazompa kichwa atatulia mwenyewe muache


Skills,

Kuna kitu kuhusu Zuma kinatukumbusha Idd Amin, hata mimi kabala hujaandika hapa nikasema jamaa ananikumbusha Idd Amin, lakini nikasema si sawa kumlinganisha na Idd Amin kwa sababu hajaua watu wengi.

Lakini the buffoonery, the disregard for diplomacy, the simpleton approach, the militancy, the populism and even the philandering is remarkably similar.
 
kwani nani alisema kuwa tamko likitoka ICC linaridhiwa na ulimwengu mzima? Bush akiwapiga waarabu mbona hakupelekwa ICC? Ni suala zima la maslahi tu. Wanaoiharibu Sudan ni wachina na hao wamarekani hadi Bashir anapata kizungux2 na kubakia kumalizia hasira kwa wabantu wenzake. Tuombe tu hizo mbwembwe na mvuto wa Xuma vikayeyuka kama kwa Jakaya
 
Tusubiri first lady tuone kituko kingine pia.....!

Zuma's two wives, two fiancées and daughter are all currently eligible to snatch the prestigious role of South Africa's "First Lady", following the victory of the African National Congress (ANC) in the country's general elections held on April 22.

The South African Parliament is expected to elect Jacob Zuma, the leader of the ANC, into the highest office on May 6. But that is not what South Africans are really waiting for… Suspense is fever high as the identity of the first lady is kept under wraps. Many traditions in Africa give impetus to all men alike to practice polygamy. Zulu men are not known to be wife-shy in the least. And Jacob Zuma, the dashing sixty-something-year-old, nicknamed "pants of love" in Zulu is a great follower of traditions. He loves to get married - albeit traditional his numerous marriages are legally binding.

Out of four or so marriages, two or so of his wives are still married to him. He married his first wife, Sizakele Khumalo, in 1973, 14 years after they had begun courting (1959). Sizakele lives in their home in KwaZulu Natal, where she takes care of her husband's numerous children. According to sources, they (the children) number between 17 and 18. Sizakele, however, is childless. According to the South African constitution, which recognizes the legality of polygamy, she is to become first lady. However, Zuma's childhood sweetheart f, "(his) wife - (his) sister - (his) lover - (his) mother" as he says, is frightfully shy.

The solid Sizakele Khumalo Jacob Zuma later married Kate Mantsho, in what seems to have been a rather sad and unhappy marriage. Kate Mantsho took her life in 2000. In a suicide letter she left behind, she said married to Zuma was "24 years of hell". She is survived by five children.

Nkosazana Dlamini-Zuma, Minister of Foreign Affairs in Thabo Mbeki's government, was the third wife of the president-in-waiting. A completely emancipated woman, Nkosazana Dlamini filed for divorce in 1998. Word has it that she has been on good terms with her former husband and father of her four children and is likely to collaborate, politically, with him. Zuma initiated Nkosazana Dlamini into the world of politics. The last of Zuma's four official wives is known as Nompumelelo Ntuli. They married in 2008. About thirty years his junior, she basks in public appearances, a necessary quality if she wants to be the first lady of South Africa - a role that others are seriously considering.

At least, it is the case of Thobeka Mabhija, who the Sunday Times announced as the future "First lady". She is reported to have immediately distanced herself from those claims. According to sources, Jacob Zuma paid a dowry in January to make the 35 year-old woman his fifth wife. Thobeka, reportedly, has two children with Zuma. Their last child is less than a year old.

Another potential bride or first lady is Bongi Nguema. Their relationship, which was confirmed by Zuma's brother, Michael, has already given fruit to a son. Jacob Zuma has the last word Jacob Zuma, once boldly said in a television interview that he "loves" his "wives" and that he is "proud" of his "children".

But for now, chosing one of his children to become first lady could indeed deal with the headache of finding the right wife to take on the role without having to explain himself to his other wives. 26 years and a fervent supporter of her father, Dudzile Zuma, who testified on Zuma's behalf during his rape trial in 2006, could be the lucky one. Not the first In fact, this is not the first time that South Africans would be faced with such a situation. After his divorce from Winnie Mandela, and before his marriage to Graça Machel, Nelson Mandela, South Africa's first black president, in 1994 invited one of his daughters, Zinzi, to take on the role.

According to his close relations, Jacob Zuma reserves the right to choose his "first lady". Unless of course, like the young Phindile Mbatha, a petty trader at the Eshowe market, close to Zuma's village, there is no need for a first lady. Phindile who thought Zuma's third wife, Dlamini-Zuma, is best suited for the role changed her mind when she learned they were Divorced. "Maybe the country does not really need one after all," she said. Jacob Zuma would not be the first President to forgo this protocol. Just like heads of governments from Saudi Arabian and the United Arab Emirates, a first lady is indeed not compulsory.
 
Last edited by a moderator:
Imani yangu ni kuwa Zuma hatakuwa na lolote kwa SA, kama ambavyo niliamini kuwa JK asingekuwa na lolote kwa Tanzania tangu walipomchagua chimwaga.
Wasouth wajiandae!
 
Nami nawaonea huruma sana wa south africa....wanadhania kutatokea mabadiliko hasa ya uchumi wa mifukoni mwa watu wa hali ya chini...sasa akifikisha 3 yrs hakuna lolote kama muuza sura wetu utasikia.....maandamano na machafuko...mpeni muda mtamsikia atakavyotolewa...mimi namfanananisha na idd amain dada ki sera hasa za kufufua uchumi wa wazalendo wa hali chini najua hana lolotee.....ni uzawa na mwenzetu ideology ndio zinazompa kichwa atatulia mwenyewe muache

miaka mitatu yote hiyo?! SA ni bomu linalosubiri kulipuka, tena si ajabu kabla hata ya kombe la dunia! wale sio "wavumilivu" kama "sisi"!
ngoja tusikilizie.
 
Tusubiri first lady tuone kituko kingine pia.....! Zuma’s two wives, two fiancées and daughter are all currently eligible to snatch the prestigious role of South Africa’s "First Lady", following the victory of the African National Congress (ANC) in the country’s general elections held on April 22. The South African Parliament is expected to elect Jacob Zuma, the leader of the ANC, into the highest office on May 6. But that is not what South Africans are really waiting for… Suspense is fever high as the identity of the first lady is kept under wraps. Many traditions in Africa give impetus to all men alike to practice polygamy. Zulu men are not known to be wife-shy in the least. And Jacob Zuma, the dashing sixty-something-year-old, nicknamed "pants of love" in Zulu is a great follower of traditions. He loves to get married — albeit traditional his numerous marriages are legally binding. Out of four or so marriages, two or so of his wives are still married to him. He married his first wife, Sizakele Khumalo, in 1973, 14 years after they had begun courting (1959). Sizakele lives in their home in KwaZulu Natal, where she takes care of her husband’s numerous children. According to sources, they (the children) number between 17 and 18. Sizakele, however, is childless. According to the South African constitution, which recognizes the legality of polygamy, she is to become first lady. However, Zuma’s childhood sweetheart f, "(his) wife - (his) sister - (his) lover - (his) mother" as he says, is frightfully shy. The solid Sizakele Khumalo Jacob Zuma later married Kate Mantsho, in what seems to have been a rather sad and unhappy marriage. Kate Mantsho took her life in 2000. In a suicide letter she left behind, she said married to Zuma was "24 years of hell". She is survived by five children. Nkosazana Dlamini-Zuma, Minister of Foreign Affairs in Thabo Mbeki’s government, was the third wife of the president-in-waiting. A completely emancipated woman, Nkosazana Dlamini filed for divorce in 1998. Word has it that she has been on good terms with her former husband and father of her four children and is likely to collaborate, politically, with him. Zuma initiated Nkosazana Dlamini into the world of politics. The last of Zuma’s four official wives is known as Nompumelelo Ntuli. They married in 2008. About thirty years his junior, she basks in public appearances, a necessary quality if she wants to be the first lady of South Africa — a role that others are seriously considering. At least, it is the case of Thobeka Mabhija, who the Sunday Times announced as the future "First lady". She is reported to have immediately distanced herself from those claims. According to sources, Jacob Zuma paid a dowry in January to make the 35 year-old woman his fifth wife. Thobeka, reportedly, has two children with Zuma. Their last child is less than a year old. Another potential bride or first lady is Bongi Nguema. Their relationship, which was confirmed by Zuma’s brother, Michael, has already given fruit to a son. Jacob Zuma has the last word Jacob Zuma, once boldly said in a television interview that he “loves” his “wives” and that he is “proud” of his “children”. But for now, chosing one of his children to become first lady could indeed deal with the headache of finding the right wife to take on the role without having to explain himself to his other wives. 26 years and a fervent supporter of her father, Dudzile Zuma, who testified on Zuma’s behalf during his rape trial in 2006, could be the lucky one. Not the first In fact, this is not the first time that South Africans would be faced with such a situation. After his divorce from Winnie Mandela, and before his marriage to Graça Machel, Nelson Mandela, South Africa’s first black president, in 1994 invited one of his daughters, Zinzi, to take on the role. According to his close relations, Jacob Zuma reserves the right to choose his "first lady". Unless of course, like the young Phindile Mbatha, a petty trader at the Eshowe market, close to Zuma’s village, there is no need for a first lady. Phindile who thought Zuma’s third wife, Dlamini-Zuma, is best suited for the role changed her mind when she learned they were Divorced. "Maybe the country does not really need one after all," she said. Jacob Zuma would not be the first President to forgo this protocol. Just like heads of governments from Saudi Arabian and the United Arab Emirates, a first lady is indeed not compulsory.


Ayafanyayo Zuma hata viongozi wetu wanafanya ila wanadhani wanafanya siri huku mtaani wanaonekana. Nyumba ndogo na watoto kibao mtaani, tena wengine na wake za watu, na wala mila haziwaruhusu kama ilivyo kwa Zuma. Waliosema he is not responsible sababu alifanya ngono zembe na yule dada tena mwenye HIV - kwani ni wangapi, wasomi wanafanya hayo hayo. Simtetei ila tusimnyanyulie bango.
 
Naona Fiksiman umetumia lugha ya mama Siphia Simba ya 'fulani kuchemsha'. Rais Zuma na Serikali ya Afrika ya Kusini haijachemsha kumwalika Rais Al-Bashir wa Sudan.

Mahakama ya Kimataifa ya ICC inafanya kazi katika nchi zilizosaini kukubali uwepo wake. Nchi kama vile Marekani, Israel na Sudan hazijasaini mkataba huo. Marekani na Israel zinapinga kabisa uwepo wa mahakama hiyo, na kwa taarifa yako Marekani imepitisha sheria inayomlazimu Rais wa Marekani kutumia nguvu za kijeshi dhidi ya Mahakama hiyo iwapo raia yeyote wa Marekani atakuja kukamatwa na Mahakama hiyo, ili kukomboa raia wake.

ila ironically ni kuwa kwa kuwa Marekani inataka kutawala kabisa dunia, inaendeleza hegemony na regime change, ndio maana wote ambao wamekamatwa na mahakama hiyo na kushtakiwa ni wale wanaopingwa na Marekani, kama marehemu Rais Milosevic wa Yugoslavia/Serbia aliyepinga kugawanywa kwa Yugoslavia ambayo Marekani ilitaka igawanywe iwe nchi nyingi(divide & rule tactics), Charles Taylor wa Liberia ambaye kosa lake kubwa ni kumshinda kwenye uchaguzi wa urais kipenzi cha wamarekani Mama Ellen Johnson-Sirleaf (ambaye hatimaye naye sasa kawa rais).

Marekani inashawishi Mahakama hiyo iwakamate maadui zake, lakini wenyewe na marafiki zake wala hawaguswi. Wangekakatwa viongozi wa Israel toka enzi Ariel Sharon alipokuwa Waziri wa Ulinzi ashitakiwe kwa mauaji ya wakimbizi kwenye kambi za Sabra na Shatila huko Lebanon, hadi aliyeondioka madarakani Ehud Olmert kwa mauaji huko Gaza. Huko West Bank pamoja na kuwa wanyonge na watiifu kwa 'Occupiers' badi wanauawa na mnyonge/kibaraka Mahmoud Abbas anaangalia tu, ndio maana ana-lose support ya watu kwenye uchaguzi. Huyo ICC prosecutor Ocampo aliulizwa mbona hatoi indictment kwa Ehud Olmert na Ehud Barak ili wakamatwe akajibu kuwa eti itaharibu Peace Process, what a shame! Mbona Sudan/Darfur kuna Peace process nako? Mbona ametoa indictment?

ICC inatakiwa kukataliwa na wapenda usawa na wapinga unyonyaji wote duniani. Hiyo mahakama inatumika kisiasa na wala siyo kisheria. Hata siku moja hutasikia kiongozi wa nchi rafiki na Marekani amekamatwa.

Turudi kwa Zuma. Tatizo ni kuwa wengi wetu ni wavivu wa kufikiri, tunataka tutafuniwe habari na Western-oriented media, na hivyo tunaziamini. Rais Jacob Zuma hapendwi na kile kinachoitwa na Western Media kuwa ni 'business community', yaani tabaka la wafanyabiashara. Hii ni kwa sababu ana support kubwa kutoka kwa watu wa tabaka la chini na wafanyakazi pamoja na vyama vyao (labour unions). Hiyo business community ilimpenda sana Rais wa zamani Thabo Mbeki, ndio maana wamesikitika, walitamani Mbeki angefanikiwa kumpachika mtu anayemtaka yeye ili awatumikie wao (business community).

Zuma anasema ataweka mbele maslahi wa wengi, ambao kwa miaka 15 iliyopita hawajapata matunda ya ukombozi. Watu wanataka social improvement kwa maana nyumba bora, huduma za maji, umeme, mashule, barabara, maslahi zaidi kazini etc., na ndio mkazo wa Zuma. Hilo la maslahi ndio linawatia tumbo joto wawekezaji na media zao.

For the west and the business community, anyone pro-them is ok, whether democratically elected or not, be Middle-Eastern Emirs & Sultans, Museveni, Mkapa/JK, Kibaki etc.

Wake up Afrika! Free yourself from the yoke of both the internal & external colonialism.
 
Naona Fiksiman umetumia lugha ya mama Siphia Simba ya 'fulani kuchemsha'. Rais Zuma na Serikali ya Afrika ya Kusini haijachemsha kumwalika Rais Al-Bashir wa Sudan.

Mahakama ya Kimataifa ya ICC inafanya kazi katika nchi zilizosaini kukubali uwepo wake. Nchi kama vile Marekani, Israel na Sudan hazijasaini mkataba huo. Marekani na Israel zinapinga kabisa uwepo wa mahakama hiyo, na kwa taarifa yako Marekani imepitisha sheria inayomlazimu Rais wa Marekani kutumia nguvu za kijeshi dhidi ya Mahakama hiyo iwapo raia yeyote wa Marekani atakuja kukamatwa na Mahakama hiyo, ili kukomboa raia wake.

ila ironically ni kuwa kwa kuwa Marekani inataka kutawala kabisa dunia, inaendeleza hegemony na regime change, ndio maana wote ambao wamekamatwa na mahakama hiyo na kushtakiwa ni wale wanaopingwa na Marekani, kama marehemu Rais Milosevic wa Yugoslavia/Serbia aliyepinga kugawanywa kwa Yugoslavia ambayo Marekani ilitaka igawanywe iwe nchi nyingi(divide & rule tactics), Charles Taylor wa Liberia ambaye kosa lake kubwa ni kumshinda kwenye uchaguzi wa urais kipenzi cha wamarekani Mama Ellen Johnson-Sirleaf (ambaye hatimaye naye sasa kawa rais).

Marekani inashawishi Mahakama hiyo iwakamate maadui zake, lakini wenyewe na marafiki zake wala hawaguswi. Wangekakatwa viongozi wa Israel toka enzi Ariel Sharon alipokuwa Waziri wa Ulinzi ashitakiwe kwa mauaji ya wakimbizi kwenye kambi za Sabra na Shatila huko Lebanon, hadi aliyeondioka madarakani Ehud Olmert kwa mauaji huko Gaza. Huko West Bank pamoja na kuwa wanyonge na watiifu kwa 'Occupiers' badi wanauawa na mnyonge/kibaraka Mahmoud Abbas anaangalia tu, ndio maana ana-lose support ya watu kwenye uchaguzi. Huyo ICC prosecutor Ocampo aliulizwa mbona hatoi indictment kwa Ehud Olmert na Ehud Barak ili wakamatwe akajibu kuwa eti itaharibu Peace Process, what a shame! Mbona Sudan/Darfur kuna Peace process nako? Mbona ametoa indictment?

ICC inatakiwa kukataliwa na wapenda usawa na wapinga unyonyaji wote duniani. Hiyo mahakama inatumika kisiasa na wala siyo kisheria. Hata siku moja hutasikia kiongozi wa nchi rafiki na Marekani amekamatwa.

Turudi kwa Zuma. Tatizo ni kuwa wengi wetu ni wavivu wa kufikiri, tunataka tutafuniwe habari na Western-oriented media, na hivyo tunaziamini. Rais Jacob Zuma hapendwi na kile kinachoitwa na Western Media kuwa ni 'business community', yaani tabaka la wafanyabiashara. Hii ni kwa sababu ana support kubwa kutoka kwa watu wa tabaka la chini na wafanyakazi pamoja na vyama vyao (labour unions). Hiyo business community ilimpenda sana Rais wa zamani Thabo Mbeki, ndio maana wamesikitika, walitamani Mbeki angefanikiwa kumpachika mtu anayemtaka yeye ili awatumikie wao (business community).

Zuma anasema ataweka mbele maslahi wa wengi, ambao kwa miaka 15 iliyopita hawajapata matunda ya ukombozi. Watu wanataka social improvement kwa maana nyumba bora, huduma za maji, umeme, mashule, barabara, maslahi zaidi kazini etc., na ndio mkazo wa Zuma. Hilo la maslahi ndio linawatia tumbo joto wawekezaji na media zao.

For the west and the business community, anyone pro-them is ok, whether democratically elected or not, be Middle-Eastern Emirs & Sultans, Museveni, Mkapa/JK, Kibaki etc.

Wake up Afrika! Free yourself from the yoke of both the internal & external colonialism.

...yote sawa lakini hakuna justification ya ujangiri wa Taylor or Bashir.
 
JK all over again. Inspire the masses then crash their hopes. Hawa viongozi wanaokuja kwa "nguvu mpya, ari mpya na kasi mpya" nawaogopa sasa. Anyways maybe he will do good, only time will tell.
 
Watu wanajiamini katika uongozi huwa hawasumbuliwi na nchi za magharbi na Marekani. Wakati wa Mandela alikuwa na uhusiano na Iran na Iraq, wakaanza kumlaumu, akawaambia kuwa Afrika ya Kusini haiwezi kuchaguliwa marafiki, wakati wa kudai kujikomboa toka kwa makaburu hizo nchi ziliwasaidia sasa iweje leo wasiwe marafiki zao. Uchumi ni kitu kimoja kizuri sana, ukitegemea sana kuomba unashindwa kuwa na misimamo. Hongera Zuma.
 
Huku akionekana kuwa ni Rais mwenye kuaminika na kuleta ari mpya miongoni mwa wanyonge wa Nchi ya Afrika Kusini, hatimaye Jacob Zuma ameibuka kidedea kwenye uchaguzi mkuu na sasa anakaribia kutawazwa kuwa Rais Mpya wa Taifa lenye nguvu Afrika.

Hata hivyo, safari yake imeanza kuingiwa na dosari baada ya kutoa mwaliko kwa Rais "wanted" na Mahakama ya Kimataifa, Alhaji Omari Al Bashir wa Sudan ambaye amewekewa RB ya kukakwamata kwa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya Ubinadanu. Zuma amemwalika Bashir katika sherehe za kuapishwa kwake pamoja na kutambua kuwa anatafutwa kwa udi na uvumba na Jumuiya hiyo.

Msemaji wa Serikali ya Afrika Kusini, Bwana Themba Maseko amethibitisha kualikwa kwa Rais huyo pamoja na wakuu kadhaa wa Nchi za Afrika japo uwepo wake umeshauriwa usiwepo ili kuepusha mahusiano mabaya na Jumuyia za kimataifa

Afrika Kusini ni miongoni mwa nchi zilizotia saini makubaliano ya Rome juu ya uwepo wa Mahakama hiyo na italazimika kumkamata kiongozi huyo wa Sudan endapo atatia mguu katika ardhi hiyo. Swali je kwanini wamemualika wakijua hali halisi ya Kiongozi huyo?

Huu watoto wa uswahili huuita MCHESHO WA HALI YA JUU.

Nafikiri walikuwa hawaja update contact book. LOL
 
Skills,
Lakini the buffoonery, the disregard for diplomacy, the simpleton approach, the militancy, the populism and even the philandering is remarkably similar.

Mi nadhani watu kama nyinyi ndo hammtendei haki Zuma. diplomacy gani kai disregard? Jamani huyu ni mtu pekee kasimama..kumnyoshea kidole Mugabe..ambako hata wengine waliogopa...in anycase...hajawahi kuwa na nafasi ya uraisi aweze kunyoshewa kidole (just deputy president with no clout in foreign affairs).

Zuma apewe mda. Period. Tuache hizi sentiments za kuwahukumu watu kutokana na kelele za CNN na BBC..its unfair mtu uko Tanzania au hata SA kwenyewe..unasoma editorial ya Washingtonpost au Economist..harafu unakuja hapa kumhukumu Zuma. Tuna haki ya kumuhukumu Kikwete kwa sababu tunaona madudu yake na sera zake...so is..Mbeki...What has Mbeki done? KAMA jamaa alivyoandika humu...Zuma aliomba kura kama wengine akashinda! alichaguliwa na hao hao waliomchagua Mbeki mara ya kwanza..na baadaye wakaona hafai..so Zuma akishindwa..basi watamtema. Ndo democrasia hiyo.

I am really tired kuona watu tunatoa hukumu kwa kuangalia editorials za wakubwa huko nje. Kama jamaa kafanya ujinga..ulete hapa tuujadili..ila siyo kiingereza kirefu cha CNN et al.

Kuhusu Zuma as a person..I respect his life. Kama aliamua kuoa wanawake 20..what has that got to do with us? It is him. Does that impair his ability to lead? Surely not. Hayo ni maamuzi binafsi. Ni kama same sex marriage..mbona "elites" wanazikubali? Zuma is a man not ashamed to be called an African! Wengi humu..tunachanganya ustaarabu wa kizungu na tamaduni zetu. Let the man do his things. Turudi hapa baada ya mwaka mmoja tuanze kuchambua utendaji wake.

Ndo maana mpaka leo nakubaliana na Zuma anaposema amehukumiwa na media. Maana jamaa hata mahakama ilimwachia huru..lakini watu wameamua ku-spin, kuspin..duh..you just ask what happened kwa hawa wahehimwa waliojipa madaraka ya kusimamia rule of law!
 
Mi nadhani watu kama nyinyi ndo hammtendei haki Zuma. diplomacy gani kai disregard? Jamani huyu ni mtu pekee kasimama..kumnyoshea kidole Mugabe..ambako hata wengine waliogopa...in anycase...hajawahi kuwa na nafasi ya uraisi aweze kunyoshewa kidole (just deputy president with no clout in foreign affairs).

Zuma apewe mda. Period. Tuache hizi sentiments za kuwahukumu watu kutokana na kelele za CNN na BBC..its unfair mtu uko Tanzania au hata SA kwenyewe..unasoma editorial ya Washingtonpost au Economist..harafu unakuja hapa kumhukumu Zuma. Tuna haki ya kumuhukumu Kikwete kwa sababu tunaona madudu yake na sera zake...so is..Mbeki...What has Mbeki done? KAMA jamaa alivyoandika humu...Zuma aliomba kura kama wengine akashinda! alichaguliwa na hao hao waliomchagua Mbeki mara ya kwanza..na baadaye wakaona hafai..so Zuma akishindwa..basi watamtema. Ndo democrasia hiyo.

I am really tired kuona watu tunatoa hukumu kwa kuangalia editorials za wakubwa huko nje. Kama jamaa kafanya ujinga..ulete hapa tuujadili..ila siyo kiingereza kirefu cha CNN et al.

Kuhusu Zuma as a person..I respect his life. Kama aliamua kuoa wanawake 20..what has that got to do with us? It is him. Does that impair his ability to lead? Surely not. Hayo ni maamuzi binafsi. Ni kama same sex marriage..mbona "elites" wanazikubali? Zuma is a man not ashamed to be called an African! Wengi humu..tunachanganya ustaarabu wa kizungu na tamaduni zetu. Let the man do his things. Turudi hapa baada ya mwaka mmoja tuanze kuchambua utendaji wake.

Ndo maana mpaka leo nakubaliana na Zuma anaposema amehukumiwa na media. Maana jamaa hata mahakama ilimwachia huru..lakini watu wameamua ku-spin, kuspin..duh..you just ask what happened kwa hawa wahehimwa waliojipa madaraka ya kusimamia rule of law!

Tuache uvivu wa kufuatilia mambo jamani..hili suala liko wazi mbona, zuma kamwalika Omari Bashir na hii inamaana moja tu, hakubaliani na tamko la mahakama ya kimataifa...kumbuka SA haikushikiwa BAKORA kusaini uanachama wa jumuiya hiyo. Sasa we huoni kama kayumba kwa kwenda kinyume. Unataka kutuambia kuwa vyombo vya habari vya nje vimedanganya suala hili au ndo tuseme kukurupuka kimtazamo??? Mi kwa mtazamo wangu kinachoendelea afrika na dunia ni lazima tufuatilie kwani inaweza kuleta athari kwetu pia, kumbuka Tanzania si kisiwa kiasi inyamazie masuala yanayoendelea kwa wenzetu.
 
Nyie mnategemea nini kwa Zuma? Hao ndio watu anaojidentify nao.......majambazi wenzie wanyanyasaji wa kijinsia n.k.nahitaji kuseam zaidi? Ila sasa kwa kutokuona mbali hatambui implications za hatua hiyo kidiplomasia!

Jamani yaani viongozi tunaowachagua Africa ni kiungulia kitupu!
 
Back
Top Bottom