Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,706
- 155,198
Huyu mwana wetu, hatukumwambia alipokosea, aliamua kufanya lolote atakalo, na hata alipofanya mabaya tukamsifu kwamba huo uovu wake aufanyao ndio uanaume wenyewe.
Alianza kwa kuwatumia rafiki zake wa kutoka mbali tusiowajua kupoteza wadogo zake, akaenda mbali akafanya maovu makubwa, tukamsifu Sana kwamba yeye ni kidume.
Lakini Kuna ndugu walikuwa wakituasa na kutushauri kuwa huyu mtoto tunamuharibu, sisi hatukusikia, tukaendelea kupuliza filimbi na nyimbo mpya tukamtungia.
Sasa leo Vyombo vya Dola vimetukamata na kutuweka korokoroni ndipo sasa tunalia na kusaga meno.
Tunapiga magoti, tunaomba, Mungu ametuma ujumbe mfupi tu.
Alianza kwa kuwatumia rafiki zake wa kutoka mbali tusiowajua kupoteza wadogo zake, akaenda mbali akafanya maovu makubwa, tukamsifu Sana kwamba yeye ni kidume.
Lakini Kuna ndugu walikuwa wakituasa na kutushauri kuwa huyu mtoto tunamuharibu, sisi hatukusikia, tukaendelea kupuliza filimbi na nyimbo mpya tukamtungia.
Sasa leo Vyombo vya Dola vimetukamata na kutuweka korokoroni ndipo sasa tunalia na kusaga meno.
Tunapiga magoti, tunaomba, Mungu ametuma ujumbe mfupi tu.