Mchawi akimaliza kuroga mtaa hugeukia familia yake: Baada ya upinzani kiama chaja CCM

Mzalendo_Mwandamizi

JF-Expert Member
Dec 12, 2007
1,117
4,764
"Mchawi akimaliza kuroga mtaa mzima, hugeukia familia yake." One of my most favourite age-old adages. Literally, msemo huu unamaanisha kwamba mtu akishamaliza kufanya mabaya kwa kila "asiyemhusu" hatimaye huwageukia wanaomhusu.

Sote tumeshuhudia yaliyojiri dhidi ya vyama vya upinzani katika miaka mitatu ya utawala wa Jiwe. Sihitaji kutonesha vidonda ambavyo havijapona hasa ikizingatiwa kuwa wahanga wa utawala wa mabavu wa Jiwe bado wanataabika - Mbowe na Matiko wapo jela, Tundu Lissu licha ya kuwa hajapona kamili bado anaandamwa kila kukicha, Azory na Ben Saanae "bado hawajulikani waliko," yaliyojiri MKIRU bado ni "siri kuu," Wapinzani wanaendelea kunyimwa haki zao za msingi huku CCM wakizichezea haki hizo kama mzaha vile....orodha ni ndefu.

Lakini pia Jiwe amefanikiwa sana katika kusambaza siasa za chuki, sio tu miongoni mwa wana-CCM wenzake bali hata kwa wafuasi wa Upinzani. Tumefika mahala kwamba aidha uwe unaimba mapambio kumsifia Jiwe - na hapohapo kupokea mvua ya matusi kutoka kwa wafuasi wa Upinzani - au uwe mfuasi wa Upinzani - na hapohapo uandamwe kama mhaini na MATAGA, Buku 7 Lumumba, na wapuuzi kama hao.

Kwahiyo "akina sie ambao itikadi yetu pekee ni maslahi na mustakabali wa Tanzania yetu," tunajikuta na choice moja tu: kukaa kimya ili kuepusha kugeuzwa punching bag la wanaojifunza matusi mtandaoni.

Hata hivyo, kukaa kimya wakati mwelekeo wa taifa sio mzuri ni sawa na usaliti, na ndio maana inalazimu mara moja moja "kuvaa kofia ya chuma" dhidi ya matusi yatakayojitokeza baada ya kuongea lolote lile, maana likiwafurahisha wafuasi wa Upinzani basi litawakera wafuasi wa CCM na hivyo kupelekea mvua ya matusi, na likiwakera wafuasi wa Upinzani litawafurahisha wafuasi wa CCM, na hivyo pia kupelekea mafuriko ya matusi.

Anyway, ndio tulipofikia hapo kama Taifa.

Hadi muda huu ni furaha tele huko CCM kwa jinsi Jiwe "anavyowaburuza" Wapinzani. Lakini sie wengine tunaofahamu yanayojiri nyuma ya pazia/chini ya kapeti tunafahamu vema kuwa haya wanayofanyiwa wapinzani ni tip of iceberg tu ya suala zima la kumuandama kila mtu anayeonekana kuwa tishio kwa dhamira ya Jiwe ya kutawala milele. Naam, kama hujui hilo ndo unaambiwa sasa. Huyo bwana hana mpango wa kutoka madarakani, sio 2025 wala baada ya hapo.

Kuna kundi moja lenye ushawishi mkubwa sana kwa jiwe. Kundi hili ni wanufaika wakubwa wa sera ya ukanda/ukabila inayoendelea kuitafuna Tanzania yetu. Wengi wa watu hawa ni vijana wa umri wa kati, waliosoma na Jiwe au waliwahi kufanya kazi pamoja huko nyuma.

Takriban wote wana nyadhifa mbalimbali, wengine wana nyadhifa muhimu kitaifa, wengine mikoani, wengine kwenye taasisi za umma, wengine wilayani. Sihitaji kuwataja majina kwani naamini wengi wenu mwawafahamu.

Uhusiano kati ya Jiwe na kundi hili ni symbiotic kama ule wa Kitengo na CCM: survival ya kila upande inategemea survival ya mwenzie. Hao jamaa hawakupewa madaraka na Jiwe kwa bahati mbaya.Hapana. Most of them walipigana kufa na kupona kuhakikisha kuwa "poti wao" anaingia Ikulu. Ikumbukwe kuwa suala la Jiwe kuingia Ikulu lilikuwa linaandika historia mpya kwa Kanda ambayo licha ya ukubwa kikabila, haikuwahi kuzalisha Rais, Makamu au Waziri Mkuu.

Kwahiyo baada ya Jiwe kuingia Ikulu, aliwalipa fadhila jamaa zake hao kwa kuwateua katika nafasi mbalimbali. Hiyo ilikuwa asante yake kwao. Lakini wakati hili sio siri sana, deni kubwa la Jiwe kwa watu hao ni "siri binafsi." Takriban wote wanajua masuala flani kuhusu Jiwe ambayo laiti wangeyamwaga hadharani 2015, Jiwe asingefika kwenye Tano Bora let alone kuibuka mshindi kwenye Tatu Bora.

Miongoni mwa "siri" hizo ni hiyo inayomfanya Jiwe kuwa "mateka wa Mtu Mrefu Paulo."

Kwahiyo, kwa namna flani, kama ilivyokuwa kwa JK ambaye kwa kiasi kikubwa alikuwa kama mateka wa mafisadi waliomsaidia kuingia mdarakani, Jiwe nae ni kama mateka wa hilo genge la marafiki zake ambao sio tu walimsaidia kuingia madarakani lakini pia wanamhifadhia "nyeti" ambazo zikivuja tu, amekwisha.

Kwa wenye uelewa wa yanayojiri nyuma ya pazia/chini ya kapeti, zama za ufisadi sio tu zimerudi bali inaelezwa kuwa katika kipindi cha takriban miaka mitatu ya Jiwe, hali ni maradufu ya yaliyojiri katika miaka 10 ya JK. Huku media zikiwa zimezibwa mdomo, kitu pekee kinachosikika ni vigelegele na mapambio kwa Jiwe. Hakuna wa kuthubutu kueleza hali halisi. Ndio maana ufisadi wa mradi wa passport za kielektroniki, ufisadi wa shilingi trilioni moja unusu, changa la macho kwenye Koroshow, ujenzi wa Chuttle Intl Airport, Ununuzi wa bombadia/drimlayna, nk ni masuala ambayo kamwe hayatowekwa hadharani.

Wanasema "wakati enzi za JK ufisadi ulikuwa suala la EQUAL OPPORTUNITY" - kwa maana kila aliyeweza kuuza unga, poa; kila aliyeweza kufanya ujangili, poa; kila aliyeweza kuchapisha noti feki, poa, nk - zama hizi za Jiwe, ufisadi ni kwa privileged few - hao washkaji zake aliotoka nao mbali, waliompigania kwenye kampeni, waliohifadhi "mabaya" yake, na wakazawadiwa madaraka katika ngazi mbalimbali. Some of them ni ndugu wa damu wa Jiwe.

Kuna mambo mawili hapa. Kwanza, utawala wa Jiwe unawanufaisha hao jamaa zake katika namna ambayo "hawawezi kuishi hivyo bila yeye kuwepo madarakani." Kwahiyo, hawa wanataka aendelee kuwepo madarakani ili nao waendelee kufakamia keki ya taifa. Lakini pili, ni maovu yanayoambatana na ufakamiaji huo wa keki ya taifa. Kama alivyotahadharisha mbunge mmoja kuhusu "mpwa wa Jiwe," pindi Jiwe akiondoka, genge hilo nalo lipo katika hatari ya kutupwa jela. Hawa ndio the brains behind idea ya "Jiwe kutawala milele."

Sijui kama hii ni habari njema au la, kuna jithada kubwa zinafanyika chinichini ndani ya CCM kukabiliana na genge hili, japo hadi sasa matokeo ni "kundi la Jiwe 5 wapinzani ndani ya CCM 0." Na sababu ni nyingi: Kitengo hasa kwa kupitia MATAGA, Msaada kutoka kwa Mtu Mrefu Paulo na teknolojia ya Waisraeli, na ukweli tu kuwa mfumo waloutengenza CCM hautoi fursa nzuri kwa wanaotaka mabadiliko ya dharura.

Sasa, baada ya kumaliza kuwashughulikia Wapinzani, ngwe iliyopo ni kuwashughulikia "wapinzani ndani ya CCM." Kuna mbinu chafu zinazotumika, kwa mfano kuna jitihada kubwa ya kukusanya taarifa kuhusu maisha binafsi ya JK - michepuko yake and stuff, - kama miongoni mwa silaha zitakazotumika kum-blackmail endapo atasimama kidete dhidi ya "mabaya" yanayoendelea ndani ya chama chao.

Kwa kuhitimisha, hatua ijayo - na ambayo imeshaanza kutimia - ni maandalizi ya ushindi wa kishindo kwa Jiwe mwaka 2020, yanayoambatana na kuondoa "wapinzani ndani ya CCM." Sambamba na "wapinzani ndani ya CCM" ni watu wanaoonekana kuwa na potential ya kuunga mkono upinzani dhidi ya Jiwe ndani ya CCM. No wonder ile approach ya awali ya kuwakalia kooni viongozi wa dini imegeuzwa na badala yake "wamerejeshwa kundini." Walengwa wengine ni wafanyabiashara na private sector kwa ujumla.

In conclusion, whether Jiwe atawarudi CCM wenzake baada ya "kuwamaliza" wapinzani au la, moja ya tafakuri muhimu ambayo "wapinzani halisi" kwa maana ya vyama vya upinzani wanapaswa kujiuliza ni jibu la swali hili kutoka kwa Watanzania: "MLI/MNA/MTAFANYA NINI KUZUWIA JANGA HILI?"
 
Ina hitaji Akili kubwa kuelewa mustakabali wa Taifa Hili
la sivyo mengine yatakuwa Ni porojo na chai

Leta evidence siyo blah blah
 
"Mchawi akimaliza kuroga mtaa mzima, hugeukia familia yake." One of my most favourite age-old adages. Literally, msemo huu unamaanisha kwamba mtu akishafanya kufanya mabaya kwa kila "asiyemhusu" hatimaye huwageukia wanaomhusu.

Sote tumeshuhudia yaliyojiri dhidi ya vyama vya upinzani katika miaka mitatu ya uatawala wa Jiwe. Sihitaji kutonesha vidonda ambavyo havijapona hasa ikizingatiwa kuwa wahanga wa utawala wa mabavu wa Jiwe bado wanataabika - Mbowe na Matiko wapo jela, Tundu Lissu licha ya kuwa hajapona kamili bado anaandamwa kila kukicha, Azory na Ben Saanae "bado hawajulikani waliko," yaliyojiri MKIRU bado ni "siri kuu," Wapinzani wanaendelea kunyimwa haki zao za msingi huku CCM wakizichezea haki hizo kama mzaha vile....orodha ni ndefu.

Lakini pia Jiwe amefanikiwa sana katika kusambaza siasa za chuki, sio tu miongoni mwa wana-CCM wenzake bali hata kwa wafuasi wa Upinzani. Tumefika mahala kwamba aidha uwe unaimba mapambio kumsifia Jiwe - na hapohapo kupokea mvua ya matusi kutoka kwa wafuasi wa Upinzani - au uwe mfuasi wa Upinzani - na hapohapo uandamwe kama mhaini na MATAGA, Buku 7 Lumumba, na wapuuzi kama hao.

Kwahiyo "akina sie ambao itikadi yetu pekee ni maslahi na mustakabali wa Tanzania yetu," tunajikuta na choice moja tu: kukaa kimya ili kuepusha kugeuzwa punching bad la wanaojifunza matusi myandaoni.

Hata hivyo, kukaa kimya wakati mwelekeo wa taifa sio mzuri ni sawa na usaliti, na ndio maana inalazimu mara moja moja "kuvaa kofia ya chuma" dhidi ya matusi yatakayojitokeza baada ya kuongea lolote lile, maana likiwafurahgisha wafuasi wa Upinzani basi litawakera wafuasi wa CCM na hivyo kupelekea mvua ya matusi, na likiwakera wafuasi wa Upinzani litawafurahisha wafuasi wa CCM, na hivyo pia kupelekea mafuriko ya matusi.

Anyway, ndio tulipofikia hapo kama Taifa.

Hadi muda huu ni furaha tele huko CCM kwa jinsi Jiwe "anavyowaburuza" Wapinzani. Lakini sie wengine tunaofahamu yanayojiri nyuma ya pazia/chini ya kapeti tunafahamu vema kuwa haya wanayofanyiwa wapinzani ni tip og iceberg tu ya suala zima la kumuandama kila mtu anayeonekana kuwa tishio kwa dhamira ya Jiwe ya kutawala milele. Naam, kama hujui hilo ndo unaambiwa sasa. Huyo bwana hana mpango wa kutoka madarakani, sio 2025 wala baada ya hapo.

Kuna kundi moja lenye ushawishi mkubwa sana kwa jiwe. Kundi hili ni wanufaika wakubwa wa sera ya ukanda/ukabila inayoendelea kuitafuna Tanzania yetu. Wengi wa watu hawa ni vijana wa umri wa kati, waliosoma na Jiwe au waliwahi kufanya kazi pamoja huko nyuma.

Takriban wote wana nyadhifa mbalimbali, wengine wana nyadhifa muhimu kitaifa, wengine mikoani, wengine kwenye taasisi za umma, wengine wilayani. Sihitaji kuwataja majina kwani naamini wengi wenu mwawafahamu.

Uhusiano kati ya Jiwe na kundi hili ni symbiotic kama ule wa Kitengo na CCM: survival ya kila upande inategemea surival ya mwenzie. Hao jamaa hawakupewa madaraka na Jiwe kwa bahati mbaya.Hapana. Most of them walipigana kufa na kupona kuhakikisha kuwa "poti wao" anaingia Ikulu. Ikumbukwe kuwa suala la Jiwe kuingia Ikulu lilikuwa linaandika historia mpya kwa Kanda ambayo licha ya ukubwa kikabila, haikuwahi kuzalisha Rais, Makamu au Waziri Mkuu.

Kwahiyo baada ya Jiwe kuingia Ikulu, aliwalipa fadhila jamaa zake hao kwa kuwateua katika nafasi mbalimbali. Hiyo ilikuwa asante yake kwao. Lakini wakati hili sio siri sana, deni kubwa la Jiwe kwa watu hao ni "siri binafsi." Takriban wote wanajua masuala flani kuhusu Jiwe ambayo laiti wangeyamwaga hadharani 2015, Jiwe asingefika kwenye Tano Bora let alone kuibuka mshindi kwenye Tatu Bora.

Miongoni mwa "siri" hizo ni hiyo inayomfanya Jiwe kuwa "mateka wa Mtu Mrefu Paulo."

Kwahiyo, kwa namna flani, kama ilivyokuwa kwa JK ambaye kwa kiasi kikubwa alikuwa kama mateka wa mafisadi waliomsaidia kuingia mdarakani, Jiwe nae ni kama mateka wa hilo genge la marafiki zake ambao sio tu walimsaidia kuingia madarakani lakini pia wanamhifadhia "nyeti" ambazo zikivuja tu, amekwisha.

Kwa wenye uelewa wa yanayojiri nyuma ya pazia/chini ya kapeti, zama za ufisadi sio tu zimerudi bali inaelezwa kuwa katika kipindi cha takriban miaka mitatu ya Jiwe, hali ni maradufu ya yaliyojiri katika miaka 10 ya JK. Huku media zikiwa zimezibwa mdomo, kitu pekee kinachosikika ni vigelegele na mapambio kwa Jiwe. Hakuna wa kuthubutu kueleza hali halisi. Ndio maana ufisadi wa mradi wa passport za kielektroniki, ufisadi wa shilingi trilioni moja unusu, changa la macho kwenye Koroshow, ujenzi wa Chuttle Intl Airport, Ununuzi wa bombadia/drimlayna, nk ni masuala ambayo kamwe hayatowekwa hadharani.

Wanasema "wakati enzi za JK ufisadi ulikuwa suala la EQUAL OPPORTUNITY - kwa maana kila aliyeweza kuuza unga, poa; kila aliyeweza kufanya ujangili, poa; kila aliyeweza kuchaposha noti feki, poa, nk - zama hizi za Jiwe, ufisadi ni kwa privileged few - hao washkaji zake aliotoka nao mbali, waliompigania kwenye kampeni, waliohifadhi "mabaya" yake, na wakazawadiwa madaraka katika ngazi mbalimbali. Some of them ni ndugu wa damu wa Jiwe.

Kuna mambo mawili hapa. Kwanza, utawala wa Jiwe unawanufaisha hao jamaa zake katika namna ambayo "hawawezi kuishi hivyo bila yeye kuwepo madarakani." Kwahiyo, hawa wanataka aendelee kuwepo madarakani ili nao waendelee kufakamia keki ya taifa. Lakini pili, ni maovu yanayoambatana na ufakamiaji huo wa keki ya taifa. Kama alivyotahadharisha mbunge mmoja kuhusu "mpwa wa Jiwe," pindi Jiwe akiondoka, genge hilo nalo lipo katika hatari ya kutupwa jela. Hawa ndio the brains behind idea ya "Jiwe kutawala milele."

Sijui kama hii ni habari njema au la, kuna jithada kubwa zinafanyika chinichini ndani ya CCM kukabiliana na genge hili, japo hadi sasa matokeo ni "kundi la Jiwe 5 wapinzani ndani ya CCM 0." Na sababu ni nyingi: Kitengo hasa kwa kupitia MATAGA, Msaada kutoka kwa Mtu Mrefu Paulo na teknolojia ya Waisraeli, na ukweli tu kuwa mfumo waloutengenza CCM hautoi fursa nzuri kwa wanaotaka mabadiliko ya dharura.

Sasa, baada ya kumaliza kuwashughulikia Wapinzani, ngwe iliyopo ni kuwashughulikia "wapinzani ndani ya CCM." Kuna mbinu chafu zinazotumika, kwa mfano kuna jithada kubwa ya kukusanya taarifa kuhusu maisha binafsi ya JK - michepuko yake and stuff, - kama miongoni mwa silaha zitakazotumika kum-blackmail endapo atasimama kidete dhidi ya "mabaya" yanayoendelea ndani ya chama chao.

Kwa kuhitimisha, hatua ijayo - na ambayo imeshaanza kutimia - ni maandalizi ya ushindi wa kishindo kwa Jiwe mwaka 2020, yanayoambatana na kuondoa "wapinzani ndani ya CCM," Sambamba na "wapinzani ndani ya CCM" ni watu wanaoonekana kuwa na potential ya kuunga mkono upinzani dhidi ya Jiwe ndani ya CCM. No wonder ile approach ya awali ya kuwakalia kooni viongozi wa dini imegeuzwa na badala yake "wamerejeshwa kundini."

In conclusion, whether Jiwe atawarudi CCM wenzake baada ya "kuwamaliza" wapinzani au la, moja ya tafakuri muhimu ambayo "wapinzani halisi" kwa maana ya vyama vya upinzani wanapaswa kujiuliza ni jibu la swali hili kutoka kwa Watanzania: "MLI/MNA/MTAFANYA NINI KUZUWIA JANGA HILI?"
Wacha wafu wazikane.
Nchi ishakata pumzi hii
kila mwenye sauti anataka kusikika
 
chahali huyu alisema ziara za lissu ni fake news, unadanganya.


binafsi namjua jiwe kwa 20%, nawajua ndugu zake aliozaliwa nao tumbo moja wote, najua ndugu wengine wa unayemwita jiwe.



jiwe hana upendeleo, chapa Kazi ionekane kama huli mema.
 
Chahali watanzania wa leo si wale wa 70s, wanaweza kuchambua pumba, mchele, mahindi na vumbi. Unaandika pumba sana, wakati mwingine napata shida ilikuaje ulifanya kazi kitengoni? Nani alikuweka? Ulifanyiwa vetting kweli?
Chahali ni kama sasa una psychological problems, ni kama una majuto hivi, kuna jambo linakusumbua sana kichwani. Tanzania haitagawika makundi kupitia maneno ya mitandaoni. Serikali inafanya kazi nzuri na ukweli zipo changamoto.

Hakuna serikali duniani isiyokua na changamoto, huo uzandiki wenu na undumila kuwili hautafanikiwa abadani.
Na endelea tu ba hii tabia yako ipo siku, utakalia kiti chenye msumari mrefu wa nchi 6

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila nikimtupia Jicho Jiwe na kumuangalia, muonekano wa afya yake unanipa matumaini kuwa mbio zake ni za Sakafuni.

Huwa namuangalia kwenye television, kila siku nanotice exhaution, loss of energy, loss of balance, loss of confidence, loss of control.

Wacha wapambe waendelee kufukuza upepo lakini Natural selection inasema kuwa IN THE STRUGGLE FOR EXISTENCE ONLY THOSE WHO ARE FIT WILL SURVIVE!
 
Hilo Lissu aliliona siku nyingi na alikwisha sema akitoka kwetu atahamia kwenu,
Tunakuomba eeh bwana mapenzi yako yatimizwe kwa huyu mtu, tunajua wewe unampenda kuzidi sisi Dr. Mwigulu Nchemba apata ajali ya gari - JamiiForums
Daahh Lissu alikosea sana kusema alipigiwa simu na former cabinet minister. Mojakwamoja wazee naona wakajua ni Former mambo ya ndani.Nayeye naona alikosea mana alijishtukia akaanza kutafuta interview huko clouds. Tuombe awe amepona ktk ajali hiyo na kama amepona basi huko hospital lisitokee LA wasiojulikana.Amen

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Anayoyasema chahali ni ukweli mtupu bali mataga wanajidai kumpinga ili kuwapotezea watanzania wasijue kinachoendelea .Maana hata sugu ametahadhalisha Pepo la kuongeza miaka mhula wa urais ,wanasubiria upenyo tu wapeleke bungeni bali mungu hawezi kuwaacha watanzania labda awe wa maboksi .
 
Anayoyasema chahali ni ukweli mtupu bali mataga wanajidai kumpinga ili kuwapotezea watanzania wasijue kinachoendelea .Maana hata sugu ametahadhalisha Pepo la kuongeza miaka mhula wa urais ,wanasubiria upenyo tu wapeleke bungeni bali mungu hawezi kuwaacha watanzania labda awe wa maboksi .
Mkuu nasikitika kukutaarifu kuwa Mungu haingilii maisha ya watu, angekua anafanya hivyo dhana zima ya dhambi ingekuwa haina maana. Hivyo basi itakapofika ile saa, maamuzi yatakuwa ni yako na yako pekeyako, utasimama upande wa haki au wa mafashisti?
 
"Mchawi akimaliza kuroga mtaa mzima, hugeukia familia yake." One of my most favourite age-old adages. Literally, msemo huu unamaanisha kwamba mtu akishamaliza kufanya mabaya kwa kila "asiyemhusu" hatimaye huwageukia wanaomhusu.

Sote tumeshuhudia yaliyojiri dhidi ya vyama vya upinzani katika miaka mitatu ya utawala wa Jiwe. Sihitaji kutonesha vidonda ambavyo havijapona hasa ikizingatiwa kuwa wahanga wa utawala wa mabavu wa Jiwe bado wanataabika - Mbowe na Matiko wapo jela, Tundu Lissu licha ya kuwa hajapona kamili bado anaandamwa kila kukicha, Azory na Ben Saanae "bado hawajulikani waliko," yaliyojiri MKIRU bado ni "siri kuu," Wapinzani wanaendelea kunyimwa haki zao za msingi huku CCM wakizichezea haki hizo kama mzaha vile....orodha ni ndefu.

Lakini pia Jiwe amefanikiwa sana katika kusambaza siasa za chuki, sio tu miongoni mwa wana-CCM wenzake bali hata kwa wafuasi wa Upinzani. Tumefika mahala kwamba aidha uwe unaimba mapambio kumsifia Jiwe - na hapohapo kupokea mvua ya matusi kutoka kwa wafuasi wa Upinzani - au uwe mfuasi wa Upinzani - na hapohapo uandamwe kama mhaini na MATAGA, Buku 7 Lumumba, na wapuuzi kama hao.

Kwahiyo "akina sie ambao itikadi yetu pekee ni maslahi na mustakabali wa Tanzania yetu," tunajikuta na choice moja tu: kukaa kimya ili kuepusha kugeuzwa punching bag la wanaojifunza matusi mtandaoni.

Hata hivyo, kukaa kimya wakati mwelekeo wa taifa sio mzuri ni sawa na usaliti, na ndio maana inalazimu mara moja moja "kuvaa kofia ya chuma" dhidi ya matusi yatakayojitokeza baada ya kuongea lolote lile, maana likiwafurahisha wafuasi wa Upinzani basi litawakera wafuasi wa CCM na hivyo kupelekea mvua ya matusi, na likiwakera wafuasi wa Upinzani litawafurahisha wafuasi wa CCM, na hivyo pia kupelekea mafuriko ya matusi.

Anyway, ndio tulipofikia hapo kama Taifa.

Hadi muda huu ni furaha tele huko CCM kwa jinsi Jiwe "anavyowaburuza" Wapinzani. Lakini sie wengine tunaofahamu yanayojiri nyuma ya pazia/chini ya kapeti tunafahamu vema kuwa haya wanayofanyiwa wapinzani ni tip of iceberg tu ya suala zima la kumuandama kila mtu anayeonekana kuwa tishio kwa dhamira ya Jiwe ya kutawala milele. Naam, kama hujui hilo ndo unaambiwa sasa. Huyo bwana hana mpango wa kutoka madarakani, sio 2025 wala baada ya hapo.

Kuna kundi moja lenye ushawishi mkubwa sana kwa jiwe. Kundi hili ni wanufaika wakubwa wa sera ya ukanda/ukabila inayoendelea kuitafuna Tanzania yetu. Wengi wa watu hawa ni vijana wa umri wa kati, waliosoma na Jiwe au waliwahi kufanya kazi pamoja huko nyuma.

Takriban wote wana nyadhifa mbalimbali, wengine wana nyadhifa muhimu kitaifa, wengine mikoani, wengine kwenye taasisi za umma, wengine wilayani. Sihitaji kuwataja majina kwani naamini wengi wenu mwawafahamu.

Uhusiano kati ya Jiwe na kundi hili ni symbiotic kama ule wa Kitengo na CCM: survival ya kila upande inategemea survival ya mwenzie. Hao jamaa hawakupewa madaraka na Jiwe kwa bahati mbaya.Hapana. Most of them walipigana kufa na kupona kuhakikisha kuwa "poti wao" anaingia Ikulu. Ikumbukwe kuwa suala la Jiwe kuingia Ikulu lilikuwa linaandika historia mpya kwa Kanda ambayo licha ya ukubwa kikabila, haikuwahi kuzalisha Rais, Makamu au Waziri Mkuu.

Kwahiyo baada ya Jiwe kuingia Ikulu, aliwalipa fadhila jamaa zake hao kwa kuwateua katika nafasi mbalimbali. Hiyo ilikuwa asante yake kwao. Lakini wakati hili sio siri sana, deni kubwa la Jiwe kwa watu hao ni "siri binafsi." Takriban wote wanajua masuala flani kuhusu Jiwe ambayo laiti wangeyamwaga hadharani 2015, Jiwe asingefika kwenye Tano Bora let alone kuibuka mshindi kwenye Tatu Bora.

Miongoni mwa "siri" hizo ni hiyo inayomfanya Jiwe kuwa "mateka wa Mtu Mrefu Paulo."

Kwahiyo, kwa namna flani, kama ilivyokuwa kwa JK ambaye kwa kiasi kikubwa alikuwa kama mateka wa mafisadi waliomsaidia kuingia mdarakani, Jiwe nae ni kama mateka wa hilo genge la marafiki zake ambao sio tu walimsaidia kuingia madarakani lakini pia wanamhifadhia "nyeti" ambazo zikivuja tu, amekwisha.

Kwa wenye uelewa wa yanayojiri nyuma ya pazia/chini ya kapeti, zama za ufisadi sio tu zimerudi bali inaelezwa kuwa katika kipindi cha takriban miaka mitatu ya Jiwe, hali ni maradufu ya yaliyojiri katika miaka 10 ya JK. Huku media zikiwa zimezibwa mdomo, kitu pekee kinachosikika ni vigelegele na mapambio kwa Jiwe. Hakuna wa kuthubutu kueleza hali halisi. Ndio maana ufisadi wa mradi wa passport za kielektroniki, ufisadi wa shilingi trilioni moja unusu, changa la macho kwenye Koroshow, ujenzi wa Chuttle Intl Airport, Ununuzi wa bombadia/drimlayna, nk ni masuala ambayo kamwe hayatowekwa hadharani.

Wanasema "wakati enzi za JK ufisadi ulikuwa suala la EQUAL OPPORTUNITY" - kwa maana kila aliyeweza kuuza unga, poa; kila aliyeweza kufanya ujangili, poa; kila aliyeweza kuchapisha noti feki, poa, nk - zama hizi za Jiwe, ufisadi ni kwa privileged few - hao washkaji zake aliotoka nao mbali, waliompigania kwenye kampeni, waliohifadhi "mabaya" yake, na wakazawadiwa madaraka katika ngazi mbalimbali. Some of them ni ndugu wa damu wa Jiwe.

Kuna mambo mawili hapa. Kwanza, utawala wa Jiwe unawanufaisha hao jamaa zake katika namna ambayo "hawawezi kuishi hivyo bila yeye kuwepo madarakani." Kwahiyo, hawa wanataka aendelee kuwepo madarakani ili nao waendelee kufakamia keki ya taifa. Lakini pili, ni maovu yanayoambatana na ufakamiaji huo wa keki ya taifa. Kama alivyotahadharisha mbunge mmoja kuhusu "mpwa wa Jiwe," pindi Jiwe akiondoka, genge hilo nalo lipo katika hatari ya kutupwa jela. Hawa ndio the brains behind idea ya "Jiwe kutawala milele."

Sijui kama hii ni habari njema au la, kuna jithada kubwa zinafanyika chinichini ndani ya CCM kukabiliana na genge hili, japo hadi sasa matokeo ni "kundi la Jiwe 5 wapinzani ndani ya CCM 0." Na sababu ni nyingi: Kitengo hasa kwa kupitia MATAGA, Msaada kutoka kwa Mtu Mrefu Paulo na teknolojia ya Waisraeli, na ukweli tu kuwa mfumo waloutengenza CCM hautoi fursa nzuri kwa wanaotaka mabadiliko ya dharura.

Sasa, baada ya kumaliza kuwashughulikia Wapinzani, ngwe iliyopo ni kuwashughulikia "wapinzani ndani ya CCM." Kuna mbinu chafu zinazotumika, kwa mfano kuna jitihada kubwa ya kukusanya taarifa kuhusu maisha binafsi ya JK - michepuko yake and stuff, - kama miongoni mwa silaha zitakazotumika kum-blackmail endapo atasimama kidete dhidi ya "mabaya" yanayoendelea ndani ya chama chao.

Kwa kuhitimisha, hatua ijayo - na ambayo imeshaanza kutimia - ni maandalizi ya ushindi wa kishindo kwa Jiwe mwaka 2020, yanayoambatana na kuondoa "wapinzani ndani ya CCM." Sambamba na "wapinzani ndani ya CCM" ni watu wanaoonekana kuwa na potential ya kuunga mkono upinzani dhidi ya Jiwe ndani ya CCM. No wonder ile approach ya awali ya kuwakalia kooni viongozi wa dini imegeuzwa na badala yake "wamerejeshwa kundini." Walengwa wengine ni wafanyabiashara na private sector kwa ujumla.

In conclusion, whether Jiwe atawarudi CCM wenzake baada ya "kuwamaliza" wapinzani au la, moja ya tafakuri muhimu ambayo "wapinzani halisi" kwa maana ya vyama vya upinzani wanapaswa kujiuliza ni jibu la swali hili kutoka kwa Watanzania: "MLI/MNA/MTAFANYA NINI KUZUWIA JANGA HILI?"

Kuna watu kadhaa siku moja walikaribishwa kwenye sherehe na miongoni mwao walikuwemo watu wasioona. Ulipofika wakati wa kula chakula, mhusika wa maswala ya chakula akaamua kuwatenga wale wasiiona kwa nia njema kwamba wanaweza wasipate nafasi nzuri ya kula wakashiba, kama wale wengine wanaoona. Baada ya kuwatenga, akawapa pia shea maradufu ukilinganisha na wenzao wasiokuwa na tatizo la kuona. Shea hiyo ilikuwa kubwa kiasi kwamba hawa watu wasioona waliweza kubaini hilo wakati wanaendelea kula. Baada ya kuona kuwa wamepewa shea kubwa sana, mmoja wa hao wasioona akawaambia wenzake SISI TUSIOONA TUMEPEWA SHEA KUBWA HIVI, WENYE MACHO JE? Huyu mtu aliuliza swali hili kwa hoja kubwa ya msingi kwamba, ilikuwa kawaida sana kwenye sherehe kama hizo kwa wasioona kutokula kabisa au kupata chakula kidogo, tofauti na alivyofanya huyu bwana aliyewakirimu hawa.

Wa-Tanzania tulizoea ufisadi na hivyo inaonyesha kuwa hakuna utawala utakaokuja na tukaamini kuwa hakuna ufisadi serikalini, hata kama utawala huo utakuwa hauna hata chembe moja ya ufisadi.
 
Paulo mrefu wa nchi jirani anatamani Jiwe afuate nyayo zake kwa sababu kuu zifuatazo

1. Ili atawale kwa utulivu anahitaji Rwanda yenye uchumi mzuri, la sivyo hali ikiwa mbaya Watusi na Wahutu kwa pamoja watapata kamba ya kuwaunganisha pamoja ya kumng'oa. Na ili Rwanda iwe na uchumi mzuri lazima iwe katika good terms na bongo maana bidhaa zao nyingi zinapitia hapa. Kwa Rwanda bandari ya Mombasa siyo option nzuri, ni mbali na itaongeza gharama za bidhaa. Kwa hiyo Paul mrefu anahitaji rafiki, mtu waliyeshibana akalie kiti cha enzi hapa bongo ikibidi kwa muda wote ambao Paulo mrefu ataendelea kuwa raisi wa maisha huko Rwanda!

2. Ili Paulo mrefu asionekane dikteta, ingempendeza nchi zote za ukanda huu zifanane na yeye ili asitolewe mifano ya mbona "Tanzania wanabadirisha utawala kila baada ya miaka....". Muelewe tu ndugu zangu Paulo Mrefu na Mu7 walikuwa hawapendi demokrasia ya Bongo, ilikuwa ikiwatia aibu, walikuwa wakijisikia vibaya kila wakialikwa kwenye uapishwaji wa raisi mpya hapa bongo. Sasa ili kuondoa hii aibu, wanafanya kila liwezekanalo na mwenzao awe kama wao, atawale tu, eti "akamilishe miradi aliyokwisha ianza". Kibaya zaidi ninaona dalili za Jiwe kuanza kukubaliana nao!. Maana mambo yote yaliyofanywa kama vile kununua wapinzani, kutunga kanuni kali za sheria ya habari, sheria ya takwimu, sheria mpya ya vyama vya siasa, hii ya kuwavuta karibu viongozi wa dini, kuminya wafanyabiashara wakubwa inaonyesha wazi kuwa naye anataka kwenda kwenye muelekeo uleule!

Je atafanikiwa?

1. Hawezi kufanikiwa, sidhani, japo akili yake namini ingependa lakini mwili wake kila ninavyomuangalia haumpi sapoti.

2. Ana kigingi kizito sana cha International Community, International Community iliweza kuifumbia macho Rwanda kwa sababu ya Guiltiness ya kutofanya chochote kuisaidia kwenye genocide, kwa hiyo Paul mrefu pamoja na madudu yake wanamvumilia kwa sababu ya Stability sake hapo Rwanda. Ila kwa bongo hii Tayari tuna precedence nzuri katika mambo ya demokrasia kiasi kwamba Kuyareverse yote inabidi ujitoe ufahamu kwelikweli!. Hata ukiamua kujitoa Ufahamu basi utapata tabu sana.
Kule Uganda , Mu7 aliingia kwa mapinduzi hakukuwa na Precedence ya kuachiana madaraka kama huku kwetu kwa hiyo kwa Uganda, Mu7 is the only president ambaye International community imefanya naye kazi mwenye nafuu kuliko madhalimu waliomtangulia akina Obote na Amin.
Hali ni Tofauti hapa kwetu, tayari tuna 4 presidents walioingia kwa amani na kustaafu kwa amani. Unahitaji kuwa na akili za kiwendawazimu kujaribu kuwaconvince International Community kuwa woote waliopita hawana maana yoyote!

3. Hana uchumi, wala Charisma, wala Heroic Stature vya kuwadanganyia watu kuwa anyway labda wacha tu tuendelee nae. Uchumi Ukijamba patakuwa mtafutano hapa, hakuna mtu atakayekubali kupanga foleni kununua robo ya sukari au kubeba noti za laki moja moja kwenda kununua kilo ya unga

4. Bongo bado kuna mizizi ya resistance, Lipo kanisa lenye nguvu la Kikatoliki na Kilutheri, Waumini wao wakianza kulia njaa na kukosa ajira na kuwekwa ndani kwa sababu ya kupinga mambo mbalimbali ya kumfanya atawale milele lazima Vilio hivyo vitaambatana na Nyaraka kali na presha kubwa ya kuheshimu utawala wa sheria. Sauti ya hawa watu Haiwezi!. Kwa BAKWATA huko hana shida maana ni taasisi yao ile. Labda tu afanye move kama za Dodoma za kugusa mambo ya Imani ya Waislamu hapo rage yao ataipata!, Ila mambo ya demokrasi Waislamu huwa hawana interest sana na mambo hayo!

5. Kuna Upinzani, Watu kama Akina Lussu, Zitto na wengineo wengi watakaoibuka itampasa atumie nguvu nyingi sana kudela nao, kila atakapokuwa anadeal nao atapoteza concentration ya kufocus kwenye mambo ya msingi ya uchumi na kuinua maisha ya watu, matokeo yake kutokana na hali hiyo plus umasikini wa watu atapingwa kila kona.

6. Hidden hand: Mwalimu alikumbana nayo katika harakati zake mara kadhaa za kunyamazisha watu na kuconsolidate power,. bahati yake ilikuwa nzuri alishinda, Mugabe alikutana nayo changamoto hii mara moja akashindwa!. Uchumi unapokuwa mbovu, maisha ya watu yakavurugika, tumaini la watu huwa ni kwa kuwa Katiba inasema utakaa muda fulani basi ngoja tuvumilie miaka ifike uondoke!. Lakini kama wanajua hutoki, basi Hidden hand na fikra za Watu kupitia Madirishani badala ya mlangoni zitakuja tu, na ole wako wafanikiwe wapite!
 
Back
Top Bottom