Mchango wa nani kisiasa wenye tija katika Taifa kati ya Zitto na dr. Slaa?

Status
Not open for further replies.

HAMY-D

JF-Expert Member
Sep 18, 2011
7,149
3,817
WanaJF,

Njia pekee ya kutambua mchango wa mwanasiasa kwa taifa ni kwa kutazama yale mazuri aliyofanya kwa taifa na kulifanya taifa kupata maslahi fulani zaidi na taifa kuwa PROUD na mwanasiasa huyo.

Kwa kuzingatia maelezo ya hapo juu, binafsi ningependa kuwa shuhuda wa mambo mema ambayo kijana Zitto amefanyia taifa letu. Mambo yenyeweni kama vile:

1) Kwanza kabisa nijirudishe kwenye suala la mgodi wa Buzwagi. Hapa naamini Tanzania itakuwa ikimshangilia kijana Zitto milele na milele.

Ni kijana Zitto ndiye aligundua uhujumu kwenye mgodi ule, ni kijana Zitto alisimamia lile sakata la Buzwagi mpaka ukweli kuhusu uhujumu ulipo thibitika.

2) Ni kijana Zitto ndiye mbunge pekee ambae anaongoza na upelekaji wa hoja binafsi bungeni zenye tija kwa taifa, hasa hoja za mambo ya nishati na madini, hoja za mambo ya kilimo n.k

3) Ni kijana Zitto ndiye alipelekea kuvunjwa kwa baraza la mawaziri kwa mara ya kwanza katika utawala wa Kikwete, hii ilitokana na kuwawajibisha mawaziri kadhaa wakati huo.

4) Ni kijana Zitto ndiye amepelekea wizara mbalimbali kulazimika kuandaa miswaada ili kuboresha sheria zetu kwenye mahala ambapo pana mapungufu ili sheria hizo ziendane na wakati uliopo na mazingira ya sasa.

5) Ni kijana Zitto ndiye alianzisha vuguvugu la vijana wengi wasomi kujihusisha na siasa. Itakumbukwa miaka ya nyuma siasa ilikuwa ikipuuzwa haswa na wasomi.

6) Ni Zitto ndiye alitoa hoja nzito bungeni na kusimamia hoja zake mpaka zikapelekea mhe. Kagasheki kujiuzuru na kusababisha mawaziri wengine kuvuliwa wadhifa wao wa uwaziri kama moja ya namna ya kuonyesha kuwajibika.

Kwa haya niliyoeleza hapa na ukilinganisha na mazuri aliyofanya Zitto kwa taifa, utagundua kuwa nimempunja mno kijana huyo, ila kwa uchache huu huu nadhani wengi mtakubaliana na mimi kuwa Zitto sio wa CHADEMA tena, Zitto ni wa Watanzania.

Sasa tukija kwa huyu babu Slaa na kutazama mchango wake kwa taifa, nakutana na mambo ya aibu aibu tu ndio yamefanywa na huyo babu. Kwa mfano ni kama vile:

1. Kuhamasisha vijana watumie GONGO.

2. Kuvunja ndoa za watu. Mfano ni ile ndoa ya Josephine.

3. Kusababisha vurugu na uvunjifu wa amani.

4. Kushusha mapato ya taifa kwa vurugu ambazo yeye ndio kinara wa kuzianzisha. Mfano mapato ya jiji la Arusha.

Kusema ukwili kabisa sioni zuri la Dr Slaa kwa taifa letu. Kama lipo liseme.

Kwa muktadha huu, Zitto ashikiki.
 
Unawashwa? Why CCM mko buzy na ZZK? nadhani dawa ni kunfukuza kabisa ndani ya CDM
 
CCM mnamuharibia Zitto, au kwa sababu ameshindwa kufanya kazi mliyomtuma ya kuisambaratisha chadema kabla ya 2014
 
Unawashwa? Why CCM mko buzy na ZZK? nadhani dawa ni kunfukuza kabisa ndani ya CDM

Suala la Zitto sio la kichama tena. Ni suala la kitaifa. Mimi kama Mtanzania nimeona waziwazi kuwa Zitto ana hujumiwa ndani ya CDM. Hivyo kumtetea ni kama nalipa fadhira kwa yale mazuri ambayo Zitto amefanyia taifa letu. Na wala CCM haipo hapo.
 
...mimi naona mchango wa zito ktk kujaribu kuharibu chama ni mkubwa sana na hakuna wa kulingananae.kwa upande wa ujenzi wa taifa uzalendo wa dr slaa na wanachadema woote wasio na usaliti ni mkubwa kuliko wabinafsi na ccm...
 
Unawashwa? Why CCM mko buzy na ZZK? nadhani dawa ni kunfukuza kabisa ndani ya CDM
Mkuu,
Yamekuwa hayo, hebu pinga kwa hoja juu ya sifa za ZZK zilizoorodheshwa hapo juu, twende kwa hoja sasa.

Pia, hebu kanusha juu ya hoja ya "gongo" aliyoitoa Slaa, twende kwa hoja.
 
Kama CCM mnaona mchango wa Zitto ni mkubwa na ni key player wa maendeleo ya Tz kwa nini msimchukue haraka badala ya kuleta hoja zenu humu?
Angalia foleni ya watu wanaosubili kuchukua kadi za Chadema baada ya mikutano ya Dr Slaa alafu tuambie ni wanachama wangapi Zitto anaingiza kwenye chama. Hapo Pima nani ana mchango mkubwa
 
Suala la Zitto sio la kichama tena. Ni suala la kitaifa. Mimi kama Mtanzania nimeona waziwazi kuwa Zitto ana hujumiwa ndani ya CDM. Hivyo kumtetea ni kama nalipa fadhira kwa yale mazuri ambayo Zitto amefanyia taifa letu. Na wala CCM haipo hapo.
Sasa kama ni la kitaifa zaidi mbona Zitto ni yule yule amendelea kutoa michango yake bungeni kama kawaida ? linalokuumiza zaidi ni lipi ? ongea bado husomeki
 
Ungelinganisha zitto na kiongozi mmoja ndani ya maccm, au dr. Slaa na kiongozi mmoja wa maccm tungekuelewa! Ndani ya CHADEMA viongozi wengi ni wazuri ukilinganisha na ccm! Poor you!
 
Kwanini CCM msimchukue Zitto Kabwe, ushabiki na kiherehere ni cha nini? Inamaana CCM hamna ajenda au Ajenda yenu ni Zitto na Chadema! Tunakatia mti Chini muda wowote aende akashiriki kuijenga CCM yenu!
 
WanaJF,

Njia pekee ya kutambua mchango wa mwanasiasa kwa taifa ni kwa kutazama yale mazuri aliyofanya kwa taifa na kulifanya taifa kupata maslahi fulani zaidi na taifa kuwa PROUD na mwanasiasa huyo.

Kwa kuzingatia maelezo ya hapo juu, binafsi ningependa kuwa shuhuda wa mambo mema ambayo kijana Zitto amefanyia taifa letu. Mambo yenyeweni kama vile:

1) Kwanza kabisa nijirudishe kwenye suala la mgodi wa Buzwagi. Hapa naamini Tanzania itakuwa ikimshangilia kijana Zitto milele na milele.

Ni kijana Zitto ndiye aligundua uhujumu kwenye mgodi ule, ni kijana Zitto alisimamia lile sakata la Buzwagi mpaka ukweli kuhusu uhujumu ulipo thibitika.

2) Ni kijana Zitto ndiye mbunge pekee ambae anaongoza na upelekaji wa hoja binafsi bungeni zenye tija kwa taifa, hasa hoja za mambo ya nishati na madini, hoja za mambo ya kilimo n.k

3) Ni kijana Zitto ndiye alipelekea kuvunjwa kwa baraza la mawaziri kwa mara ya kwanza katika utawala wa Kikwete, hii ilitokana na kuwawajibisha mawaziri kadhaa wakati huo.

4) Ni kijana Zitto ndiye amepelekea wizara mbalimbali kulazimika kuandaa miswaada ili kuboresha sheria zetu kwenye mahala ambapo pana mapungufu ili sheria hizo ziendane na wakati uliopo na mazingira ya sasa.

5) Ni kijana Zitto ndiye alianzisha vuguvugu la vijana wengi wasomi kujihusisha na siasa. Itakumbukwa miaka ya nyuma siasa ilikuwa ikipuuzwa haswa na wasomi.

6) Ni Zitto ndiye alitoa hoja nzito bungeni na kusimamia hoja zake mpaka zikapelekea mhe. Kagasheki kujiuzuru na kusababisha mawaziri wengine kuvuliwa wadhifa wao wa uwaziri kama moja ya namna ya kuonyesha kuwajibika.

Kwa haya niliyoeleza hapa na ukilinganisha na mazuri aliyofanya Zitto kwa taifa, utagundua kuwa nimempunja mno kijana huyo, ila kwa uchache huu huu nadhani wengi mtakubaliana na mimi kuwa Zitto sio wa CHADEMA tena, Zitto ni wa Watanzania.

Sasa tukija kwa huyu babu Slaa na kutazama mchango wake kwa taifa, nakutana na mambo ya aibu aibu tu ndio yamefanywa na huyo babu. Kwa mfano ni kama vile:

1. Kuhamasisha vijana watumie GONGO.

2. Kuvunja ndoa za watu. Mfano ni ile ndoa ya Josephine.

3. Kusababisha vurugu na uvunjifu wa amani.

4. Kushusha mapato ya taifa kwa vurugu ambazo yeye ndio kinara wa kuzianzisha. Mfano mapato ya jiji la Arusha.

Kusema ukwili kabisa sioni zuri la Dr Slaa kwa taifa letu. Kama lipo liseme.

Kwa muktadha huu, Zitto ashikiki.

Hapo kwenye namba 3 Zitto alisababisha baraza la mawaziri kuvunjwa baada ya mawaziri kupotoka.Leo Zitto kapotoKa maccm hawataki afukuzwe wala hawauoni upotofu wake kwa sababu wamemupandikiza wao kusambaratisha CHADEMA.
 
WanaJF,

Njia pekee ya kutambua mchango wa mwanasiasa kwa taifa ni kwa kutazama yale mazuri aliyofanya kwa taifa na kulifanya taifa kupata maslahi fulani zaidi na taifa kuwa PROUD na mwanasiasa huyo.

Kwa kuzingatia maelezo ya hapo juu, binafsi ningependa kuwa shuhuda wa mambo mema ambayo kijana Zitto amefanyia taifa letu. Mambo yenyeweni kama vile:

1) Kwanza kabisa nijirudishe kwenye suala la mgodi wa Buzwagi. Hapa naamini Tanzania itakuwa ikimshangilia kijana Zitto milele na milele.

Ni kijana Zitto ndiye aligundua uhujumu kwenye mgodi ule, ni kijana Zitto alisimamia lile sakata la Buzwagi mpaka ukweli kuhusu uhujumu ulipo thibitika.

2) Ni kijana Zitto ndiye mbunge pekee ambae anaongoza na upelekaji wa hoja binafsi bungeni zenye tija kwa taifa, hasa hoja za mambo ya nishati na madini, hoja za mambo ya kilimo n.k

3) Ni kijana Zitto ndiye alipelekea kuvunjwa kwa baraza la mawaziri kwa mara ya kwanza katika utawala wa Kikwete, hii ilitokana na kuwawajibisha mawaziri kadhaa wakati huo.

4) Ni kijana Zitto ndiye amepelekea wizara mbalimbali kulazimika kuandaa miswaada ili kuboresha sheria zetu kwenye mahala ambapo pana mapungufu ili sheria hizo ziendane na wakati uliopo na mazingira ya sasa.

5) Ni kijana Zitto ndiye alianzisha vuguvugu la vijana wengi wasomi kujihusisha na siasa. Itakumbukwa miaka ya nyuma siasa ilikuwa ikipuuzwa haswa na wasomi.

6) Ni Zitto ndiye alitoa hoja nzito bungeni na kusimamia hoja zake mpaka zikapelekea mhe. Kagasheki kujiuzuru na kusababisha mawaziri wengine kuvuliwa wadhifa wao wa uwaziri kama moja ya namna ya kuonyesha kuwajibika.

Kwa haya niliyoeleza hapa na ukilinganisha na mazuri aliyofanya Zitto kwa taifa, utagundua kuwa nimempunja mno kijana huyo, ila kwa uchache huu huu nadhani wengi mtakubaliana na mimi kuwa Zitto sio wa CHADEMA tena, Zitto ni wa Watanzania.

Sasa tukija kwa huyu babu Slaa na kutazama mchango wake kwa taifa, nakutana na mambo ya aibu aibu tu ndio yamefanywa na huyo babu. Kwa mfano ni kama vile:

1. Kuhamasisha vijana watumie GONGO.

2. Kuvunja ndoa za watu. Mfano ni ile ndoa ya Josephine.

3. Kusababisha vurugu na uvunjifu wa amani.

4. Kushusha mapato ya taifa kwa vurugu ambazo yeye ndio kinara wa kuzianzisha. Mfano mapato ya jiji la Arusha.

Kusema ukwili kabisa sioni zuri la Dr Slaa kwa taifa letu. Kama lipo liseme.

Kwa muktadha huu, Zitto ashikiki.

We kipofu kweli, kachukue ujira wako kwa aliyekutuma.
 
Suala la Zitto sio la kichama tena. Ni suala la kitaifa. Mimi kama Mtanzania nimeona waziwazi kuwa Zitto ana hujumiwa ndani ya CDM. Hivyo kumtetea ni kama nalipa fadhira kwa yale mazuri ambayo Zitto amefanyia taifa letu. Na wala CCM haipo hapo.

...acha kuleta utetezi dhaifu mkubwa mzima. Tulipopiga kelele kuhusu tembo na maliasili za tanzania mbona hamkuunga mkono na mpaka report ya kamati imewaumbua ndo mnajifanya wazalendo. Kama huyo dogo anahujumiwa machukue ukamfariji nyumbani kwako au muende ujerumani mkakamilishe uzalendo wa kula hela za walipakodi bila jasho...
 
Kwanini CCM msimchukue Zitto Kabwe, ushabiki na kiherehere ni cha nini? Inamaana CCM hamna ajenda au Ajenda yenu ni Zitto na Chadema! Tunakatia mti Chini muda wowote aende akashiriki kuijenga CCM yenu!

wewe una mchango gani chadema zaidi ya uropokaji? kadi yako ya uanachama bado imeandikwa kwa penseli. unaringia nini dogo wewe??
 
kwa nini anang'ang'ania Chadema?cdm hawamtaki kwani haki yake ipo chadema tu?kwa nini anashindana na boss wake slaa?kama ana umaarufu si aanzishe chama uzuri wafuasi anao wengi sana afanya kama hamadi wa CUF yuko ADC but huyu kijana hataki kutoka wamemvua nyazfa zake anangoja avuliwe uanachama?hapa naona kuna jambo nyuma ya pazia kwa nini wanamnadi zito kuliko chama yupo juu ya chama au ?
 
Kama CHADEMA hawamtaki ZZK nyie ccm mna mapenzi ya dhati na ZZK kwa nn msimchukue agombee uenyekiti kwenu ccm!!!
 
Hapa ndipo napata tabu na Ma-CCM, mbona mnalia sana na Zitto? Kama ni mtu mzuri, si mchukueni nyie? Umezungumzia Bugwazi, ni wabunge wa CCM wakishirikiana na Spika walimwondoa bungeni kwa kusema "Uongo". Leo ni MaCCM yanaleta hadithi za hoja nzuri "ya Buzwagi". SHAME ON YOU
 
Status
Not open for further replies.
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom