WanaJF,
Njia pekee ya kutambua mchango wa mwanasiasa kwa taifa ni kwa kutazama yale mazuri aliyofanya kwa taifa na kulifanya taifa kupata maslahi fulani zaidi na taifa kuwa PROUD na mwanasiasa huyo.
Kwa kuzingatia maelezo ya hapo juu, binafsi ningependa kuwa shuhuda wa mambo mema ambayo kijana Zitto amefanyia taifa letu. Mambo yenyeweni kama vile:
1) Kwanza kabisa nijirudishe kwenye suala la mgodi wa Buzwagi. Hapa naamini Tanzania itakuwa ikimshangilia kijana Zitto milele na milele.
Ni kijana Zitto ndiye aligundua uhujumu kwenye mgodi ule, ni kijana Zitto alisimamia lile sakata la Buzwagi mpaka ukweli kuhusu uhujumu ulipo thibitika.
2) Ni kijana Zitto ndiye mbunge pekee ambae anaongoza na upelekaji wa hoja binafsi bungeni zenye tija kwa taifa, hasa hoja za mambo ya nishati na madini, hoja za mambo ya kilimo n.k
3) Ni kijana Zitto ndiye alipelekea kuvunjwa kwa baraza la mawaziri kwa mara ya kwanza katika utawala wa Kikwete, hii ilitokana na kuwawajibisha mawaziri kadhaa wakati huo.
4) Ni kijana Zitto ndiye amepelekea wizara mbalimbali kulazimika kuandaa miswaada ili kuboresha sheria zetu kwenye mahala ambapo pana mapungufu ili sheria hizo ziendane na wakati uliopo na mazingira ya sasa.
5) Ni kijana Zitto ndiye alianzisha vuguvugu la vijana wengi wasomi kujihusisha na siasa. Itakumbukwa miaka ya nyuma siasa ilikuwa ikipuuzwa haswa na wasomi.
6) Ni Zitto ndiye alitoa hoja nzito bungeni na kusimamia hoja zake mpaka zikapelekea mhe. Kagasheki kujiuzuru na kusababisha mawaziri wengine kuvuliwa wadhifa wao wa uwaziri kama moja ya namna ya kuonyesha kuwajibika.
Kwa haya niliyoeleza hapa na ukilinganisha na mazuri aliyofanya Zitto kwa taifa, utagundua kuwa nimempunja mno kijana huyo, ila kwa uchache huu huu nadhani wengi mtakubaliana na mimi kuwa Zitto sio wa CHADEMA tena, Zitto ni wa Watanzania.
Sasa tukija kwa huyu babu Slaa na kutazama mchango wake kwa taifa, nakutana na mambo ya aibu aibu tu ndio yamefanywa na huyo babu. Kwa mfano ni kama vile:
1. Kuhamasisha vijana watumie GONGO.
2. Kuvunja ndoa za watu. Mfano ni ile ndoa ya Josephine.
3. Kusababisha vurugu na uvunjifu wa amani.
4. Kushusha mapato ya taifa kwa vurugu ambazo yeye ndio kinara wa kuzianzisha. Mfano mapato ya jiji la Arusha.
Kusema ukwili kabisa sioni zuri la Dr Slaa kwa taifa letu. Kama lipo liseme.
Kwa muktadha huu, Zitto ashikiki.
Njia pekee ya kutambua mchango wa mwanasiasa kwa taifa ni kwa kutazama yale mazuri aliyofanya kwa taifa na kulifanya taifa kupata maslahi fulani zaidi na taifa kuwa PROUD na mwanasiasa huyo.
Kwa kuzingatia maelezo ya hapo juu, binafsi ningependa kuwa shuhuda wa mambo mema ambayo kijana Zitto amefanyia taifa letu. Mambo yenyeweni kama vile:
1) Kwanza kabisa nijirudishe kwenye suala la mgodi wa Buzwagi. Hapa naamini Tanzania itakuwa ikimshangilia kijana Zitto milele na milele.
Ni kijana Zitto ndiye aligundua uhujumu kwenye mgodi ule, ni kijana Zitto alisimamia lile sakata la Buzwagi mpaka ukweli kuhusu uhujumu ulipo thibitika.
2) Ni kijana Zitto ndiye mbunge pekee ambae anaongoza na upelekaji wa hoja binafsi bungeni zenye tija kwa taifa, hasa hoja za mambo ya nishati na madini, hoja za mambo ya kilimo n.k
3) Ni kijana Zitto ndiye alipelekea kuvunjwa kwa baraza la mawaziri kwa mara ya kwanza katika utawala wa Kikwete, hii ilitokana na kuwawajibisha mawaziri kadhaa wakati huo.
4) Ni kijana Zitto ndiye amepelekea wizara mbalimbali kulazimika kuandaa miswaada ili kuboresha sheria zetu kwenye mahala ambapo pana mapungufu ili sheria hizo ziendane na wakati uliopo na mazingira ya sasa.
5) Ni kijana Zitto ndiye alianzisha vuguvugu la vijana wengi wasomi kujihusisha na siasa. Itakumbukwa miaka ya nyuma siasa ilikuwa ikipuuzwa haswa na wasomi.
6) Ni Zitto ndiye alitoa hoja nzito bungeni na kusimamia hoja zake mpaka zikapelekea mhe. Kagasheki kujiuzuru na kusababisha mawaziri wengine kuvuliwa wadhifa wao wa uwaziri kama moja ya namna ya kuonyesha kuwajibika.
Kwa haya niliyoeleza hapa na ukilinganisha na mazuri aliyofanya Zitto kwa taifa, utagundua kuwa nimempunja mno kijana huyo, ila kwa uchache huu huu nadhani wengi mtakubaliana na mimi kuwa Zitto sio wa CHADEMA tena, Zitto ni wa Watanzania.
Sasa tukija kwa huyu babu Slaa na kutazama mchango wake kwa taifa, nakutana na mambo ya aibu aibu tu ndio yamefanywa na huyo babu. Kwa mfano ni kama vile:
1. Kuhamasisha vijana watumie GONGO.
2. Kuvunja ndoa za watu. Mfano ni ile ndoa ya Josephine.
3. Kusababisha vurugu na uvunjifu wa amani.
4. Kushusha mapato ya taifa kwa vurugu ambazo yeye ndio kinara wa kuzianzisha. Mfano mapato ya jiji la Arusha.
Kusema ukwili kabisa sioni zuri la Dr Slaa kwa taifa letu. Kama lipo liseme.
Kwa muktadha huu, Zitto ashikiki.