SULEIMAN ABEID
JF-Expert Member
- Feb 26, 2013
- 390
- 385
Mheshimiwa Spika, Maeneo mengi muhimu ya kijamii na kiuchumi kutotungiwa Sheria mahsusi na badala yake kutumika matamko ya baadhi ya viongozi na watendaji wa Serikali
(a) Mheshimiwa Spika, Biashara za Machinga, Bodaboda, Mama Ntilie, Wauza mbogamboga kundi hili liko kwenye hekaheka kila leo mara hawa wasionekane mjini, mara wafukuzwe na kuhamishwa, mara hawaruhusiwi kufanya biashara sehemu fulani, mara kupangwa katika maeneo maalum na hivyo biashara zao kutegemea matamko ya viongozi kila uchao hali inayowaletea usumbufu mkubwa na wengi kuishia kufilisika.
(b) Mheshimiwa Spika, Kundi la Vijana na Ajira, hakuna sheria inayomuongoza kijana kupata ajira na masharti ya ajira yanabadilika kila tangazo la ajira linapotoka, mara ajira zitapatikana kwa usaili (Interview), mara kwa kuchaguana tu, mara ukiomba upande huu huruhusiwi kuomba upande mwingine, mara umri huu hautakiwi, mara lazima uwe umepitia JKT, huku wakijua vijana wengi hawapati fursa hiyo na wakati mwingine ajira kutolewa kwa upendeleo hali iliyopelekea Serikali kulalamikiwa kwa kiwango kikubwa.
Mheshimiwa Spika, Ili kuondoa matamko na utashi binafsi kuwa mbadala wa Sheria, ni muhimu maeneo nyeti yatambuliwe na kutungiwa Sheria mahususi kwa mustakabali wa maendeleo ya Taifa na kuondoa bugudha na usumbufu unaojitokeza mara kwa mara kwenye jamii zetu.
(a) Mheshimiwa Spika, Biashara za Machinga, Bodaboda, Mama Ntilie, Wauza mbogamboga kundi hili liko kwenye hekaheka kila leo mara hawa wasionekane mjini, mara wafukuzwe na kuhamishwa, mara hawaruhusiwi kufanya biashara sehemu fulani, mara kupangwa katika maeneo maalum na hivyo biashara zao kutegemea matamko ya viongozi kila uchao hali inayowaletea usumbufu mkubwa na wengi kuishia kufilisika.
(b) Mheshimiwa Spika, Kundi la Vijana na Ajira, hakuna sheria inayomuongoza kijana kupata ajira na masharti ya ajira yanabadilika kila tangazo la ajira linapotoka, mara ajira zitapatikana kwa usaili (Interview), mara kwa kuchaguana tu, mara ukiomba upande huu huruhusiwi kuomba upande mwingine, mara umri huu hautakiwi, mara lazima uwe umepitia JKT, huku wakijua vijana wengi hawapati fursa hiyo na wakati mwingine ajira kutolewa kwa upendeleo hali iliyopelekea Serikali kulalamikiwa kwa kiwango kikubwa.
Mheshimiwa Spika, Ili kuondoa matamko na utashi binafsi kuwa mbadala wa Sheria, ni muhimu maeneo nyeti yatambuliwe na kutungiwa Sheria mahususi kwa mustakabali wa maendeleo ya Taifa na kuondoa bugudha na usumbufu unaojitokeza mara kwa mara kwenye jamii zetu.