Mchango wa Askofu Gwajima leo nilitamani yawe mawazo ya Rais

kibaravumba

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
6,635
7,005
Kusema kweli nimeguswa sana na Gwaji boy kiasi kwamba pamoja na mapungufu yake yaliyonifanya nisimuheshimu tena, umenifungua akili na kunifanya nirudi nyuma kutafakari upya jinsi ninavyomchukulia.

Ijapo aligusia tu kama mfano,wazo la kuhakikisha kila mtanzania anayeweza kusoma hadi chuo kikuu apewe nafasi, wakati akizungumzia taifa kuwa na vision, jambo hilo limenigusa sana kwa kuwa ninawafahamu watu wengi wenye uwezo wa kiakili, ila kutokana na sera isiyo rafiki ya elimu,wameshindwa kufikia ndoto zao za kufika chuo kikuu.Kikwazo kikiwa ni gharama kubwa mno kwa mtanzania wa kawaida.

Kipo chama cha upinzani kilikuwa na sera hii kwamba kingehakikisha kila mtanzania mwenye uwezo wa kusoma anasoma hadi atakapoamua kuchoka mwenyewe.

Taifa linakosa wasomi wa kweli kwani hakuna ushindani wa kweli katika elimu,na matokeo yake wale wachache waliopata bahati ya elimu ya chuo kikuu,kazi yao imekuwa kuitumia kama kitu cha kutambia mtaani tu huku wakishindwa kuonesha tofauti,jambo lililoamsha kasi ya mbunge mmoja anayejiita LY kuwaponda hadi maprof. kila wanapoongea kwa kuwa wanaonekana kutokuwa na faida inayoonekana na wakihisiwa ni watu waliojipanga kupiga dili tu kwa jina la usomi wao, huku wakikejeli kuhojiwa na watu wasio na elimu.

Natamani mawazo ya Gwajima yangekuwa ya Rais wetu akaliona hilo. Wasomi wakiwa wengi watashindana kuwa wabunifu kama wachezaji wanavyogombania namba kwenye timu.Tofauti na sasa,wale wachache wanashindwa kuwa wabunifu na ndio maana wanadharauliwa tu na wanaojiita LY.

Unaweza kuchukua tu mfano mtu ni LY anasomesha watoto wake zaidi ya watano kwa level za degree, lakini wanaporudi nyumbani,anasikitika kuwa walipoteza muda kwani wanarudi nyumbani wakiwa hawana uwezo wowote kukabiliana na mazingira wanayoyakuta nyumbani na mtaani.Aliyesomesha anabaki kuhoji,ni utafiti upi na nani aliufanya ulioonesha ni lazima watu wote wasome mwaka mzima kabla ya kuongia darasa jingine!

Gwajima leo umenigusa sana
 
Mawazo hayo yanapaswa yawe Kwenye katiba na yatoholewe kutoka Kwenye katiba na kuwekwa Kwenye Sera ya nchi Kwa kunyambuliwa ili iwe dira ya Taifa

Kwa maana nyingine,swala la katiba mpya halikwepeki kama Kweli tunapaswa kusonga mbele
 
Unaposema unatamani alichoongea kiwe mawazo ya rais usitie shaka maana yeye ni msaidizi wa rais na anashiriki kwenye kufanya kazi za rais

Gwaji yupo smart sana siku zote.... hakuna mjinga anaweza kuwa na waumini wengi kiasi cha waumini wa Gwaji
 
Kuna elimu na maarifa, watu wakipata mazingira bora tunahitaji wachache elimu ya juu.wengi kada ya kati na chini elimu ya msingi.
Nilichomsoma mimi Ask. Gwajima ni pale aliposema lazima tutafsiri maendeleo yetu sisi wenyewe; sio kunakili kutoka kwa watu wengine.
Tunaweza kupanga kwamba elimu ya msingi ni kuanzi daraja fulani mpaka fulani.

Shida iliyopo ni muunganiko na ushikamanishaji wa hayo maono na walengwa, yaani wananchi. Maono yakibaki kwenye makaratasi, unabaki kuwa wimbo wa viongozi na watumishi wachache huku wananchi tukibaki ‘kusikiaga’ tu!

Maono yanawekwa yanabaki yakivunda kwenye makaratasi, mpaka tunajisahau wakati mwingine, sheria, matamko na sera havichezi mdundo mmoja.
 
Unaposema unatamani alichoongea kiwe mawazo ya rais usitie shaka maana yeye ni msaidizi wa rais na anashiriki kwenye kufanya kazi za rais

Gwaji yupo smart sana siku zote.... hakuna mjinga anaweza kuwa na waumini wengi kiasi cha waumini wa Gwaji
Waumini? Saa zingine tuache kufuru mchezesha chekundu na cheusi akiwa na kundi kubwa limemzunguka unamsifu?
Sawa na bunge linapopiga makofi mengi wakati Spika kauliza mtamchagua Kibajaji kuwa Mneki
 
Waumini? Saa zingine tuache kufuru mchezesha chekundu na cheusi akiwa na kundi kubwa limemzunguka unamsifu?
Sawa na bunge linapopiga makofi mengi wakati Spika kauliza mtamchagua Kibajaji kuwa Mneki

Watu ndio mtaji mkubwa kwenye siasa... Gwaji ana wengi sanaaa

Kama unaona uko smart zaidi yake au unaona hayuko smart basi nawewe jenga kundi kubwa walau linalokuelewa tuu walau hapa jf......
 
Natamani mawazo ya Gwajima yamgekuwa ya Rais wetu akaliona hilo.
Wasomi wakiwa wengi watashindana kuwa wabunifu kama wachezaji wanavyogombania namba kwenye timu.Tofauti na sasa,wale wavhache wanashindwa kuwa wabunifu na ndio maana wanadharauliwa tu na wamaojiita LY.
Mkuu, kiujumla sipingani na mawazo yako na huyo Gwajiboy wako. Lakini sioni mantiki hasa ya haya unayoyaandika hapa.

Chukulia hicho kipande nilichonyanyua na kukibandika hapo juu.

Kwani uhalisia wake upo wapi?

"Ushindani"? upi tena? Michujo si ndiyo hiyo inayofanyika toka primari, sekondari, na kuendelea?

Ushindani? Kwani kuna uhaba wa watu waliomaliza vyuo vikuu tena hapa nchini siku hizi? Si ndio hao wengine wengi tu tunaowaona wanahangaika kila kona kutafuta ajira bila mafanikio yoyote/ Kwani hawa hawa hawatoi ushindani kwa wenzao wanaopata nafasi za kazi, hadi wapatikane wengi kiasi gani?

Mimi ningeelewa vizuri sana mada yako, pamoja na huyo Gwaji Boy, kama mngekazia zaidi pawepo na elimu madhubuti katika ngazi zote, tokea primari hadi vyuo vikuu, ili wahitimu wake wawe wameiva hasa na kuwa na uelewa wa kutosha kabisa kuyakabili mazingira yao popote walipo.
Kama ni ushindani, hawa ndio wangetoa ushindani wa kweli na wa manufaa zaidi kwa taifa letu.

Lakini ushindani wa mamilioni ya wahitimu waliojaa ujinga? Huo sio ushindani mkuu wangu.
 
Gwajima,nenda kasome Tanzania development vision 2025.Iko tangu enzi ya Mkapa.
Yote aliyoongea yamo humo.Hakuna jipya aliloongea.Shida yetu utekelezaji ila mipango tuu aaah!

Hayo yote aliyoyasema Gwajima yamo kwenye mipango ya maendeleo ya Taifa hili. Na miaka yote hii serikali ya chama cha Mapinduzi ndio inatawala; kwanini ccm haihakikishi kuwa serikali yake inatekeleza vision ya Taifa?

Whatever the vision; mipango yote huwa inapitishwa na bunge, kusingizia kuwa Marais kila mmoja anakuja na mipango yake ni kukili kuwa muhimili wa BUNGE unaotakiwa kupitisha budget za mipango yote ni DHAIFU!!! IT IS BECAUSE OF OUR WEAK INSTITUTIONS THAT THE GOVERNMENT DOES NOT FOLLOW THE TENETS OF GOOD GOVERNANCE WHICH INCLUDE, THE FOLLOWING OF THE RULE OF LAW. This is where the rub is! TAASISI ZETU LIKIWEMO BUNGE NI DHAIFU SANA.
 
Watu ndio mtaji mkubwa kwenye siasa... Gwaji ana wengi sanaaa

Kama unaona uko smart zaidi yake au unaona hayuko smart basi nawewe jenga kundi kubwa walau linalokuelewa tuu walau hapa jf......
LOOoo, ni ngumu sana kukinzana na hili!

Hasa inapojulikana kwamba hata kundi la wajinga ni kundi pia!

Mtu yeyeote anaweza kuwa na kundi kubwa nyuma yake kwa sababu mbalimbali hata zisizokuwa na manufaa katika jumuia kiujumla.

Unajua, hata akina Hitler nao walikuwa na kundi kbwa sana nyuma yao! Angalia yaliyotokea!
 
LOOoo, ni ngumu sana kukinzana na hili!

Hasa inapojulikana kwamba hata kundi la wajinga ni kundi pia!

Mtu yeyeote anaweza kuwa na kundi kubwa nyuma yake kwa sababu mbalimbali hata zisizokuwa na manufaa katika jumuia kiujumla.

Unajua, hata akina Hitler nao walikuwa na kundi kbwa sana nyuma yao! Angalia yaliyotokea!

Wajinga nao watu.....

Na kwa hao wajinga unaowaona kwenye kundi kipo wanachokiona kina manufaa kwao hata kama kwako hakina

Nguvu ya siasa ni umma.... haijalishi ni siasa ya aina gani
 
Wajinga nao watu.....

Na kwa hao wajinga unaowaona kwenye kundi kipo wanachokiona kina manufaa kwao hata kama kwako hakina

Nguvu ya siasa ni umma.... haijalishi ni siasa ya aina gani
Na kweli kwako haijalishi ni siasa za aina gani. Ndio maana ukawa mshabiki wa siasa za kidhalimu za jiwe, kwasababu alihakikisha anasujudiwa na kundi la wajinga, waoga na wasaka fursa.
 
Watu ndio mtaji mkubwa kwenye siasa... Gwaji ana wengi sanaaa

Kama unaona uko smart zaidi yake au unaona hayuko smart basi nawewe jenga kundi kubwa walau linalokuelewa tuu walau hapa jf......
Tungekuwa bungeni nigekuita wa lasaba f"
 
Mtu yeyote mwenye mawazo ya Umagufuli lazima aguse mioyo ya Watanzania wazalendo.
yaani watu hawawez ku think out of kivuli cha magufuli? this is bullshit.
si kila mawazo yanatokana na magufuli. acha kulazimisha watu watembelee kivuli cha wafu.
R.I.P rais wetu JPM
 
Back
Top Bottom