Mchanganyiko huu ni dawa ya haraka sana ya kuondoa mafua, kufungua kifua

Oct 14, 2011
49
44
Wadau nimeona ku-share na nyie jambo hili huenda ikawa sababu ya kusaidia kuokoa uhai wa watu wanaosumbuliwa na maradhi hayo, ikumbukwe kwa sasa Dunia inapita kwenye taharuki kubwa ya ugonjwa unao sababishwa na virusi vya Corona, na watu wamekuwa wakitumia njia mbalimbali kujinusuru na janga hilo, siku ya ijumaa nilipata taharuki kidogo nilipo amka asubuhi mwenza wangu alikuwa ana joto kali sana, mafua makali na pia alikuwa analalamika kifua kinambana.

Nilipata khofu sana maana ni miongoni mwa dalili na hili janga la sasa, ukizingatia mwenzangu huyo anafanya kazi hospital kubwa sana hapa nchini, kama mwanaume niliona ngojea nijiongeze ili kuweza kumnusuru mwenzangu, so nilienda duka la dawa nikanunua vicks ya kikopo, pia nikaenda duka la dawa za asili nikanunua dawa inaitwa COGONI, nikarudi home, nikachukua vitunguu Swaumu vya kiasili 2 nikaponda, na mbegu za Habbat sawda (black seed), nikachemshwa mchanganyiko wa vitunguu Swaumu, Habbat sawda na vicks.

Baada ya hapo, nikaweka matone 5 ya COGONI nikampa ajifushe, wadau ndani ya dakika 5, mafua yalikata kifua kikaachia, akawa mzima wa afya, nashauri wadau ambaye atakuwa amepata dalili hizo ajaribu na yeye kutumia njia hii huenda ikawa msaada kwake.

Asanteni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwa walokwisha rasimisha mahusiano (me/ke) dawa ni kufanya kale kamchezo mara kwa maraaa na kunywa chai ya tangawizi yenye iliki, mdalasini na karafuuu
Lovebird, na hofu ya huu ugonjwa, unadhani hata magobole yanasimama vizuri? Ukihisi muwasho kwenge Koo, unatafuna Hadi msasa ili kuwaondoa hao kina kolona kooni. Halafu wazee ndio huyo kolona anawaonea Sana.

Wake na watoto wamekuwa wanakuzunguka, wanakutia moyo, lakini hofu ni kubwa
 
Jamani mwenzenu hapa nilipo sielewi, majuzi nilipatwa na mafua makali nikayadhibiti vya kutosha na yakanitii lkn sasa usiku wa leo kuanzia ile saa tisa nitashikwa na tumbo naendesha ni balaa hii imekaaje au ni mchanganyiko wa dawa niloutumia ndo umenipiga tumbo nn....!!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo ndio COGONI
IMG_20200503_064328_4.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Habbat sawda ni dawa ambayo waislamu wanaijua vizuri, mtume Muhammad (SAW) aliwahi nukuliwa akisema dawa hiyo inatibu maradhi yote isipokuwa kifo tu, so nikajalibu kuchanganya dawa nyengine zinazosaidia mfumo wa upumuaji,vicks, kitunguu Swaumu na COGONI, ili nipate matokeo Mazuri, na kwa hakika nilishangazwa sana na matokeo yake, ata mgonjwa akutegemea hali ingekuwa vile, Alhamdulillah
nini kilikufanya udhani kua hiyo itakua ni tiba

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom