Mkuu, Mchanga si sehemu(ya chakula/virutubisho) vinavyohitajika mwilini na hivyo basi, uwepo wake katika mwili huweza kusababisha madhara mbali mbali..hii yaweza kuwa kwa wale binadamu wenye kutumia mchanga makusudi kama chakula(mf. watoto, wajawazito, baadhi ya magonjwa kama Pica) au kwa bahati mbaya kama ulivyosema katika baadhi ya vyakula wali, mboga n.k
Madhara hayo ni pamoja na haya;
-Kuharibu meno(hasa katika utafunaji)
-Mchanga unakwaruza/kwangua katika sehemu ya tumbo, utumbo n.k
-Magonjwa(tumbo, minyoo) hasa kutokana na wanyama tunaowafuga na wale wa porini kuweza kuacha vimelea, mayai katika udongo).
-Mwishoni, kuna tatizo linaloitwa Appendicitis, ambapo sehemu ile mchanga ulipokuwa ukihifadhiwa(ingawa hauhitajiki) kujaa/kujiviringa/n k kutokea.
Muhimu ni kuepuka kutumia mchanga/vitu vinavyofanana na hivyo mfano Chaki(Chalk), udongo kina mama wajawazito wanaoutumia wakati wa mimba "pemba", majivu, vipande vidogo vya miti(magome), n.k kwa njia ya
-Kuwachunga(kuwaangalia) watoto wadogo.
-Kusafisha vyakula vizuri na kwa umakini kama mboga za majani, mchele n.k
- Kuwasaidia wajawazito kutotumia udongo kwa mazoea.
-Kutafuta msaada wa kiafya hali inapozidi(kula udongo).
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.