Ndagafumuni
Member
- Jul 26, 2018
- 7
- 5
Mchambuzi wa siasa za Afrika Mashariki, Dkt. Gakere Gathoni amesema demokrasia imetumika kumuondoa madarakani aliyekua Meya wa Jiji la DSM, Isaya Mwita.
Madiwani wa Jiji hilo walipiga kura ya kutokua na Imani na Meya huyo kutokana na kile walichoeleza kuwa ni matumizi mabaya ya ofisi.
"Demokrasia inatakiwa itumike kuleta maendeleo, Pindi kiongozi akishindwa kuleta maendeleo, inapaswa aondolewe madarakani kama ilivyotokea kwa Meya wa DSM" alisema Dkt. Gathoni
Alisema kitendo cha Meya huyo kutembelea gari kubwa, kutumia fedha nyingi kuliko mshahara wake kinaashiria kuwa alikua akiwakamua wakazi wa Dar.
"Katika tasnifu yangu ya Shahada ya Uzamili nilikua nikiangalia jinsi wananchi wanavyotozwa fedha na serikali za mitaa kwa kushirikiana na serikali ya Jiji.
"Kwa bahati mbaya niligundua mitaa yenye viongozi kutoka vyama pinzani hali ilikua mbaya sana." alisema
Alisema katika utafiti wake huo wa Shahada ya Uzamili, aliwahi kwenda ofisi ya Meya ili apate ufafanuzi lakini alinyomwa taarifa.
"Kitendo cha kuninyima taarifa ni kuzuia Uhuru wa taarifa, pia ni jambo linalotia shaka kuhusu uongozi wake" alisema
Sent using Jamii Forums mobile app
Madiwani wa Jiji hilo walipiga kura ya kutokua na Imani na Meya huyo kutokana na kile walichoeleza kuwa ni matumizi mabaya ya ofisi.
"Demokrasia inatakiwa itumike kuleta maendeleo, Pindi kiongozi akishindwa kuleta maendeleo, inapaswa aondolewe madarakani kama ilivyotokea kwa Meya wa DSM" alisema Dkt. Gathoni
Alisema kitendo cha Meya huyo kutembelea gari kubwa, kutumia fedha nyingi kuliko mshahara wake kinaashiria kuwa alikua akiwakamua wakazi wa Dar.
"Katika tasnifu yangu ya Shahada ya Uzamili nilikua nikiangalia jinsi wananchi wanavyotozwa fedha na serikali za mitaa kwa kushirikiana na serikali ya Jiji.
"Kwa bahati mbaya niligundua mitaa yenye viongozi kutoka vyama pinzani hali ilikua mbaya sana." alisema
Alisema katika utafiti wake huo wa Shahada ya Uzamili, aliwahi kwenda ofisi ya Meya ili apate ufafanuzi lakini alinyomwa taarifa.
"Kitendo cha kuninyima taarifa ni kuzuia Uhuru wa taarifa, pia ni jambo linalotia shaka kuhusu uongozi wake" alisema
Sent using Jamii Forums mobile app