MrFroasty
JF-Expert Member
- Jun 23, 2009
- 1,195
- 590
Asalamaleykum,
Nashauri Waislamu kwa umoja wao na wote wapenda haki dunia nzima kuanza mchakato wa kushinikiza Serikali ya Tanzania na Zanzibar kuwatoa waislamu walioko magerezani. Tunajua masheikh kama wa UAMSHO wako ndani kwa sababu zisizoeleweka/kisiasa zaidi.
Mchakato huu utakuwa na mipango ya hatua ya umoja kama waislamu na kuna mambo mengi yanaweza kufanywa na individuals yaani katika hatua ya mtu binafsi (mifano itafuata hapo chini). Tupange maandamano na kuwasilisha malalamiko yetu kwenye wizara za mambo ya nchi za nje siku ya ramadhan ya mwanzo ya 2021 inshallah kwa njia mtu binafsi kufika ofisini na kuwasilisha kwa barua. Hususan nchi za kiislamu, lakini hata za kimagharibi wanafahamu umuhimu wa haki za binadamu.
Hatua za kuchukuliwa na mtu kibinafsi:
Maasalaam.
Nashauri Waislamu kwa umoja wao na wote wapenda haki dunia nzima kuanza mchakato wa kushinikiza Serikali ya Tanzania na Zanzibar kuwatoa waislamu walioko magerezani. Tunajua masheikh kama wa UAMSHO wako ndani kwa sababu zisizoeleweka/kisiasa zaidi.
Mchakato huu utakuwa na mipango ya hatua ya umoja kama waislamu na kuna mambo mengi yanaweza kufanywa na individuals yaani katika hatua ya mtu binafsi (mifano itafuata hapo chini). Tupange maandamano na kuwasilisha malalamiko yetu kwenye wizara za mambo ya nchi za nje siku ya ramadhan ya mwanzo ya 2021 inshallah kwa njia mtu binafsi kufika ofisini na kuwasilisha kwa barua. Hususan nchi za kiislamu, lakini hata za kimagharibi wanafahamu umuhimu wa haki za binadamu.
Hatua za kuchukuliwa na mtu kibinafsi:
- Kususa kununua bidhaa yoyote itokayo Tanzania katika hatua ya vyakula kama kahawa, chai, chocolate, korosho n.k
- Kususa kupanda vyombo vya usafiri vya serikali kama ndege za serikali.
- Kususa kutumia mawasiliano mitandao ya kiserekali.
- Kususa kwenda matembezi TZ kwa mapumziko na kuchagua nchi zengine (hususan diaspora)
- Kususa kutuma pesa kwa njia za benki na badala yake kutumia njia za mashirika mengine kama western union (hususan diaspora)
- Kususa kwenda hospitali za serekali
- Kususa kupeleka watoto wapya maskuli ya serikali na kutumia ya watu binafsi
Maasalaam.