Mchakato wa kuwania urais ndani ya CCM mwaka 1995

Sungi

Senior Member
Apr 29, 2009
149
47
Wakubwa - hivi wangapi mnakumbuka majina ya wagombea wa urais kupitia CCM mwaka 1995 kwenye round ya kwanza? Nakumbuka walikuwa wanne, Msuya, Mkapa, Kikwete na nimesahau wanne, kabla ya mchujo walipobaki Kikwete, Mkapa na Msuya. Ninaandika paper fulani hapa na ningependa kukumbushwa.

Asanteni
 
Wakubwa - hivi wangapi mnakumbuka majina ya wagombea wa urais kupitia CCM mwaka 1995 kwenye round ya kwanza? Nakumbuka walikuwa wanne, Msuya, Mkapa, Kikwete na nimesahau wanne, kabla ya mchujo walipobaki Kikwete, Mkapa na Msuya. Ninaandika paper fulani hapa na ningependa kukumbushwa.

Asanteni

Mkuu heshima mbele kwa kujaribu kutoa mchango wako kwa kuweka historia mahali pake. Lakini nina wasi wasi na kitu unachotaka kuandika kuwa kinaweza kikapindisha hiyo historia kutokana na lugha ilivyokaa kwenye hili bandiko lako.

kwanza sio kweli kuwa round ya kwanza ilikuwa na wagombea wanne, sijui unaposema round ya kwanza unamaanisha katika hatua/kikao kipi.

kwasababu waliochukua form na kizirejesha walikuwa wana CCM 17 hapo mimi ndio napaona ndio pa kupaita round ya kwanza, kati ya hao alikuwepo mwanamke 1, baada ya kikao cha kamati kuu wagombea wawili majina yao yaliondolewa kwa kukosa kutimiza msharti, yakabaki majina 15 ambayo hayo yalipelekwa NEC. Na baada ya hapo mchujo uliendela hatimaye ngazi ya Mkutano mkuu wa Taifa.

Ninachojua round zilikuwa kama ifuatavyo. 17 -15-10-5-3-2-1
Kwa hiyo katika 3 bora walikuwepo Msuya, Ben na JK round ya kwanza ya tatu Bora aliongoza JK na msuya alikuwa wa mwisho, kwa vile JK hakupata zaidi ya 50% ya kura zote ilibidi uchaguzi urudiwe kwa kumuondoa mjumbe liyekuwa ameshika nafasi ya 3 Mzee Msuya. JK alikuwa akiungwa mkono na kundi kubwa la vijana (ambao awali walikuwa wamegawanyika kambi 2 moja ya JK na nyingine ya EL lakini baada ya jina la EL kuondolewa kwenye NEC vijana waliomuunga mkono EL walihamia kwa JK) EL ndiye aliyempa Lift ya ndege ya kukodi JK kukusanya sahihi 1000 kutoka mikoa ya Tanzania Bara na Visiwani ya wanachama wa kumdhamini kugombea Urais, na Msuya alikuwa chaguo la wazee, kwa kumuondoa Msuya wazee waliokuwa wanamuunga mkono walihamia kwa Ben ambaye alionekana anaendana na sera zao kiasi ukilinganisha na JK na pia walimuona amekomaa na inaonekana KNM wa kivinje alishawanong'oneza wanakamati kuwa JKN anamtaka BWM.
 
Huo mchakato siwezi kuusahau hasa pale watanzania tulpoona na kushuhudia role ya mwalimu katika siasa za nchi hii, big up mwalimu!
 
Nalikumbuka jina la John Samuel Malecela aka Tingatinga ambaye this time Mwalimu mwenyewe alipiga chini!
Wakuu hivi ile ya Kikwete kutofikisha asilimia zaidi ya 50 ya kura ilikuwepo kwenye katiba ya CCM au lilikuwa ni zengwe tu la Nyerere?
 
Nyerere alifanya janja moja ambayo baadhi ya watu wanaamini ilimsaidia Mkapa kupita. Baada ya kupigwa kwa kura, Nyerere alikataa kutaja kura za kila mtu na badala walitaja tu Msuya kushika nafasi ya tatu na hivyo kutolewa.

Ni kawaida kwa mwanadamu kwenda upande wa mshindi, kuna watu wanaamini laiti kura zote zingetajwa kama ilivyo kawaida, huenda watu wengi kutoka kambi ya Msuya wangemuunga mkono JK kwenye round ya mwisho.

Pia kulikuwa na kundi la Wazanzibar ambalo lilimwunga mkono Msuya na kuwa na makubaliano kwamba Omar Juma angelikuwa makamu wa rais. Baada ya Msuya kutolewa, kundi la Mkapa liliwafuata Wazanzibari na kuahidi kumteua Omar Juma kuwa makamu wa rais. Kundi zima la Zanzibar likahamia kwa Mkapa.

JK kutokufikisha asilimia 50 ilikuwepo kwenye katiba na bado ipo. Mwaka 2005 JK alipita 50% kwenye round ya kwanza hivyo hakukuwa na haja ya kubakiza wagombea wawili.
 
Nyerere alifanya janja moja ambayo baadhi ya watu wanaamini ilimsaidia Mkapa kupita. Baada ya kupigwa kwa kura, Nyerere alikataa kutaja kura za kila mtu na badala walitaja tu Msuya kushika nafasi ya tatu na hivyo kutolewa.

Ni kawaida kwa mwanadamu kwenda upande wa mshindi, kuna watu wanaamini laiti kura zote zingetajwa kama ilivyo kawaida, huenda watu wengi kutoka kambi ya Msuya wangemuunga mkono JK kwenye round ya mwisho.

Pia kulikuwa na kundi la Wazanzibar ambalo lilimwunga mkono Msuya na kuwa na makubaliano kwamba Omar Juma angelikuwa makamu wa rais. Baada ya Msuya kutolewa, kundi la Mkapa liliwafuata Wazanzibari na kuahidi kumteua Omar Juma kuwa makamu wa rais. Kundi zima la Zanzibar likahamia kwa Mkapa.

JK kutokufikisha asilimia 50 ilikuwepo kwenye katiba na bado ipo. Mwaka 2005 JK alipita 50% kwenye round ya kwanza hivyo hakukuwa na haja ya kubakiza wagombea wawili.



asante sana mkuu.umeniondolea dukuduku nililokuwa nalo kwa muda mrefu
 
Mtanzania,

..kambi ya JK na ile ya Msuya zilikuwa haziivi.

..JK alikuwa na malalamiko kwamba, Dr.Lawrence Gama, aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, alikuwa akipiga kampeni kwa ajili ya Msuya.

..kilifanyika kikao cha "usuluhishi" ambacho habari zake nakumbuka ziliandikwa na gazeti la Rai. sina hakika kikao hicho kiliongozwa na nani lakini nadhani Dr.Gama hakuwa na wakati mzuri.

..kuna wanaodai kwamba Mkapa alifaidika na ugomvi kati ya kambi ya JK na ile ya Msuya. ukiangalia mgawanyo wa kura za raundi ya kwanza na ya pili, utaona karibia kura zote alizopata Cleopa Msuya ktk raundi ya kwanza zilihamia kwa Mkapa ktk raundi ya pili alipobakia na JK.

..kwa upande mwingine hotuba za Mzee Mwinyi na Mwalimu Nyerere zilikuwa ni kama maelekezo kwamba kura ziende kwa JK na Mkapa na siyo Cleopa Msuya.

..Mwinyi aliwaasa wajumbe wampigie kura mgombea anayetajwa vizuri Watanzania wenzao walioko nje ya mkutano. sasa hiyo ilikuwa ni kama maelekezo kwamba wampigie kura JK ambaye alikuwa akiandikwa vizuri na magazeti.

..Mwalimu aliwaasa wajumbe wampigie kura mgombea ambaye wana uhakika atapiga vita rushwa, ukabila, na udini. hotuba ya Mwalimu ilikuwa kama maelekezo kwamba wajumbe wasimpigie kura Cleopa Msuya ambaye wakati wote amekuwa akituhumiwa kwa rushwa na ukabila. suala la udini sina uhakika kama lilikuwa ni dongo dhidi ya JK kwasababu wakati huo alikuwa hana tuhuma zozote zile za udini.
 
Hawa makatibu wakuu wawili wa CCM wamepata dhahma baada ya mchujo wa wagombea urais katika chama chao kwavile washindi wamekuwa wale ambao hawakuwa chaguo lao
Mangula nasikia nae alikuwa na mtu wake ndiyo maana alimuandikia ripoti mbovu Kikwete.Huyo mtu wake alikuwa nani?
 
Asante na vile nimepata mwanga juu ya hilo . Nilikuwa gizani juu ya hilo . honger a wana Jk.
 
Ni hatua hiyo hiyo imefuatwa mwaka 2005.. Waliochukua form na kuondolewa ktk hatua ya kwanza inaonyesha hawahesabiki ila wale waliobakia na kupigiwa kura.. Malecela aliondolewa mapema lakini waulize wenyewe watasema ati alipigwa chini ktk kura wakati Mkapa alimwengua kiroho mbaya kabla hata ya upigaji kura!
 
Mtanzania,

..kambi ya JK na ile ya Msuya zilikuwa haziivi.

..JK alikuwa na malalamiko kwamba, Dr.Lawrence Gama, aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, alikuwa akipiga kampeni kwa ajili ya Msuya.

..kilifanyika kikao cha "usuluhishi" ambacho habari zake nakumbuka ziliandikwa na gazeti la Rai. sina hakika kikao hicho kiliongozwa na nani lakini nadhani Dr.Gama hakuwa na wakati mzuri.

..kuna wanaodai kwamba Mkapa alifaidika na ugomvi kati ya kambi ya JK na ile ya Msuya. ukiangalia mgawanyo wa kura za raundi ya kwanza na ya pili, utaona karibia kura zote alizopata Cleopa Msuya ktk raundi ya kwanza zilihamia kwa Mkapa ktk raundi ya pili alipobakia na JK.

..kwa upande mwingine hotuba za Mzee Mwinyi na Mwalimu Nyerere zilikuwa ni kama maelekezo kwamba kura ziende kwa JK na Mkapa na siyo Cleopa Msuya.

..Mwinyi aliwaasa wajumbe wampigie kura mgombea anayetajwa vizuri Watanzania wenzao walioko nje ya mkutano. sasa hiyo ilikuwa ni kama maelekezo kwamba wampigie kura JK ambaye alikuwa akiandikwa vizuri na magazeti.

..Mwalimu aliwaasa wajumbe wampigie kura mgombea ambaye wana uhakika atapiga vita rushwa, ukabila, na udini. hotuba ya Mwalimu ilikuwa kama maelekezo kwamba wajumbe wasimpigie kura Cleopa Msuya ambaye wakati wote amekuwa akituhumiwa kwa rushwa na ukabila. suala la udini sina uhakika kama lilikuwa ni dongo dhidi ya JK kwasababu wakati huo alikuwa hana tuhuma zozote zile za udini.
Kabisa
 
Ni hatua hiyo hiyo imefuatwa mwaka 2005.. Waliochukua form na kuondolewa ktk hatua ya kwanza inaonyesha hawahesabiki ila wale waliobakia na kupigiwa kura.. Malecela aliondolewa mapema lakini waulize wenyewe watasema ati alipigwa chini ktk kura wakati Mkapa alimwengua kiroho mbaya kabla hata ya upigaji kura!
Mmeona kwamba Mkapa ana mkono wake
 
Wagombea walikuwa 17 kwenye Uchaguzi wa 1995
Kwenye Tano bora waliingia

Msuya, Jakaya, Mkapa, Msekwa Na Warioba

Mzee Malecela alishinikizwa kujitoa Na Hayati Baba wa Taifa Kwa Kuwa Malecela hakuonekana Kama ni Muumini Mzuri wa Serikal mbili Na Azimio la Arusha Ila ndie aliekuwa ana nguvu zaid Kuliko wote

Katika Tano bora Mkapa ndie aliekuwa Mgombea ambae hana umaarufu kabisa akiwa Ni Waziri wa Sayansi, Teknolojia Na Elimu ya Juu, alizidiwa umaarufu Na beki namba wa tatu wa Yanga Keneth Kaunda Mkapa!
 
Back
Top Bottom