Mch. Mtikilila Chutama Nguo Imeshakuvuka

Songambele

JF-Expert Member
Nov 20, 2007
4,696
2,553
Ni muda mrefu Mtikila amelalamikiwa na wanasiasa wenzie wa upinzani kwa kuwazunguka na kutoa misimamo yenye utata, yaliyomtokea juzi baada ya kulipuliwa na RA imetoa picha kamili kwamba jamaa na yeye ni fisadi aliye jificha kwa kisingizio cha upinzani na uchungaji.

Haiwezekani upinge ufisadi halafu unufaike na ufisadi, hoja kusema kwamba alikopa na msaada ni dhaifu sana kwani zipo taasisi zinazokopesha na kwanini asiende huko kukopa, na mbona hakuwahi kusema kwamba wanaoshutumiwa mafisadi ni rafiki zake na anapata pesa kutoka kwao.

Mtikila ametuyeyusha kwa muda mrefu na kujifanya mtata katika kupigania maslahi ya nchi hii, kumbe ni mnafiki mkubwa, anatakiwa atuombe radhi watanzania badala ya kwenda mahakamani kupoteza muda wakati pesa amepokea na pia ahorozeshe ni wapi tena amekuwa akipata pesa na amepata jumla ya kiasi gani kutoka kwa hao rafiki zake anowaita mashetani na mafisadi kutuzuga. Kama atataka kuendelea na mapambano dhidi ya ufisadi arudishe pesa zote alizopokea kutoka kwa mafisadi.

Mtikila anatakiwa kutambua kwamba watanzania wanaelewa na wanaouwezo wa kupima na kuchukua hatua bila ya kwenda mahakamani, badala ya kujifanya hamnazo amrejee mungu wake na kuomba msamaha kuliko kuendelea kukimbia wakati nguo zimeshadondoka na aibu itampata zaidi kama ataendelea kukimbia.

Siasa za kibongo zinaonekana sio kabisa, jamaa amewaita sana magabachori kumbe anazunguka kwenda kuvuta mapene kimtindo! Jamaa tuendelee kuwakimbiza hivi hivi watatajana tuu!
 
inawezekana na wewe upo kwenye payrall ya Rostam kwani lugha unayoitumia haiashirii kufikisha ujumbe wa kile alichokifanya mtikila bali kumvua nguo ili aonekane hana heshma kwa jamii.
 
Sioni alichofanya cha maana zaidi ya kuvuta mshiko kutoka kwa fisadi, na simple logic ni kama unavuta mshiko kwa fisadi na wewe ni fisadi. Isipokuwa ni kufanya jamii ikuone mwema wakati unavuta mshiko wa mafisadi ndio sio poa, kama unafiki ni heshima kwa jamii sikubaliani na nziku.
 
Leo Kipanya anasema hivi, if I may quote,
Mtikila amesema ".....RA kanikopesha milioni 3 tu....nitazirudisha"!!!
 
inawezekana na wewe upo kwenye payrall ya Rostam kwani lugha unayoitumia haiashirii kufikisha ujumbe wa kile alichokifanya mtikila bali kumvua nguo ili aonekane hana heshma kwa jamii.

Ba nkwe, mbona mtikila keshajivua nguo mwenyewe??????
 
uyu jamaa anatuchanganya sana. sisi wengine hapa hatutaki hata kuiona sura ya rostam azizi, lakini tukija kwa mtikila, nashindwa kumdefine, ilikuwaje akaanza kumkopa Rostam pesa tena hela ndogo kama hiyo, alikuwa anajibembeleza nini?walikuwa kwenye mazingira gani? kulikuwa na kitu gani kilichokuwa kinaendelea hapo? au walikuwa marafiki toka mda mrefu? najiuliza maswali mengi sana aisee. au mtikila aliona kuwa Rostam yuko kwenye ufa na kwasababu yeye ndo mpiga mabom, akaamua to take advantage of that loop hole, kwamba, nikimuomba hela lazima atanipa tu kwasababu ataogopa kuwa nisipompa mtikila hela, atanipiga mabom yake? au mtikila ndo inakuwaga zake to take advantage of the suspects?...mhhhh! mi sijui. kama yupo humu ndani, tafadhali mtikila tueleze vizuri, manake wewe ulimkopa hela rostam, kwani rostam anamiliki benk ambapo mlikutania? yaani ulimfuata ofisini kwake ukamkope hela wakati unajua kuwa yeye ni fisadi? hauoni hata aibu mtikila? jamani tumueleweje sasa huyu jamaa?

pamoja ya yote, nakupongeza kwa kuzila hela ambazo ni za kwetu. hata kama hautarudisha, si kosa kwasababu hizo zimejilipa zenyewe, ni zetu na wewe chukua chako hicho toka kwa Rostam. hahahaha.
 
Mtikira...Ndio aina ya wanasiasa wetu???Njaa mlima!! Duh amechemka sio pole pole!!! ama kweli ufisadi umeshika kasi kwa style mbali mbali..
 
Njaa haina mwenyewe.....mtikila kinacho mmaliza ni ujinga wake mwenyewe toka ameanza siasa sijaona la maana ziadi ya (kanakwamba)tu..neno alipendalo.

Aziz kaona watu wanamwandama inagawa justice haija confirm kuwa ni guilty.Harafu mtu anaye mtuhumu kwa maneno makali ndio anakwenda kuomba pesa...kwa kweli utu uzima kazi...jamaa ka kaa nalo mpaka kaona bora asema apunguze uzito wake....

Blv me kama rostam ataendelea kuongea .... bila kuzuiwa...utasikia hata serikari ilikopa kwake...tupo hapa...vinginevyo wamefumbe mdomo kabisa.
 
Mtikila alitakiwa kukaa kimya au kukana kuwa hakuchukua ili walao aonekane kasingiziwa na RA. Maadamu kakubali kuwa kachukua, katia aibu, tena kubwa sana. Mtu mzima akubali ukweli kwa kachemsha
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom