Umeme hauwezi kupatikana kwa kubadilisha mawaziri bila kuwekeza kwenye miundo mbinu ya kisasa ya kuzalisha, kusafirisha na kusambaza umeme. Hapa kwetu tumekuwa hatufanyi uwekezaji wowote wa maana kwenye sekta ya umeme tunabaki kudanganyana kuwa mgawo utakuwa historia! Mgawo hauwezi kuisha kwa mbinu za dharula zenye sura ya Richmond and Dowans na ni uendawazimu kudhani kuwa hizi mbinu ni endelevu. Yawezekana kabisa huku ndio kudumaa akili anakoongelea huyu mchungaji.tumemuondoa ngereja wamemleta ngereja umeme bado wa mgao, tumemuondoa waziri maige na kuja kagasheki ni yale yale.