kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 266
Kwa heshima na taadhima naomba uweke hii habari hapa kwani sitaki tukio kama hili lijitokeze kwa mtu mwingine, naomba sana naomba sana, Juzi jumamosi tarehe 4/12/2010 tulikuwa na harusi ya mshikaji ilifanyika pale Msasani Club. Ilikuwa ni harusi nzuri imeandaliwa kwa mda mrefu. Lilitokea tukio la ajabu sana kwani MC wa Shughuli hiyo ambaye anaitwa MC ( Jina kapuni) hakuonekana (aliingia mitini). Cha ajabu zaidi akawa hapokei simu na ukimpigia simu anaandika msg (kwa namba xxxx) na (xxxxx) kwamba amepata dharura ameenda Arusha kitu ambacho tunaamini si kweli alikuwa yupo kwenye shughuli nyingine. MC huyo tayari alikuwa ameshalipwa kiasi cha 350,000. Wananchi nimelileta hili kwenu hasa kwa wale waliopo Dar/TZ ili mjihadhari na utapeli wa aina hii. Kwa kweli sherehe nzima iliharibika japo ilibidi tutafute MC wa haraka haraka na sherehe kuanza saa mbili na nusu.