Mbwana Samatta cheza mpira sasa

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,418
108,518
Ningependa kuchukua FURSA hii murua kumshauri Mtanzania pekee aliyetutoa KIMASOMASO katika mchezo wa mpira wa miguu Mbwana Ally Samatta a.k.a POPA kuwa kwakuwa tayari tumeshajua kuwa yupo MAJUU na mambo yake ni safi kimtindo basi apunguze sasa kupiga piga MIPICHA na kuituma kwa Wana Blog na Washikaji zake kila mara huku zingine zikiwa hata hazina maana. Kwa mfano kuna moja amejipiga yupo juu GHOROFANI nadhani katika APARTMENT yake anapiga mswaki huku nyingine akiwa anavaa KANDAMBILI. Halafu kwa MSHANGAO mkubwa Miandishi yetu ya Habari za Kibongo na Bloggers nao wanatuwekea picha hizo hizo tuziangalie. Tunafaidika na nini sasa hapa?

Ningependa nichukue muda huu adhimu nimuonye Mbwana Ally Samatta kuwa hapo alipo asidhani ndiyo kamaliza tena kwa tunaojua soka la kulipwa hasa la ULAYA sasa Mbwana Samatta ndiyo anatakiwa akazane sana KIMAZOEZI huku akizingatia MAADILI yote muhimu ya Mchezaji wa Kulipwa ili aweze kuonekana zaidi na Klabu zingine Kubwa ILA akiwaendekeza Watanzania ambao wengi wao leo wanajifanya WANAMJUA namuhakikishia ATAPOROMOKA sasa hivi. Tulimuonya Mcheza Kikapu Mtanzania Hasheem Thabit hivi hivi kuwa awe makini na Kazi yake hakutusikia na matokeo yake VIDEMU DEMU vya kibongo bongo VIKAJIPENDEKEZA kwake na kumuharibu kabisa hadi akakosa nafasi na kupelekwa timu nyingine kwa MKOPO na sasa anahangaika kurudi katika KIWANGO lakini bado.

Mbwana Ally Samatta napenda nikutaarifu kuwa Watanzania SISI SISI ambao sasa tunajifanya tupo karibu nawe ndiyo SISI SISI ambao ukishindwa huko tutakuwa wa kwanza kukupiga MADONGO na KUKUZUSHIA mengine hadi ambayo HUKUYAFANYA. Sipendi nikufanye labda USIJICHANGANYE nao katika MITANDAO YA KIJAMII la hasha bali NAKUHUSIA tu kuwa acha KUTUMIA MUDA WAKO MWINGI MITANDAONI huku UKITURUSHIA au KUTUTUMIA PICHA zako bali poteza muda wako mwingi KUJIFUNZA SOKA LA KULIPWA LA ULAYA LIPOJE, CHANGAMOTO ZAKE ZIPOJE, PAMBANA na UWE NA MALENGO MAKUBWA zaidi.

Ushauri wangu una hiari ya KUUCHUKUA na KUUPIMA au KUUPUUZA ila kuna siku UTANIKUMBUKA na KUUKUMBUKA. Nakutakia maisha na mafanikio mema hapo Ubelgiji na FAHAMU kwamba Watanzania wote TUNAKUTEGEMEA Wewe uwe NURU ya kuwaangazia wenzako akina Mkude, Telela, Busungu na Ajib na WAANDISHI WA HABARI ZA MICHEZO hebu muacheni basi Kijana ajipange kwanza na msaidieni KIUSHAURI.
 
To each his own. Usichagulie watu maisha. Anaweza kuwa muuza sura mitandaoni na Bado akaperform cha msingi wewe msapoti tu mtanzania mwenzio.
 
To each his own. Usichagulie watu maisha. Anaweza kuwa muuza sura mitandaoni na Bado akaperform cha msingi wewe msapoti tu mtanzania mwenzio.

Asante kwa kuchangia japo nikiri kuwa katika UFUATILIAJI wangu wa masuala ya Soka NDANI na NJE ya Tanzania sijawahi kuona Mchezaji NYOTA wa KIZAZI hiki Lionel Messi " La Pruga " akifanya hayo ambayo Samatta anayafanya sasa wakati KIUHALISIA yeye ndiyo alitakiwa AFANYE hivyo ila anajua nini maana ya NIDHAMU YA SOKA. Watu wa DIZAINI yako ndiyo MLIMPONZA Mcheza Kikapu Hasheem Thabit na sasa MNAMCHEKA anavyofulia zake tu huko mamtoni. Watanzania ni WAFAFIKI TULIOKITHIRI!
 
Asante kwa kuchangia japo nikiri kuwa katika UFUATILIAJI wangu wa masuala ya Soka NDANI na NJE ya Tanzania sijawahi kuona Mchezaji NYOTA wa KIZAZI hiki Lionel Messi " La Pruga " akifanya hayo ambayo Samatta anayafanya sasa wakati KIUHALISIA yeye ndiyo alitakiwa AFANYE hivyo ila anajua nini maana ya NIDHAMU YA SOKA. Watu wa DIZAINI yako ndiyo MLIMPONZA Mcheza Kikapu Hasheem Thabit na sasa MNAMCHEKA anavyofulia zake tu huko mamtoni. Watanzania ni WAFAFIKI TULIOKITHIRI!
Cristiano Ronaldo anaweka picha kila muda na kufanya mambo mbalimbali nje ya soka na bado anapafomu. Karim Benzema vivyo hivyo. Wachezaji kikapu na football wa US ndio usiseme na Bado wanafanya vizuri. Interests za watu ni tofauti mkuu hivyo acha waishi vile wapendavyo.

On the contrary, Thabeet hakuwa muuza sura mitandaoni kama wengine wengi ila hakuwa akijituma mazoezini na ndicho kilichopelekea kushuka kwake. Ukifanya nafasi yako na kupata nafasi ya kuconnect na fans wako utakuwa sawa tu
 
Si afanye kilichompeleka hukoo jamanii kama picha sukuiz hata Mtoto wa mwezi mmoja anajipiga selfiee
Hakuna jipya kila MTU anajua ykoo majuu cha ziada kipii........??
Tunakoelekea atapipa nyingine ANATITA Eti tuone vyoo vya Ulaya
 
ila namuunga mkono mleta mada hapa, samata anatakiwa kuzingatia kilichompeleka kule la sivyo achelewi kuwa hashim thabit wa pili, au anazani pale ni TP MAZEMBE?
 
Mwacheni aishi atakavyo yeye!

UZI wangu huu UNANIONYESHA vizuri sana watu ambao KICHWANI ZIPO na ambao HAMNAZO. Kwa mfano tu post yako imenionyesha kuwa dhahiri wewe ni Mr. HAMNAZO katika Bichwa lako. Kama ingekuwa ni hivyo basi hata hawa MARAIS wote duniani wasingekuwa na WASHAURI bali wangejifanyia tu wenyewe mambo yao! Hivi kule Vyuoni mlikuwa mnaenda kufanya nini kama hamjui hata kujenga HOJA yenye MASHIKO tena nyepesi tu kama hii?
 
Agreed !
Tena asali sana pia maana huu umri anaosema anao ukipiga hesabu alipokuwa Lyoni na Simba data zinagongana !!
 
Namuombea sand huyu shujaa wetu. Mashaka yangu yako kwenye safari aliyoifanya lumumba, sijui kama itapelekea kwenye baraka!
 
Asante kwa kuchangia japo nikiri kuwa katika UFUATILIAJI wangu wa masuala ya Soka NDANI na NJE ya Tanzania sijawahi kuona Mchezaji NYOTA wa KIZAZI hiki Lionel Messi " La Pruga " akifanya hayo ambayo Samatta anayafanya sasa wakati KIUHALISIA yeye ndiyo alitakiwa AFANYE hivyo ila anajua nini maana ya NIDHAMU YA SOKA. Watu wa DIZAINI yako ndiyo MLIMPONZA Mcheza Kikapu Hasheem Thabit na sasa MNAMCHEKA anavyofulia zake tu huko mamtoni. Watanzania ni WAFAFIKI TULIOKITHIRI!

Mbona ozil huwa anapiga picha miguu yake ikiwa na soksi huku anacheza game ya mpira geto kwake af anakula malike millioni, makoment laki9, mbona fresh tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom