Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,000
- 9,862
Rwanda na Ujerumani wamesaini makubaliano ya ushirikiano katika mradi wa kutumia mbwa kuwatambua walioambukia virusi vya Corona.
Makubaliano hayo yamesainiwa kati ya Balozi wa Rwanda nchini Ujerumani Dkt. Thomas Kurz na Mkuu wa kituo cha kitaifa cha utambuzi wa utambulisha wa watu (RBC) Dkt Nzanimana Sabin.
Mradi huo uliopewa jina la ‘’ utambuaji wa harufu’’ (scent Identification) utawahusisha mbwa waliopewa mafunzo maalum ya utambuzi wa watu wenye maambukizi ya Covid -19 na hivyo kuharakisha juhudi za kuzuwia usambaaji zaidi wa virusi vya corona.