Mbwa aliyetelekezwa baada ya mmiliki kufariki

Hayanihusu lakini fasihi iliyotumika hapa ni ndogo sana......raha ya fasihi ifikirishe, sio sentensi ya kwanza tu tayari unakiona anachohangaika nacho mwandishi.
 
Tena ashukuru angekuwa huku kilolo tungemtengeza supu huyo mbwa.
Kala kuku wetu na vifaranga wengi tu
 
Nimejifunza kwamba mwenye mbwa alikuwa na wazimu kwa kufuga mbwa koko aliyechukiwa hata na wanafamilia sembuse wapita njia!!?.
 
Ukiona hivyo jua mbwa alikuwa anautii kwa mwenye mbwa tu, aling'ata hata wanafamilia au mbwa alikuwa kichaa, lakini mwenye mbwa peke yake alikuwa akimwona huyo mbwa ni mzima.
 
nimejifunza mbwa alikuwa mbwa koko,angekuwa mbwa mwenye discipline angependwa na kukubalika hata baada ya bwana wake kufariki
 
Tatizo la mbwa ni vile alijipa mamlaka hata ya kung'ata wapita njia.

Tena akawa anaenda mpaka nyumba za jirani kusumbua watu kwa vile tu tajiri yake anamlinda.

Sasa mbwa anakula jeuri yake.
 
Mbwa alifundishwa ujambazi, means mwenye nyumba nae alikuwa jambazi
 
TUJIFUNZE KIDOGO HAPA KUHUSU HUYU MBWA
(Jeremiah kipoya)
Mwenye nyumba aliamua kufuga mbwa ili amsaidie kulinda mali zake nyumbani hasa nyakati za usiku
Akamfundisha yule mbwa kulinda nyumba na mbwa akawa mkali kweli yani ana bweka hata ukisogelea tu uzio wa nyumba anayolinda
Mwenye nyumba akampenda sana yule mbwa kwakua alikuwa anafanya kazi aliyo mfundisha pia wana familia wa nyumba hiyo walifurahi pia kwa utendaji wa yule mbwa
Majirani na wezi walimchukia sana yule mbwa kwakua kubweka kwake wao waliona ni kelele usiku anawasumbua wezi nao wakaona anawakosesha fursa ya kuiba mali za mwenye nyumba
Siku moja mwenye nyumba alifariki na hapo mambo yakaanza kuwa magumu kwa yule mbwa, Majirani na wezi walisema atakoma aliyemfuga na kumpa chakula kashaondoka sasa ngoja tumnyooshe huyu mbwa.Mbaya zaidi hata wanafamilia wa hiyo nyumba anayoilinda nao wakaanza kumuona huyo mbwa ni kero anawapigia kelele usiku na amezidi ukali na ukorofi
Wanafamilia wakajadili wamfanye nini huyo mbwa? Wamtupe mitaani? Wamuue? Wakaona hapana ni bora wamng'oe meno na kucha kwakua hata kuwa tena na nguvu ya kung'ata, atakuwa mnyonge na mwenye msongo wa mawazo yani hata kuwa na maana tena na hata piga kelele za kubweka
majirani na wezi wakafurahi sana kwakuwa kazi ya kumkomesha huyo mbwa imefanywa na wanafamilia wenyewe
Je nani wa kumtetea mbwa? Watu wote wamemgeukia?Amepewa hukumu nzito kwa kufanya kazi aliyo fundisha na aliye mnunua na kumfuga je tumlaumu marehemu mwenye nyumba?
UMEJIFUNZA NINI KWENYE HIKI KISA??
Jeremiah Kipoya
Nimejifunza kuwa sabaya ni jambazi tu ila kuna mandezi wanamtetea. Acha mahakama ifanye kazi yake.
 
Kumtetea mbwa aliyekuwa anaumiza maisha ya watu haina maana.Naona waliokuwa wanafuga mbwa wanahangaika sana na walisahau maisha ya watu waliokuwa wanaumizwa na watu
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom