Mbunifu wa majiko sanifu yanayotumia kuni na mkaa anahitajika

kajansi

JF-Expert Member
Sep 19, 2012
485
221
Salaam wana JF,
Kwa kuzingatia kuwa jukwaa hili ni moja ya majukwaa ambayo kila kitu kinawezekana, ombi langu nahitaji mtu yoyote ambaye anaweza kubuni energy cooking stove na hasa stove(jiko) linalotumia kuni lenye uwezo wa kuserve hadi asilimia 50 ya kuni na mkaa kwa wakati mmoja. Technolojia inayotakiwa inatakiwa iwe ni rahisi sana ambayo mwananchi wa kawaida anaweza kuhimudu katika mazingira yake bila kwenda kuitafuta sehemu yoyoye. Mradi wetu utalenga kuwafundisha wananchi wenyewe kuzalisha majiko yao wenyewe baada ya kupata mafunzo ya wewe mbunifu ili mpango uweze kuwa endelevu. Mradi unakusudiwa kufanyika katika jamii za wavuvi waliopo katika ziwa victoria ambao wameunganishwa katika mradi wa uvuvi bora ( Eco-Label fishers).
Madhumuni ya mradi huu ni kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa kwa hadi asilimia 50 na hii itaweza kusaidia kulinda mazingira na kipato cha wavuvi kwani kwa sasa wanatumia gharama kubwa sana kununua kuni na mkaa.
Yeyote mwenye kutaka kushiriki anaweza kuwasiliana na mimi ili mambo mengine yajadiliwe mojakwamoja.
Tuwasiliane naturlandlake@gmail.com
 
yap naamini JF ni kila kitu...ngoja na mie niake chonjo hapa naweza kupata moja mbili...

Kweli kaka nimeshaanza mazungumzo na wadau kupia mail bado nawakaribisha ili tuweze kufanikiwa zaidi!
 
Back
Top Bottom