Mbunge: Watumishi wameifikisha Tanzania Uchumi wa Kati, tunasubiri nini kuwaongeza mishahara? Asema imeshusha utendaji

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,444
7,808
Mbunge wa viti maalum Wafanyakazi, Janejelly James Ntate amesema watumishi wameweza kuifikisha Tanzania Uchumi wa Kati kabla ya wakati wake mwaka 2025.

Akiwa kwenye vikao vya bajeti vinavyoendelea mjini Dodoma amesema watumishi walifanya hayo kwasababu serikali kupitia vyama vya watumishi iliwaomba watumishi waivumilie miaka mitano wajenge uchumi na baada ya hapo wataenda na maslahi ya wafanyakazi.

Ntate amesema ilani ya CCM ukurusa wa 180/1 inaongelea maslahi ya watumishi lakini waziri Jenster Mhagama alipowasilisha bajeti ya waziri mkuu hajaona nyongeza ya mishahara na TAMISEMI haijasema kama kutakuwa na nyongeza ya mishahara.

"Tunasema matatizo lakini hatuangalii chanzo cha tatizo, yawezekana hata kushuka kwa utendaji ni watumishi wamefika mahali wamekufa ganzi, tujiulize kwa miaka mitano ni watumishi wangapi wamestaafu kwa mshahara wa zamani na kikokotoo hufanyika kwenye mshahara" Alisema mbunge.

"Tumeshajenga uchumi umefika uchumi wa kati tena kabla ya muda wake na mambo ya kufanyia watumishi kwenye ilani yako 16. Kama wizara ya fedha ikija haina nyongeza ya mishahara, wabunge mnisapoti tukamate shilingi, watumishi wanaumia" Alipiga mkwara mbunge Janejelly.


 
Ndiyo maana nilimchukia sana magufuli na serikai yake ya ccm. Yaani mwaka huu wa 2021, ilikuwa nipande daraja kwa mara ya pili!

Lakini mpaka sasa, hata ile mara moja tu sijapanda! na hata haijulikani kama watanipandisha mwaka huu, au wataendelea na stori zao za kudemka.
 
Nitashangaa sana wakipotezea na mwaka huu. Kipimo changu kwa mama Samia ni May 1.
 
Huyo mbunge naye hajielewi, Nani aliyemwambia juhudi za kulifikisha Taifa hili ktk Uchumi wa Kati, wamehusika wafanya kazi pekee??

Je wakulima, wataongezwa na nani mishahara? Wamachinga na wachimbaji nao?

Wavuvi na wafigaji Nani atawaongeza mishahara??

Wafanya biashara nao, hao wote wamehusika kuipaisha nchi na kuifikisha katika Uchumi wa Kati

Swala la kuongezwa mishahara ni la kisheria, halihusiani na hoja ya mbunge, hiyo hoja Kwa nchi zenye watu vichwa, linazua utata!!
 
Ndiyo maana nilimchukia sana magufuli na serikai yake ya ccm. Yaani mwaka huu wa 2021, ilikuwa nipande daraja kwa mara ya pili!

Lakini mpaka sasa, hata ile mara moja tu sijapanda! na hata haijulikani kama watanipandisha mwaka huu, au wataendelea na stori zao za kudemka.
Andika maumivu tu mkuu, CCM ni shetani kabisa
 
Enzi za dikteta asiongea hivi akabaki salama
Mimi mwenyewe nashangaa kuona Wabunge wa ccm wakiwa mstari wa mbele kutetea stahiki za wafanyakazi baada tu ya magufuli kufariki!

Miaka yote walikuwa wameufyata, na kutuacha wachache kupaza sauti zetu humu jukwaani! Unafiki tu ndiyo umewajaa.
 
Huyo Mbunge kuna kitu hakipo sawa... unaposema Wafanyakazi waliambiwa wavumilie uchumi upande bila nyongeza yeyoye katika mishahara basi ajue punjo lao ndio limeongeza hali ya uchumi so wafanyakazi wakiongezwa mshahara basi uchumi utateremka pwaaa chini... naona zigo la lawama anaangushiwa Mama SASHA
 
Ndiyo maana nilimchukia sana magufuli na serikai yake ya ccm. Yaani mwaka huu wa 2021, ilikuwa nipande daraja kwa mara ya pili!

Lakini mpaka sasa, hata ile mara moja tu sijapanda! na hata haijulikani kama watanipandisha mwaka huu, au wataendelea na stori zao za kudemka.
Eti kudemka ....umenichekesha kaka mkuu.
 
Back
Top Bottom