Mbunge wangu wa Kibamba, changamkia fursa ya mheshimiwa Rais haraka iwezekanavyo kabla ya bajeti

Kwasenga

Member
Feb 24, 2021
50
52
Leo Mh. Rais wakati akizindua stand ya mabasi ya mbezi luis amepokea maombi murua kutoka kwa mwakilishi wa wananchi ambaye ni mbunge, nitapenda kuongelea ombi moja kati ya mengi aliyoyaomba kwa maana yote yamepata majibu safi sana.

Ombi lenyewe ni barabara za jimbo la Kibamba. Nakupongeza sana mh mbunge kwa kuomba kupatiwa japo barabara kidogo za lami. Ukikumbuka majibu ya Mh Rais ni kwamba umepewe majukumu ya kuungana na team ya TANROAD ili kuandaa barabara ambazo wananchi wako wanaomba ziwekwe katika kiwango cha lami.

Mimi kwenye hili nakukumbusha kujitahidi kwa hali na mali kuhakikisha unaendelea kufuatilia TANROAD ili wasije fanya yale ambayo hukuomba kwa mh rais. Barabara za kibamba unazijua vizuri sana, mfano barabara ya kutoka mbezi mwisho, msakuzi mpaka mpigi magoe kupitia makabe, mbezi mwisho kupitia Mbezi High School mpaka Mpigi Magoe, Kibamba Shule mpaka Mpigi Magoe, Mpigi Magoe mpaka Bunju n.k.

Hizi zote ni barabara za TANROAD na kwa ukubwa wake na umuhimu wake nitashangaa kama zote hizi tatu zitakosa kwenye huu ujenzi kwa maana ni kiungo muhimu sana na ziko busy sana na pia ukizingatia kwa mfano, hii inayotoka mbezi mwisho kupitia mbezi high-machimbo mpaka mpigi magoe, ni barabara yenye daladala kubwa ambazo hupotea kipindi cha mvua na kusababisha usumbufu mkubwa kwa wananchi.

Kwa ushauri wangu, hizi ndo barabara kiungo ambazo mm naona ndo zinatakiwa ziwe za kwanza kuwa presented kwa mheshimiwa rais ili ziweze kuingia kwenye bajeti ya 2021/2022. (Kwa maana pia ziko chini ya TANROAD).

Nawasilisha
 
Mbezi Mwisho Hadi Msumi Mwisho nayo ni muhimu Sana na Ina daladala nyingi na watu wengi pia, inaenda kuungana na Madale kuelekea Tegeta Hadi Bagamoyo. Tukumbukwe Jamani.
 
Mbezi Mwisho Hadi Msumi Mwisho nayo Ni muhimu Sana na Ina daladala nyingi na watu wengi pia, inaenda kuungana na Madale kuelekea Tegeta Hadi Bagamoyo. Tukumbukwe Jamani.
Huwa najiuliza magari ya kwenda Pwani, Tanga, Kilimanjaro Arusha, Manyara ambayo hupita Bagamoyo Road yatapita wapi maana njia pekee kiungo ambayo lami ni ya Goba, kwa kutokea stendi mpya.
 
Mbunge wetu wa Kibamba, ulipewa fursa na Mh Rais, mbona hutushirikishi wapiga kura wako? Tupe mrejesho basi wa barabara ulizompelekea rais wetu?
 
Huwa najiuliza magari ya kwenda Pwani, Tanga, Kilimanjaro Arusha, Manyara ambayo hupita Bagamoyo Road yatapita wapi maana njia pekee kiungo ambayo lami ni ya Goba, kwa kutokea stendi mpya.
Barabara ya Mbezi mwisho hadi msumi hadi tegeta ndio suluhisho la swali lako . Bonge la short-cut
 
Itapaswa kutumiwa ya Mbezi High -Mpiji- Bunju-...
Huwa najiuliza magari ya kwenda Pwani, Tanga, Kilimanjaro Arusha, Manyara ambayo hupita Bagamoyo Road yatapita wapi maana njia pekee kiungo ambayo lami ni ya Goba, kwa kutokea stendi mpya.
 
Itapaswa kutumiwa ya Mbezi High -Mpiji- Bunju-...
Na hii ni barabara muhimu sana tena sana ukizingatia ndio sebule ya stand. Round about imewekwa pale Mbezi high, halafu ukimaliza tu round about unaanza vumbi. Itakuwa aibu kweli kweli. Lakini pia uwepesi wake wa kufika Bunju kwa mabasi kwa maana inapasua moja kwa moja bila kona kona. Na kigezo kingine ni kuwa, hii ni barabara ya Tanroads ambayo inatumia gharama nyingi kuchongwa kila mara kutokana na kupitiwa magari mengi sana, hivyo kupunguza hizo gharama za reja reja ni bora kuweka lami. Na pia, hakuna gharama za fidia kwa maana watu wamejenga kwa kufuata alama za mwisho wa barabara.
 
Barabara ya Mbezi mwisho hadi msumi hadi tegeta ndio suluhisho la swali lako . Bonge la short-cut
Ukiingiza mabasi tegeta unayapeleka tena kwenye kifoleni wakati una option ya kuyatoa moja kwa moja bunju. Nadhani barabara inayoenda moja kwa moja bunju ni muhimu sana zaidi ya hiyo ya kuanza kupitia tegeta.
 
Kwa vajeti ya 2021/22 ameshachelewa imeshaandaliwa bado kupitishwa tu na Bunge. Labda mjaribu ya mwaka 2022/23. Ingawa Mh. Rais anaweza kuwezesha hayo yote.

Nimeona hapo juu kuna mtu anambeza Mh. Mbunge Mtemvu. Naomba nikwambie tuweke siasa pembeni Mh. Mtemvu ni mbunge bora kati ya wabunge wote wa DSM utakuwa kunielewa baadae. Hata ili la kufikisha jambo kwa Mkuu ni juhudi zake. Mnachotakiwa wananchi sio kumwacha peke yake. Inabidi mtengeneze mikakati ya pamoja ya kuliendeleza Jimbo la Kibamba kisha mnamweka Mbunge wenu kama kinara wa kuyapeleka mbele. Mkikaa tu na kuleta masiasa yenu ya sijui mbunge wa kuchuchumaa mtayasikia maendeleo kwenye majimbo ya wenzenu. Mapambano ya kuleta maendeleo yanaanza na nyie na mkipata Mbunge makini inakuwa easy kutoboa. Wenzetu wa wilaya ya Temeke huko Mbagara, Tandika, Buza, Mtoni wana lami mpk milangoni mwa nyumba zao wakati jimbo la Kibamba na Ubungo lami ziko barabara kuu tu

Tujifunze kufanya kazi na wabunge, tuunde kamati za maendeleo maaalum kwa jimbo, tuweke mikakati kama jimbo ili kulifanya lifike mbali tuachane na business as usual, thamani ya eneo ni miundo mbinu

SICHANGIAGI SIASA NA SI MWANASIASA ILA NAPENDA WATU TUBADILIKE NA TUTUMIE FURSA KAMA HIZI ALIZOSEMA MH. RAIS KWA WELEDI ILI TUSIZIPOTEZE
 
Ukiingiza mabasi tegeta unayapeleka tena kwenye kifoleni wakati una option ya kuyatoa moja kwa moja bunju. Nadhani barabara inayoenda moja kwa moja bunju ni muhimu sana zaidi ya hiyo ya kuanza kupitia tegeta.
Ambayo ni ipi ?
 
Kwa vajeti ya 2021/22 ameshachelewa imeshaandaliwa bado kupitishwa tu na Bunge. Labda mjaribu ya mwaka 2022/23. Ingawa Mh. Rais anaweza kuwezesha hayo yote.

Nimeona hapo juu kuna mtu anambeza Mh. Mbunge Mtemvu. Naomba nikwambie tuweke siasa pembeni Mh. Mtemvu ni mbunge bora kati ya wabunge wote wa DSM utakuwa kunielewa baadae. Hata ili la kufikisha jambo kwa Mkuu ni juhudi zake. Mnachotakiwa wananchi sio kumwacha peke yake. Inabidi mtengeneze mikakati ya pamoja ya kuliendeleza Jimbo la Kibamba kisha mnamweka Mbunge wenu kama kinara wa kuyapeleka mbele. Mkikaa tu na kuleta masiasa yenu ya sijui mbunge wa kuchuchumaa mtayasikia maendeleo kwenye majimbo ya wenzenu. Mapambano ya kuleta maendeleo yanaanza na nyie na mkipata Mbunge makini inakuwa easy kutoboa. Wenzetu wa wilaya ya Temeke huko Mbagara, Tandika, Buza, Mtoni wana lami mpk milangoni mwa nyumba zao wakati jimbo la Kibamba na Ubungo lami ziko barabara kuu tu

Tujifunze kufanya kazi na wabunge, tuunde kamati za maendeleo maaalum kwa jimbo, tuweke mikakati kama jimbo ili kulifanya lifike mbali tuachane na business as usual, thamani ya eneo ni miundo mbinu

SICHANGIAGI SIASA NA SI MWANASIASA ILA NAPENDA WATU TUBADILIKE NA TUTUMIE FURSA KAMA HIZI ALIZOSEMA MH. RAIS KWA WELEDI ILI TUSIZIPOTEZE
Hili la kuhamashisha maendeleo na kuja na mkakati maalum yeye ana nafasi nzuri ya kulifanikisha
 
Kwa vajeti ya 2021/22 ameshachelewa imeshaandaliwa bado kupitishwa tu na Bunge. Labda mjaribu ya mwaka 2022/23. Ingawa Mh. Rais anaweza kuwezesha hayo yote.

Nimeona hapo juu kuna mtu anambeza Mh. Mbunge Mtemvu. Naomba nikwambie tuweke siasa pembeni Mh. Mtemvu ni mbunge bora kati ya wabunge wote wa DSM utakuwa kunielewa baadae. Hata ili la kufikisha jambo kwa Mkuu ni juhudi zake. Mnachotakiwa wananchi sio kumwacha peke yake. Inabidi mtengeneze mikakati ya pamoja ya kuliendeleza Jimbo la Kibamba kisha mnamweka Mbunge wenu kama kinara wa kuyapeleka mbele. Mkikaa tu na kuleta masiasa yenu ya sijui mbunge wa kuchuchumaa mtayasikia maendeleo kwenye majimbo ya wenzenu. Mapambano ya kuleta maendeleo yanaanza na nyie na mkipata Mbunge makini inakuwa easy kutoboa. Wenzetu wa wilaya ya Temeke huko Mbagara, Tandika, Buza, Mtoni wana lami mpk milangoni mwa nyumba zao wakati jimbo la Kibamba na Ubungo lami ziko barabara kuu tu

Tujifunze kufanya kazi na wabunge, tuunde kamati za maendeleo maaalum kwa jimbo, tuweke mikakati kama jimbo ili kulifanya lifike mbali tuachane na business as usual, thamani ya eneo ni miundo mbinu

SICHANGIAGI SIASA NA SI MWANASIASA ILA NAPENDA WATU TUBADILIKE NA TUTUMIE FURSA KAMA HIZI ALIZOSEMA MH. RAIS KWA WELEDI ILI TUSIZIPOTEZE
Kwa kauli ya mheshimiwa Rais, ahadi ile kwa mbunge haikuwa ya kungojea mpaka 2022. Kama tujuavyo rais wetu ni mtu wa outcome na anachoahidi anatenda. Na alivyomwahidi mbunge alimaanisha anafanya with immediate, hapo ni mbunge kuwahi kutekeleza wajibu wake wa kupeleka barabara hitaji.
 
Nina imani Mheshimiwa Raisi
Mama Samia SH huu ujumbe atakuwa kauona make ni mojawapo ya ahadi za JPM (R.I.P)
 
Back
Top Bottom