Henry Kilewo
JF-Expert Member
- Feb 9, 2010
- 899
- 1,084
Polisi wamepiga simu kwa viongozi wa Chadema Ubungo kuzuia mkutano wa hadhara wa mbunge wa kueleza kazi za mbunge kwa mwaka mmoja pamoja na kupokea maoni ya wananchi kuhusu muswada wa katiba mpya usifanyike.
Sababu walizotoa polisi kwa simu ni kuwa kuna tishio la Alshabab. Polisi walipewa taarifa ya mkutano toka tarehe 3 wakakumbushwa tena tarehe 4 lakini hawakujibu.
Taarifa ndani ya Chadema zinasema kwamba mbunge ameamua kuendelea na mkutano kama kawaida kwa kuwa hakuna katazo la maandishi lililotolewa na polisi.
Mkutano unatarajiwa kuanza saa 10 jioni eneo la Ubungo mwisho pembeni ya stand ya daladala karibu na Yenu Bar.
Update
polisi yakamata gari na kuchukua nyaraka za katiba pamoja na viongozi wa chadema ubungo. Waweka rumande. Mnyika aendelea na mkutano bila vipaza sauti na kuzungumza na wananchi. Wananchi walaani hatua ya polisi, waamua kwenda na mbunge kituo cha polisi kuwatoa waliokamatwa na kudai nyaraka zilizochukuliwa
Sababu walizotoa polisi kwa simu ni kuwa kuna tishio la Alshabab. Polisi walipewa taarifa ya mkutano toka tarehe 3 wakakumbushwa tena tarehe 4 lakini hawakujibu.
Taarifa ndani ya Chadema zinasema kwamba mbunge ameamua kuendelea na mkutano kama kawaida kwa kuwa hakuna katazo la maandishi lililotolewa na polisi.
Mkutano unatarajiwa kuanza saa 10 jioni eneo la Ubungo mwisho pembeni ya stand ya daladala karibu na Yenu Bar.
Update
polisi yakamata gari na kuchukua nyaraka za katiba pamoja na viongozi wa chadema ubungo. Waweka rumande. Mnyika aendelea na mkutano bila vipaza sauti na kuzungumza na wananchi. Wananchi walaani hatua ya polisi, waamua kwenda na mbunge kituo cha polisi kuwatoa waliokamatwa na kudai nyaraka zilizochukuliwa