Mbunge wa Temeke, Abdallah Mtolea ataka CHADEMA ifutiwe usajili

digba sowey

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
7,872
14,294
Mbunge wa Temeke Nchini (CCM) Abdallah Mtolea amehoji kwanini Msajili wa Vyama vya Siasa nchini hakifuti chama cha CHADEMA kutokana na kufanya siasa za fujo na chuki licha ya kupewa meno na sheria iliyopitishwa na Bunge ya kumpa nguvu.

Mbunge huyo ambaye aliwahi kuwa Mbunge kupitia CUF katika jimbo hilo kabla ya kuhamia CCM mwaka 2018, ametoa kauli hiyo leo Aprili 3 2020 wakati akichangia bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2020/2021.

“Mwaka jana tuliboresha sana Sheria ya Vyama vya Siasa na kumpa nguvu sana na meno Msajili wa vyama vya siasa, sasa ni lini atakuwa amejiridhisha kwamba matukio ya fujo, siasa za chuki kuamshwa mihemko ya hasira kwa wananchi zinazofanywa na Chadema kuwa ni sababu za kutosha kukifuta chama hicho,” amesema.

Amesema chama hicho kimesababisha fujo nyingi na miongoni ni fujo zilizosababisha kifo cha mwanafunzi Akwilina Februari 16, 2018 baada ya kukataa amri halali ya polisi na hakionyeshi kujutia jambo hilo.

“Baada ya humu yao Wakafanya vikao vingi wakilia kwa furaha wakati wao wakilia kwa furaha mama wa Marehemu Akwilina analia kwa uchungu. Mama yake Akwilina hana mtu wa kumfuta machozi. Kama sisi sio wa kumsemea ni nani aliyemsemeha,” amesema.

Amesema mbwembwe za kuchanganishana fedha hazikuwa zikifanywa dhidi ya CCM wala Serikali bali ni dhidi ya mama yake Akwilina ambaye amepoteza mtoto.

My take:
Chadema wajihadhari tofauti na hapo tutaongea mengine baada ya uhakiki wa vyama vya siasa kumalizika

Have a good day.
 
Wakuu habari za Leo?

Mheshimiwa Abdaallah Mtolea mbunge wa jimbo la Temeke ametoa pendekezo lake bungeni kuwa haoni sababu ya Chadema kuendelea kuwa chama cha siasa nchini,amemtaka msajili wa vyama vya siasa kukifuta chama hicho Mara moja

Amedai kuwa chadema ni chama kinacho penda Fujo na vurugu hivyo haoni thamani ya chama hicho nchini

My take : chadema wajihadhari tofauti na hapo tutaongea mengine baada ya uhakiki wa vyama vya siasa kumalizika

Have a good day.

Sent using Jamii Forums mobile app

Huyo mbunge hajakosea maana cdm kuendelea kuwa hai ni hatari kwa ccm. Huyo mbunge amewakilisha matamanio ya Magufuli na wanaccm wote. Ccm chini ya Magufuli imejinasibu kufanya mambo makubwa, sambamba na hizo sifa, wamewafanyia uhayawani wote cdm, lakini bado cdm haijafa na wananchi wengi bado wanaipenda sana. Hata ukaguzi wa huyo msajili kwa vyama, lengo hasa ni cdm, na Katazo la mikutano ya siasa lengo hasa ni cdm. Pamoja na visa vyote hivyo bado wananchi wanaipenda sana cdm.

Sasa hatari ya dhahiri inakuja kuwa cdm wanataka tume huru ya uchaguzi, na dalili zote zinaonesha kuwa hili swala litawaweka ccm kwenye wakati mgumu kuliko wakati mwingine wowote, ndio maana NCCR wanapewa nguvu ili kupunguza nguvu ya cdm, lakini nayo haionyeshi kuleta matokeo tarajiwa, hivyo huyo mbunge ametumwa kusema hayo ili kuiondoa ccm kwenye dhahama ya hatari, kwani iwapo cdm wataendelea kulazimisha tume huru ya uchaguzi itakuwa balaa kubwa kwa ccm.
 
Ni swala la muda tu ,wewe subiri,muda sio mrefu kichaka kitawaka moto

Sent using Jamii Forums mobile app

Kuifuta cdm ndio njia pekee ya kuinusuru ccm kwa muda mfupi, lakini kifo cha ccm kipo palepale. Ccm ni cha cha kizazi kilichopita, hata ifanye nini sio rahisi tena kuvutia watu wa kizazi hiki. Hivyo ccm itaendelea kutumia nguvu kwa muda fulani, lakini kwa uzee wake, kifo chake ni dhahiri.
 
Mbunge yuko sahihi maana chama kimrgeuzwa Saccos ya mbowe na majangili wenzake wanao hujumu pesa za chama kwa manufaa binafsi
Kuifuta cdm ndio njia pekee ya kuinusuru ccm kwa muda mfupi, lakini kifo cha ccm kipo palepale. Ccm ni cha cha kizazi kilichopita, hata ifanye nini sio rahisi tena kuvutia watu wa kizazi hiki. Hivyo ccm itaendelea kutumia nguvu kwa muda fulani, lakini kwa uzee wake, kifo chake ni dhahiri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu habari za Leo?

Mheshimiwa Abdaallah Mtolea mbunge wa jimbo la Temeke ametoa pendekezo lake bungeni kuwa haoni sababu ya Chadema kuendelea kuwa chama cha siasa nchini,amemtaka msajili wa vyama vya siasa kukifuta chama hicho Mara moja

Amedai kuwa chadema ni chama kinacho penda Fujo na vurugu hivyo haoni thamani ya chama hicho nchini

My take : chadema wajihadhari tofauti na hapo tutaongea mengine baada ya uhakiki wa vyama vya siasa kumalizika

Have a good day.

Sent using Jamii Forums mobile app
Waanze kufutwa waliopata hati chafu toka kwa CAG.

Huwezi kutumia hela za umma hovyo hovyo.
 
Huyo mtulia anatafuta kiki ya kuonewa huruma ili mchujo apitishe. Namwambia CCM ina wenyewe yeye ni mvamizi na ushongo wa wanaccm kindakindaki watamtupia mbali. Akumbuke Mtemvu anamvutia pumzi hana lake hasitafute kiki kupitia CHADEMA

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Saccos mwisho wake October 2020

Ni kweli, hiyo itafanyika kwa hujuma kwakuwa rais ana nongwa na chuki binafsi dhidi ya cdm, hivyo anaweza kutumia madaraka yake vibaya kunajisi box la kura, ila sio kwa ridhaa ya wananchi. Madai ya tume huru ya uchaguzi yasisite baada ya Katazo la mikusanyiko kutokana na Corona. Toka hapo tutaelewana tabia. Kulazimisha kukaa madarakani kutaigharimu ccm na nchi kwa ujumla. Muda utaamua.
 
Wakuu habari za Leo?

Mheshimiwa Abdaallah Mtolea mbunge wa jimbo la Temeke ametoa pendekezo lake bungeni kuwa haoni sababu ya Chadema kuendelea kuwa chama cha siasa nchini,amemtaka msajili wa vyama vya siasa kukifuta chama hicho Mara moja

Amedai kuwa chadema ni chama kinacho penda Fujo na vurugu hivyo haoni thamani ya chama hicho nchini

My take : chadema wajihadhari tofauti na hapo tutaongea mengine baada ya uhakiki wa vyama vya siasa kumalizika

Have a good day.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nikisoma hii meseji inaniuma kweli. Yani kura yangu nilimpa huyu mwehu...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom