Mbunge wa Sirisia John Waluke ahukumiwa kuhudumu kifungo cha miaka 67 gerezani au faini ya KES 1Billion kwenye kesi ya ufisadi dhidi yake

pingli-nywee

JF-Expert Member
Sep 16, 2015
11,923
13,344
Siku ya 40 ya mwizi hatimaye ilitimia kwa Mbunge wa Sirisia John Waluke na mshukiwa mwenza Grace Wakhungu, kwenye kesi ya ufisadi dhidi yao ndani ya mahakama ya ufisadi(Anti-Corruption Court) jijini Nairobi hivi majuzi.

Hii ni baada ya Chief Magistrate Elizabeth Juma kuwapata na hatia, wao na kampuni yao ya Erad Supplies and Contracts Limited, kwenye wizi wa KES 247Million za NCPB(National Cereals and Produce Board). Ambapo wawili hao na Erad Ltd walipokea hela kwenye kandarasi hewa ya kuwauzia NCPB mahindi miaka miwili iliyopita.

Mbunge John Waluke na Grace Wakhungu ambao walikuwa 'directors' wa Erad Supplies watahudumia vifungo vya miaka 67 na 69 mtawalia au walipe faini ya jumla ya KES 2.1Billion. Kongole kwa hakimu Elizabeth Juma na idara ya mahakama pia, kwa kazi nzuri hii kwenye vita vikali hivi dhidi ya ufisadi. Kazi iendelee.

 
As I know, if they are connected to Jublee watasafishwa kama pamba.
 
As i know, if they are connected to Jublee watasafishwa kama pamba
Wasafishwe na nani baada ya kuhukumiwa? Rais mwenyewe hana uwezo huo au madaraka ya kufanya hayo. Hakimu akishatoa maamuzi yake uheshimiwa huwa unaishia hapo, hata panya na mende wote kwao nyumbani watahama.

Hakuna pa kupenyeza isipokuwa kukata rufaa kabla ya siku 14 baada ya hukumu kutolewa, ambayo ni haki ya kila mkenya kikatiba.
 
Wasafishwe na nani baada ya kuhukumiwa? Rais mwenyewe hana huo uwezo au madaraka ya kufanya hayo. Hakimu akishatoa maamuzi yake uheshimiwa huwa unaishia hapo, hata panya na mende wote kwao nyumbani watahama. Hakuna pa kupenyeza isipokuwa kukata rufaa kabla ya siku 14 baada ya hukumu kutolewa, ambayo ni haki ya kila mkenya kikatiba.
Muosho mmoja tu pale capital Hill.

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
 
Wasafishwe na nani baada ya kuhukumiwa? Rais mwenyewe hana huo uwezo au madaraka ya kufanya hayo. Hakimu akishatoa maamuzi yake uheshimiwa huwa unaishia hapo, hata panya na mende wote kwao nyumbani watahama. Hakuna pa kupenyeza isipokuwa kukata rufaa kabla ya siku 14 baada ya hukumu kutolewa, ambayo ni haki ya kila mkenya kikatiba.
Look at waiguru impeachment, how it was handled na uache kutubeba Wana.

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
 
As i know, if they are connected to Jublee watasafishwa kama pamba

Kivipi labda, maana kwetu huku taasisi ndio zinafanya kazi, rais hana uwezo kama nilivyoona kwenu eti anaamrisha mafisadi waombe msamaha, waingine kwenye makubaliano fulani na DPP halafu yaishe, huku rais hatakuokoa hata kama anakupenda kivipi.
 
It's just PR ,the real thieves are based at Statehouse led by Wanjohi wamashati AKA metameta.

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
Mimi naona Walukhe afungwe kama kameiba ndo ikifikia akina Uhunye na Ruto hakutakua na excuse.

Kama kuna evidence utafungwa tuu. 'Being caught with yours hands inside the cooking jar' Ata wizi inataka ujanja mingi sana.

Alot of errad boys kama Waluke ndo hua wanaumia sababu majina yao ndo inatumika kufungua makampuni ambayo pesa ya corruption zitawekwa.

Unaeza pata ata Waluke kwa hio 290m alikula pesa kidogo sana lakini pesa kisheria iliwekwa kwa kampuni yake kwa hio yeye ndo ataenda ndani sio mwenye alimtumia(big fish) kuiba hiyo pesa.
 
Look at waiguru impeachment, how it was handled na uache kutubeba Wana.
Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
MCAs wa Kirinyaga tayari wamewasilisha kesi. I hope Waiguru ataondolewa kupitia mahakama ndio washike adabu zao. Pale Seneti kuna mapimbi wa aina yake. Sijam'beba' mtu yeyote kama unavosema. Naamini kwa uhakika kwamba mahakama ndio 'the last frontier' kwenye vita dhidi ya ufisadi na vita pia dhidi ya 'interferance' za kisiasa.
 
If they sing BBI song you won't hear about that case anymore, that judgement was made to create fear among those with dissenting views so that they drop their stand and join the caravan.

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
Uhuru na Raila wanajipa stress za bure tu na hiyo BBI yao. Wakati wake utakapowadia sisi wakenya ndio tutaibwaga chini.
 
Mimi naona Walukhe afungwe kama kameiba ndo ikifikia akina Uhunye na Ruto hakutakua na excuse.

Kama kuna evidence utafungwa tuu. 'Being caught with yours hands inside the cooking jar' Ata wizi inataka ujanja mingi sana.

Alot of errad boys kama Waluke ndo hua wanaumia sababu majina yao ndo inatumika kufungua makampuni ambayo pesa ya corruption zitawekwa.

Unaeza pata ata Waluke kwa hio 290m alikula pesa kidogo sana lakini pesa kisheria iliwekwa kwa kampuni yake kwa hio yeye ndo ataenda ndani sio mwenye alimtumia(big fish) kuiba hiyo pesa.
The company was opened in 2004 with Jacob juma as director waluke by then was Moody awori's PA na hapo ndio maana waliweza kufanya biashara na awori's sister.The fine was abnormal and it will go nowhere,look at samburu governor's fine and babu owino ukitoa fine kwa mihemko ujue hio case haiendi popote, court of appeal will reverse that fine,na utaona akilipa around 20 M , and by the way it will take a political angle na itafifia tu.

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
 
MCAs wa Kirinyaga tayari wamewasilisha kesi. I hope Waiguru ataondolewa kupitia mahakama ndio washike adabu zao. Pale Seneti kuna mapimbi wa aina yake. Sijam'beba' mtu yeyote kama unavosema. Naamini kwa uhakika kwamba mahakama ndio 'the last frontier' kwenye vita dhidi ya ufisadi na vita pia dhidi ya 'interferance' za kisiasa.
Mahakama ipo ICU just like parliament expect it to clear waiguru,at the moment nothing good can come out of courts other than jailing opponents with awkward jail term and exorbitant fine.

Sent from my CPH1937 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom