Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini ajiuzulu nafasi ya Mnadhimu wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni

digba sowey

JF-Expert Member
Mar 1, 2017
7,883
14,322
Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini amejiuzulu na kumtaka M/kiti wa Chadema, Freeman Mbowe kumteua mtu mwingine kukaimu nafasi ya Mnadhimu wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni

Amesema tangu alipomkaimisha hajawahi kumpa barua rasmi wala kumthibitisha katika kukaimu nafasi hiyo.

---
My take ,kufikia Oktoba CHADEMA itabaki na mwenyekiti na katibu peke, Mungu ni mwema siku zote
Screenshot_20200113-212020~2.png

Screenshot_20200113-212103~2.png


Sent using Jamii Forums mobile app
 

Attachments

  • SELASINI MBUNGE1.pdf
    308 KB · Views: 3
  • SELASINI MBUNGE2.pdf
    274.3 KB · Views: 1
Huko nyuma kuna mahali niliandika kuwa mpaka 2020 wakati wa uchaguzi Chadema haita kuwa na nguvu tena

Sent using Jamii Forums mobile app

..Mbowe ana wakati mgumu.

..Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya upinzani amepigwa RISASI ktk eneo linalolindwa na serikali, baada ya hapo Spika amemvua ubunge kwasababu zisizo na ubinadamu wala mashiko.

..Ikiwa Kiongozi wa kambi ya upinzani atateua mbunge mwingine kujaza nafasi ya Mnadhimu wa kambi ya upinzani, atakuwa anabariki na kuhalalisha yaliyomtokea TL.

..kwa hiyo hili ni suala la KIMSIMAMO. Ni bora kutokuwa na mnadhimu wa upinzani kuliko kuhalalisha shambulizi la kigaidi dhidi ya TL na ukatili aliotendewa baada ya hapo.
 
Tatizo itakuwa fungu la Mnadhimu Mkuu lote anakula Kiongozi wa Upinzani Bungeni

Ukiwa huna barua rasmi ya uteuzi unakosa nguvu ya kisheria kudai mafungu ya ofisi husika

Mbowe kaifaidi sana Chadema kuanzia Ruzuku mpaka Viti maalum

Iyo hajapewa barua rasmi ni zuga tu
 
Hila zote zitashindwa kama zilivyoshindwa,kuna wakati Wassira alisema Chadema haitafika 2015,ikatunisha Msuli hasa,na kuna mtu aliwahisema"mpaka 2020 upinzani utakufa",leo ni Siku 14 zimepita.
Selasini atapoteza umaarufu kama mzee Balozi na Chadema itaongeza wanachama na mashabiki.
 
Wakati anamteua huyo mbowe hakujua hili? Acheni kujitekenya ,kiufupi huko chadema kuna fukuta sana,time will tell

Sent using Jamii Forums mobile app

..amemkaimisha.

..maana yake ni kwamba Mbowe bado anamtambua TL kama mnadhimu wa kambi ya upinzani bungeni.

..Mbowe akimthibitisha Selasini atakuwa anahalalisha kuwa ni sahihi TL kuvuliwa ubunge, na pia ni halali alivyopigwa risasi.
 

Nijipe moyo kwa kipi? Hata Selasini angejiuzulu ubunge, bado cdm haiwezi kuwa dhaifu kwa ajili ya nafasi ya kimadaraka ya huyo Selasini. Wameondoka wabunge na madiwani kibao kwenda ccm, lakini bado ccm inanajisi uchaguzi ili ibaki madarakani, itakuwa hiyo Selasini kutokuwa mnadhimu wa kambi ya upinzani bungeni?
 
Back
Top Bottom