Mbunge wa Pakistan mwenye asili ya Tanzania alaani ubaguzi wa rangi unaofanyika nchini Marekani

STRUGGLE MAN

JF-Expert Member
May 31, 2018
8,638
16,566
Mbunge wa Pakistan mwenye asili ya Tanzania alaani ubaguzi wa rangi Marekani

Mbunge mmoja wa Pakistan mwenye asili ya Afrika amekosoa vikali vitendo vya utumiaji mabavu na ubaguzi wa rangi dhidi ya raia wa Marekani wenye asili ya Afrika.

Mbunge huyo wa jimbo la Kusini mwa Pakistan mwenye asili ya Tanzania amelaani vikali wimbi la ubaguzi wa rangi na ukatili wa polisi ya Marekani dhidi raia weusi wa nchi hiyo.

Tanzilah Qanbarani mwenye umri wa miaka 41 ni mwanamke wa kwanza kutoka jamii za walio wachache kujitosa katika siasa na kugombea ubunge nchini Pakistan. Anasema lengo lake kuu la kuingia kwenye siasa ni kupigania maslahi ya jamii za walio wachache.

Mbunge huyo wa Uttar Pradesh nchini Pakistan amesema, "jamii zetu zinapaswa kuwa huru na kuwa mbali na vitendo vya kibaguzi haswa ubaguzi dhidi ya watu weusi."

Maandamano ya kulaani ubaguzi dhidi ya watu weusi yameshuhudiwa ndani na nje ya Marekani

Ameashiria kuhusu matatizo yanayowakali watu weusi wa jamii ya Sheedi katika nchi hiyo ya Asia ambapo amesema watu wa jamii hiyo wanabaguliwa hata katika sekta ya elimu. Aghalabu ya watu 250,000 wa kabila la Sheedi wanaishi kusini mwa mkoa wa Sindh, na katika maeneo ya kusini mwa Punjab.

Kadhalika amelaani mauaji ya kikatili ya George Floyd aliyekuwa na umri miaka 46, ambaye aliaga dunia baada ya kukabwa shingoni kwa goti na polisi mzungu kwa jina la Derek Chauvin kwa muda wa dakika tisa huko Minneapolis jimboni Minnesota Mei 25 mwaka huu. Kifo cha kikatili cha raia huyo Mmarekani mweusi mwenye asili ya Afrika kimeibua maandamano makubwa nchini Marekani na katika nchi nyingine huku watu wakiendelea kupinga vitendo vya mabavu vya polisi na ubaguzi wa rangi nchini Marekani.

4bvaa9f23cd5bb1oiy8_800C450.jpg
 
Hawa Pakistan wanaoua Wapakistan wenzao kisa Ni Wakristo au Wahindi au ndio wanajidai Wanatetea haki za minority? Makubwa..!

Kule hata ukiwa Muislam mwenzao Ila hauna msimamo mkali unauawa, Kuna Waziri alipinga Sheria Kali ya hukumu ya kifo kwa anayekufuru akauawa na wananchi wenye hasira
 
Mbongo mwenzako huyo mkuu
Hawa Pakistan wanaoua Wapakistan wenzao kisa Ni Wakristo au Wahindi au ndio wanajidai Wanatetea haki za minority? Makubwa..!

Kule hata ukiwa Muislam mwenzao Ila hauna msimamo mkali unauawa, Kuna Waziri alipinga Sheria Kali ya hukumu ya kifo kwa anayekufuru akauawa na wananchi wenye hasira
 
Pakistan kitivo cha Ugaidi hapo mashariki ya kati, Huyo Mbunge akemee kwanza ya Kashmir na Uighur wa China.
 
Pakistan kitivo cha Ugaidi hapo mashariki ya kati, Huyo Mbunge akemee kwanza ya Kashmir na Uighur wa China.
... hapo alipo anaongea huku akitetemeka kwa hofu maana muda wowote bomu laweza kulipuka tokea upande wowote. Nchi ya kishetani ile.
Kwahio mme mmaind hapo kuukemea huo ubaguzi

Kuna watu bado mko utumwani aseee....

dudus:
bhachu:

mnamatatizo sana WAYAHUDI...
 
Mtanzania gani huyo apewe ubunge Pakistan, huyo ni mpakistan tu ila labda alizaliwa huku.

Hakuna watu wabaguzi kama wapakistan wao wanafahamu binadamu ni muislamu aliye tayari kuchinja mwenzie kwa jina la Allah. Bure kabisa hao.
 
Mtanzania gani huyo apewe ubunge Pakistan, huyo ni mpakistan tu ila labda alizaliwa huku.

Hakuna watu wabaguzi kama wapakistan wao wanafahamu binadamu ni muislamu aliye tayari kuchinja mwenzie kwa jina la Allah. Bure kabisa hao.
Mbna unatoka povu hata google pia inakushinda

WAYAHUDI mnashida gani kwan ?!
 
Back
Top Bottom