Mbunge wa Nyamagana ashikiliwa na Polisi

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
POLISI mkoani Mwanza Desemba 15 ilimshikilia kwa mahojiano Mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje (Chadema), kutokana na madai ya kutoa maneno ya uchochezi wakati alipohutubia wananchi hivi karibuni kwenye Uwanja wa Sahara jijini hapa.

Mahojiano baina ya mbunge huyo na Jeshi la Polisi yalianza saa 11.30 jioni baada ya mbunge huyo kujisalimisha mwenyewe polisi akitokea Dar es Salaam.

Wenje alikuwa ameambatana na wakili wake pamoja na Katibu wa Chadema Mkoa wa Mwanza, Wilson Mshumbusi.

Gazeti hili lilifika polisi saa 12 jioni na hadi saa 1.15 usiku, mbunge huyo alikuwa bado akiendelea kuhojiwa.

Katika mkutano huo, Wenje anadaiwa kuwahamasisha wananchi kufika kwa wingi katika ofisi za Halmashauri ya Jiji Mwanza leo kwenye uchaguzi wa Meya wa Jiji ili kuhakikisha Chadema inashinda kiti hicho huku akiwasisitiza kufanya kama vile walivyofanya wakati wa kutangaza matokeo ya ubunge.

Wakati wa kutangaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 31, mwaka huu, vijana wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chadema walifanya uharibifu wa miundombinu pamoja kuchoma moto jengo la CCM na kutishia kuchoma moto ofisi za Halmashauri ya Jiji wakishinikiza msimamizi wa uchaguzi kutangaza matokeo.

Hata hivyo, jeshi hilo limepiga marufuku wananchi ambao sio wafanyakazi wa halmashauri kufika katika jengo la Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa nia ya kufanya vurugu siku ya uchaguzi wa Meya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Simon Sirro alithibitisha kushikiliwa kwa mbunge huyo na kueleza kuwa baada ya mahojiano, aliachiwa kwa dhamana.

“Ni kweli tulimshikilia na kumhoji kwa saa takribani nne, lakini tulimuachia kwa dhamana baada ya kuandika maelezo yake,” alisema Kamanda Sirro na kuongeza kuwa mbunge huyo alikiri kuhamasisha wananchi kwenda jiji kusikiliza matokeo ya uchaguzi wa Meya.

Hata hivyo, Kamanda Sirro alisema ushahidi kwa upande wa polisi umekamilika na kwamba faili limepelekwa kwa Mwanasheria wa Serikali kwa hatua zaidi za kisheria.

Sirro alisema ofisi yake imekuwa ikipokea ushahidi kutoka kwa wananchi waliohudhuria mkutano wa Wenje juu ya kauli za uchochezi alizozitoa na hivyo waliona ni bora akakamatwa na kuhojiwa juu ya kauli hizo.
 
Hizi ndiyo siasa za tanzania. Uhuru unahitajika, wenje anaonewa
 
Nimeona hapojuu wanasema uchaguzi wa meya wajiji la mwanza unafanyika leo je nani ameshinda?ni chadema matarajio itashinda je matokeo rasmi imekuaje?mwenye data atupatie jamani.
 
POLISI mkoani Mwanza Desemba 15 ilimshikilia kwa mahojiano Mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje (Chadema), kutokana na madai ya kutoa maneno ya uchochezi wakati alipohutubia wananchi hivi karibuni kwenye Uwanja wa Sahara jijini hapa.

Mahojiano baina ya mbunge huyo na Jeshi la Polisi yalianza saa 11.30 jioni baada ya mbunge huyo kujisalimisha mwenyewe polisi akitokea Dar es Salaam.

Wenje alikuwa ameambatana na wakili wake pamoja na Katibu wa Chadema Mkoa wa Mwanza, Wilson Mshumbusi.

Gazeti hili lilifika polisi saa 12 jioni na hadi saa 1.15 usiku, mbunge huyo alikuwa bado akiendelea kuhojiwa.

Katika mkutano huo, Wenje anadaiwa kuwahamasisha wananchi kufika kwa wingi katika ofisi za Halmashauri ya Jiji Mwanza leo kwenye uchaguzi wa Meya wa Jiji ili kuhakikisha Chadema inashinda kiti hicho huku akiwasisitiza kufanya kama vile walivyofanya wakati wa kutangaza matokeo ya ubunge.

Wakati wa kutangaza matokeo ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 31, mwaka huu, vijana wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chadema walifanya uharibifu wa miundombinu pamoja kuchoma moto jengo la CCM na kutishia kuchoma moto ofisi za Halmashauri ya Jiji wakishinikiza msimamizi wa uchaguzi kutangaza matokeo.

Hata hivyo, jeshi hilo limepiga marufuku wananchi ambao sio wafanyakazi wa halmashauri kufika katika jengo la Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa nia ya kufanya vurugu siku ya uchaguzi wa Meya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Simon Sirro alithibitisha kushikiliwa kwa mbunge huyo na kueleza kuwa baada ya mahojiano, aliachiwa kwa dhamana.

"Ni kweli tulimshikilia na kumhoji kwa saa takribani nne, lakini tulimuachia kwa dhamana baada ya kuandika maelezo yake," alisema Kamanda Sirro na kuongeza kuwa mbunge huyo alikiri kuhamasisha wananchi kwenda jiji kusikiliza matokeo ya uchaguzi wa Meya.

Hata hivyo, Kamanda Sirro alisema ushahidi kwa upande wa polisi umekamilika na kwamba faili limepelekwa kwa Mwanasheria wa Serikali kwa hatua zaidi za kisheria.

Sirro alisema ofisi yake imekuwa ikipokea ushahidi kutoka kwa wananchi waliohudhuria mkutano wa Wenje juu ya kauli za uchochezi alizozitoa na hivyo waliona ni bora akakamatwa na kuhojiwa juu ya kauli hizo.

Nadhani tunahitaji maana nyingine ya demokrasia hapa kwetu, Kama kuhamasisha watu kusikiliza matokeo ya uchaguzi ni hatia.,mmh!!
 
CCM wameshajipanga kuchakachua matokea wako radhi kufanya kama baraza la katiba la cote d' ivoire lilivyofanya kupindisha matokeo ili wasilipoteze jiji hilo la pili kwa ukubwa nchini linalokua kwa kasi na lenye mapato mengi. Kutokana na hali hiyo ndio maana wameanza kutumia dola kutisha wananchi kwa sababu wanajua nini wamepanga kukifanya.. Najua kamanda sirro hataki kulaumia kama alivyolaumiwa wakati wa matokeo ya ubunge...
 
Back
Top Bottom