Ujira wa mwihaalipewa takrima
Akiwa ni miongoni mwa wabunge wa CCM waliopita bila kupingwa, mbunge huyu amekuwa kama mtalii katika bunge letu mjini Dodoma.
Aliyekuwa mgombea wa ubunge kupitia CHADEMA maarufu kwa jina la " Focus" alijitoa dakika za mwisho na kumfanya mama huyu kupita bila kupingwa.
Lakini cha ajabu huyu mama hajawahi kuisimamia serikali kutokana na ahadi alizozitoa mh Rais ikiwamo kuunganishwa kwa jimbo la Ngenge katika gridi ya taifa.
Sasa basi sisi kama vijana tunakuahidi mh Mbunge kwamba hautorudi mjengoni tena baada ya 2015!
TUMECHOKA
Mkoa gani wa wapambanaji?mbona wabunge wenu wote ni design moja?Huyu Mhe. Asumpta hafai hata kidogo kuwakilisha mkoa wa wapambanaji kama Kagera. Nikikumbuka matusi, vijembe, hoja za uongo na dharau wakati wa bunge maalumu la katiba. Hatuwezi kuwa na mbunge wa mipasho wa namna hii katika maswala muhimu kama kutunga katiba mpya.
Haaaah khaaa khaaa Teh Teh Teh kwi kwi kwi ! !Tatizo huko mliko hakuna watu,wapo kenge ndio maana mmechagua kenge mwenzenu!Nawachukia sana ccm.
Habari zenu watanzania. Huu ni ujumbe mahususi kwa wana Nkenge na wapenda maendeleo ya jimbo letu. Hivi kweli tulikosa mtu makini, msomi na thabiti mwenye kuweza kuleta maendeleo kwa jimbo letu. Huwa nashikwa na aibu kubwa pale ninapoona mawazo ya mbunge wetu akichangia hoja mbalimbali bungeni na hata nje ya bunge kwa maana hayo mawazo na michango yake huesabika kuwa ametumwa na wananchi wa Nkenge. Ebu rejea michango yake ya escrow na katiba. Naomba kuwauliza wana Nkenge, je ni kweli hatuna watu wazuri wenye uwezo wa kuwasilisha mawazo na michango yetu iliyosahihi pale bungeni? Nachelea kusema kuwa tukiendelea kumkumbatia huyu mama tunaendelea kudumaza maendeleo yetu na tunashusha hadhi yetu wanankenge.