Mbunge wa Muleba Kusini, Profesa Tibaijuka aliaga Bunge kwa kilio

Etwege

JF-Expert Member
Jul 4, 2018
5,703
15,156
Mbunge wa Muleba kusini Prof Anna Tibaijuka leo tarehe 3, April 2020 wakati akichangia bajeti ya Waziri Mkuu ameliaga Bunge na kutangaza rasmi kuwa hatagombea tena ubunge kwenye Uchaguzi Mkuu mwaka huu.

Prof. Tibaijuka ameliaga Bunge kwa kilio cha kuhukumiwa bila kusikilizwa kwenye sakata la Tegeta Escrow ,amesema hali hiyo ilimuumiza sana na ameacha andiko lake kwa Waziri Jenista Mhagama akilitaka bunge lifanye mabadiliko ya kusikiliza kwanza watuhumiwa kabla ya kuwahukumu.

Prof. Tibaijuka amesema baada ya kustaafu rasmi ubunge sasa anaenda kuwa mwandishi wa vitabu ili ayaweke kwenye kumbukumbu yote mengi aliyojifunza kwenye safari yake ya utumishi.

My take
Na wabunge wengine waliokaa muda mrefu bungeni kama akina Mbowe ni vizuri wakaiga mfano wa Prof Anne Tibaijuka wa kustaafu kwa hiari na kuachia wengine siyo kusubiri mpaka uzomewe jimboni na wananchi kwamba wamekuchoka ondoka.
 
Analia nini kama sio mnafiki? Alikuwa mbunge ameshindwa kupeleka hoja binafsi ili bunge kurekebishe hiyo kuhukumu bila kusikiliza.

Anataka waliobaki bungeni ndio wafanyie kazi matamanio yake? Hivyo vitabu sijui kitabu akiandika atasoma yeye na wajukuu zake.
 
Analia nini kama sio mnafiki? Alikuwa mbunge ameshindwa kupeleka hoja binafsi ili bunge kurekebishe hiyo kuhukumu bila kusikiliza, anataka waliobaki bungeni ndio wafanyie kazi matamanio yake? Hivyo vitabu sijui kitabu akiandika atasoma yeye na wajukuu zake.
Tulia kwanza, inaonekana una hasira sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kurudisha bilioni 1.6 inauma sana,hadi kitabu cha mipasho kwa hasira

$iasa imeharibu CV yake...hadi cheo cha kuwa Propesa mtuhumiwa wa escro

*ashukuru ana nyongo kali na inamsaidia

imagine: amekamata bilions na hakunenepa hata pua na ameitema bilions bila kukonda hata mdomo
 
Analia nini kama sio mnafiki? Alikuwa mbunge ameshindwa kupeleka hoja binafsi ili bunge kurekebishe hiyo kuhukumu bila kusikiliza, anataka waliobaki bungeni ndio wafanyie kazi matamanio yake? Hivyo vitabu sijui kitabu akiandika atasoma yeye na wajukuu zake.
Hii ndiyo ilitakiwa iwe hoja. Kuwataka watu wengine wafanye kwa niaba yako ni uoga uleule . Wanapokuwa kwenye vikao vya chama hana uthubutu wakati akijua kuwa ndiko penye maamuzi

Odhis *
 
Back
Top Bottom