Mbunge wa Mlimba, Godwin Kunambi: Tujenge 'Monument' ya kumuenzi Hayati Dkt. Magufuli jijini Dodoma

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
617
1,797
Leo Jumanne, tarehe 30 Machi, 2021, Mbunge wa Jimbo la Mlimba mkoani Morogoro, Godwin Kunambi ametoa mapendekezo ya kujenga monument ya kuenzi kazi iliyofanywa na rais Magufuli.

Akichangia hoja Bungeni, Kunambi amesema:

Kazi kubwa ambayo mimi naomba nishauri Bunge letu tukufu ni... amefanya mambo makubwa ndani ya nchi na kukumbukwa kwake itakuwa ni jambo la msingi sana.

Ukienda South Africa pale Johannesburg, utaona kuna mnara pale lakini pia kuna sanamu zuri sana ya Mandela, wanaita Mandela Square.

Kwa kazi kubwa aliyoifanya kuhamisha makao makuu yetu ya nchi kuja Dodoma; hapa Dodoma kuna eneo tengwa la serikali; lina hati miliki maeneo ya Chimwaga. Na Chimwaga tunaifahamu kihistoria — zaidi ya heka 100 zimetengwa pale kwa ajili ya recreational park, eneo la mapumziko.

Niombe kushauri Serikali; ingefaa tujenge monument pale. Tujenge monument ambayo wajukuu, watoto na kizazi kijacho kitakuwa kinasema, "Magufuli ni nani?"— wanakwenda pale.

Na hii itasaidia kumjengea heshima kubwa kwa aliyotutendea Watanzania.
 
Kunambi amepiga sana hela za miradi ya kustawisha makao makuu akiwa sambamba na Meko .wabunge wasiunge mkono hiyo hoja.
 
Marais wakristu ni wabinafsi sana. Mbona hamna mtu anasema tujenge sanamu ya Kikwete. Hivi hawa watu wamelogwa au ni nini? Huyo magufuli mpora uchaguzi ndiyo wanamwona wa maana
Kazi zake na matokeo ya hizo kazi! Ndo inamfanya aseme hivyo. Sasa kikwete ajengewe ndege inayoenda angani na kusema rais wa angani au?? JPM amepiga kazi ndugu! Kama alikutumbua! Pole kwa hilo. Na hauna haja ya kulaumu! ni vyema ukaangalia ni wapi ulikosea.
 
Marais wakristu ni wabinafsi sana. Mbona hamna mtu anasema tujenge sanamu ya Kikwete. Hivi hawa watu wamelogwa au ni nini? Huyo magufuli mpora uchaguzi ndiyo wanamwona wa maana
Baadhi yao. Mimi nawafahamu Wakristo baadhi wenye utu sana. Tusiwajumuishe wote.
 
Back
Top Bottom