SEAL Team 6
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 655
- 118
Ukimaliza kumuuliza Bashe, nenda kamuulize Gikwangala.
Yawezekana ni kweli katika kutafuta maisha na alipopata pesa na ideas za kusaidia bongo kama malaria no more akajivua gamba na kurudi, sasa sijui inafanananje na elimu ya nyalandu, mama nagu, udokta wa JK, na ufisadi wa magamba
Hivi unajua tuna waziri foreigner?
better nusu shari kuliko shari kamili
Sugu kweli amejilipua Uingereza na kweli alishinda kesi yake ya ukimbizi na makaratsi alipata ya kufanyia kazi, na ana pasipoti ya Uingereza ingiwa atumii jina la Mbilinyi.
Mwaka 2000 nimekutana nae Uingereza alikuwa anakaa Milton Keynes, karibia na duka DEBENHAMS, wanaopinga hawajui chochote kuhusu sugu
Halafu mbona we mjeshi umekomaa na sugu wivu ni mbaya,mbona mzee mkapa an asili ya msumbiji lakin aliongoza nchi vizur zaid ya handsome kikwete,obama hapend ubaguzi.
Mkuu naona hii inamkamata pabaya Mr. II. Kama hakurekebisha mambo yake kama marafiki zangu wengi ambao nawajua kuwa waliji;ipua kama wakimbizi wa Burundi wakaishi huko ughaibuni wakarudi bila kuomba upya uraia wa Tanzania, basi tena Mr. II huenda akawa si Riziki kwenye Ubunge!!
Sugu mwenyewe ndio aliidanganya Serikali ya Uingereza hayo mambo yanafanyika sana ata mimi ningetaka kujilipua ningefanya hivyo huko Uingereza wakati nipo huko ukifika pale MILTON KEYNES kuna Watanzania kibao pale kama kariakoo, wanashirikiana na wanasheria wa kinigeria unawapa pesa wanawafungulia kesi za kudai ukimbizi, pasipoti zenu mnazichoma moto, mimi nimekaa sana Berkshire Vanwall Road, Hili jambo badae litakuja kuichafua vibaya CDMTuliona Jenerali Ulimwengu alivyotiwa kitahanani wakati wa Mkapa kuhusu uraia wake, nashaangaa hawa uhamiaji leo wanasikia au wanajuwa kuwa kuna Mbunge ambae ni mkimbizi wa Kirundi na ana passport ya kiingereza wanashindwa kumuhoji ukweli. Halafu utakuta mtu kama huyu anaingizwa bungeni, sehemu nyeti na anaingizwa kwenye kamati hata za ulinzi na kadhalika. wakati ukimpima "credibility" yake haimruhusu hata kusogelea jengo la bunge, iwe tu kwa kudanganya kwake huko Uingereza na kula viapo huko kuwa yeye ni Mrundi. Huo ni uongo tosha wa kumvuwa joho la Ubunge.Nashangaa sana labda iwe alitumwa na serikali ya Tanzania kwenda kuchunguza watu wanaojiruwa huko Uingereza. Kwani lolote linawezekana. Ikiwa huyu anawekwa bungeni na anawachwa kuwa katika mmoja wa mihimili ya hii nchi, kwanini? Serikali itueleze, alitumwa huko Uingereza au ni yeye mwenyewe aliiidanganya serikali ya Uingereza kwa njaa zake?
tunaulizia uraia wa sugu wakati yuko mjengoni?kwa hiyo vyombo vyetu vya usalama sio makini!Ok kama hatuongele ukabila sasa nauliza tena kwani Rostam ni raia wa nchi ipi?Mkuu hapa si suala la ukabila hapa ni suala la uraia. Hiyo post sikuisoma wakati huo. Lakini huenda kuna ukweli ndani yake kwa kuwa kuna kaka yake ambaye naye nasikia alijilipua huko ughaibuni na akawa anaishi kama mkimbizi huko Uholanzi kwa sasa nasikia yupo hapa nchini. Kuna wakati nilimsikia akiwa katika mambo ya akina Aunt Ezekiel!! Kwa mwendo huo huenda ikawa Mr II naye alijilipua. Akanushe habari hii.Watanzania wengi sana walishajilipua kama wakimbizi wa Burundi na baada ya muda wanarudi lakini wanasahau kuuhuisha uraia wao. Kama Mr. II alifanya hivyo basi tena!!Kuna watu wanasema ukitaka kuonekana wewe ni mchafu ama msafi kiasi gani basi ingia kwenye siasa!! Siasa itakuumbua
Hee sasa mkuu passport yake ya Uingereza inatumia jina gani? Hii ndiyo Tanzania usiyoijua; Mawaziri ni madokta wa kughushi, wabunge ni wakimbizi, duh tutafika kweli?
sijawahi kusikia hili kabila la kibulushi hapa tanzania labda limeanzishwa na familia ya Rostamu,Rostam ni Mbulushi kwa asili na ni Raia wa Tanzania kwa kuzaliwa yeye na wazee wake na hajawahi kuwa mkimbizi. Wacha.
Mkuu, unaelezwa Sugu ni Raia wa Uingereza na ana passport ya huko kwa mapenzi yako unasema labda ana Travel document!Mkuu sio passport labda travel document!
Kama Balali sio wa Tanzania basi ni Sugu anapata Excuse, nimekupata mkuuBalali alikuwa raia wa tanzania?
Mkuu MTM, hayo ndiyo mambo ya kujadili hapa. Kama kuna waziri foreigner atajwe tumjadili. Udaktari wa baadhi ya watu ni kichefuchefu na sijui kuna mtu wa kuwatetea. Ila udaktari wa JK ni sawa kabisa kwa kuwa ni wa heshima. Mimi nadhani wanatakiwa wachukuliwe hatua za kisheria. Kuna jamaa mmoja anaitwa msemakweli aliwaanika wengine wakasema wanmshitaki. Sijui nini kinaendelea. Kosa ni kosa tu uwe Magamba au Ngozi!! Kama magamba wana waziri foreigner ni kosa na asemwe na kama CHADEMA wana Mbunge Mrundi asemwe! Hii nchi ni yetu sote na hawa watu wanatutawala sote.
MTM lete habari
Mkuu, unaelezwa Sugu ni Rais wa Uingereza na ana passport ya huko kwa mapenzi yako unasema labda ana Travel document!