HNIC
JF-Expert Member
- Sep 6, 2011
- 1,898
- 2,195
Katika hali isiyo ya kawaida Mbunge wa Kisiwa cha faia bwana Abdulkarim Shah ameamua kufanya ambayo hayajawahi kutokea kisiwani Mafia. Bwana Shah amesema kuwa anafuata maneno na vitendo vya baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kwa kutangaza kuwa ana NGATUTA na hatogombea tena ubunge kwa sababu za kiafya na anaona bora azipishe damu changa ambao wanaweza kukifikisha kisiwa cha mafia kuwa na maendeleo kama visiwa vya Taiwan.
Ndugu Shah amesema kuwa anashukuru Mnyaaaz Mungu kumjaalia na anategemea kutoa taarifa rasmi kupitia kwenye ukurasa wake wa Facebook, twitter, na whatsapp. Pia vile vile Shah anasema kuwa kashazifikisha hizo taarifa kwa katibu mkuu wa CCM taifa, Mwenye kiti wa CCM taifa ambao wamefurahishwa sana na uzalendo na siasa za ukomavu za kungatuka akama alivyofanya baba wa Taifa mwalimu Nyerere.
Amesisitiza kuwa yeye sasa hivi anataka afanye jitihada za kwenda kufanya ibada ya Umra na kushughulika na masuala ya uvuvi na pia kuendeleza biashara zake za trucks na bila kusahau kuweka familia yake sawa.
Mbunge Shah amesema kuwa atamuunga mkono mgombea yoyote yule na hasa ikiwa mgombea huyo ni Kijana Msomi na kadhalika. Ikumbukwe kuwa Ndugu Shah alikuwa anasakamwa sana na aliyekuwa mtoto wa jimbo hilo (Omari Kimbau) kuwa Shah alikuwa hajasoma na kaishia darasa la pili na hajui kusoma wala kuandika (sifa ambazo kwa kweli imeshindikana kuzithibitisha).
Omari Kimbao ambaye ana miliki Baa Mbali mbali za Pombe hapa Dar amekuwa naye anafanya kampeni za chini kwa chini na ametenga kiasi cha Bilioni 1 ili kuweza kuwanunua CCM wilaya, Mkoa na Taifa ili jina lake lipite na hatimaye kuupata ubunge wa Kisiwa cha Mafia.
Kama kawaida ya Jamiiforums tutaendelea kuwaletea habari kwa kadri muda unavy