Mbunge wa Kisese, Luhaga Mpina aitaka Serikali itaje zilipo Tsh. Trilioni 360

Hizo zilitokana baada ya ripoti ya madini kubaini kwamba kampuni za madini kwa miaka yote zilizokuwepo nchini wakichimba madini walikuwa halipi stahiki ya nchi kwa thamani hiyo kupitia utoroshaji wa makinikia.

Baadae mazungumzo yalipokamilika mkuu wa kampuni kutoka Marekani bwana Thorn alikubaliana kutoa kishika uchumba cha dola bilioni 360

Sijui tafsiri hapo ni ipi ni mpaka mjumbe maalumu aliyeshirika aje afafanue kwa kina ili jukwaa waelewe hizo shilingi trilioni 360 ni zipi?

Inawezekana kwenye baraza walikuwa na mengi ambayo yalikuwa yanajiri ila umma ulifichwa kwa sababu maalumu lakini sasa ufukunyunyu utasababisha balaa kwenye mamlaka.




Ilikuwa dollar milioni 400 na sio dollars bilioni
 
Ilikuwa dollar milioni 400 na sio dollars bilioni
Hata wewe umekosea ukweli ni huu
Dola milioni 300 sawa na shilingi za kitanzania 690,390,118,566.54


Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli wiki hii alikutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof John L Thornton.

Tanzania imepoteza takriban shilingi za kitanzania trilioni 188 (dola bilioni 84 za Marekani ) katika kipindi cha miaka 19 kati ya mwaka 1998 na mwaka 2017 kupitia usafirishaji wamakinikia ya dhahabu na shaba.

Kampuni ya inayomiliki migodi ya madini nchini Tanzania, Barrick Gold imekubali kuilipa Serikali ya Tanzania hisa ya asilimia 16 na mgawo wa asilimia hamsini ya mapato ya mauzo ya dhahabu kutoka migodi 3 inayoimiliki.




Hatua hiyo ni utekelezaji wa sheria mpya za madini ya Tanzania baada ya kampuni hiyo kukubali kuwa na mazungumzo na Serikali ya Tanzania .

Vilevile kampuni hiyo imekubali kutoa Dola za Kimarekani milioni 300 kama malipo ya kuonesha nia njema ya kufidia fedha zilizotokana na upotevu wa mapato kutokana na biashara ya kampuni hiyo.

Mkurugenzi mtendaji wa kampuni hiyo,Prof. Thornton amesema Barrick Gold Corporation watazingatia makubaliano haya na wanaamini kuwa yamefungua ukurasa muhimu utakaowezesha kufanya biashara kisasa.

Source: BBC News/Swahili: Kampuni ya Barrick yakubali kuilipa Tanzania dola za Marekani milioni 300
 
Mpina mnafiki tu, si alikuwa Waziri ktk serikali ya awamu ya 5, alikuwa wapi kushughulikia haya anayosema na kama waziri alikuwa na sauti na nafasi kubwa kuwezesha hizo fedha kupatikana na kuipa mbinu serikali wakati ule.

Majitu mengine hovyo sana, once you have given them good position in the government yako kimya tu hawatendi yale wanayojua vema kuisaidia serikali, yakitoka nje ya serikali, yanaanza kupiga kelele, tulishauriiii, tulishauriiiii.. nyoko nn
 
Mpina mnafiki tu, si alikuwa Waziri ktk serikali ya awamu ya 5, alikuwa wapi kushughulikia haya anayosema na kama waziri alikuwa na sauti na nafasi kubwa kuwezesha hizo fedha kupatikana na kuipa mbinu serikali wakati ule.

Majitu mengine hovyo sana, once you have given them good position in the government yako kimya tu hawatendi yale wanayojua vema kuisaidia serikali, yakitoka nje ya serikali, yanaanza kupiga kelele, tulishauriiii, tulishauriiiii..
Alikuwa busy na kuhamasisha wananchi kutembea na futi kwa ajili ya kupimia samaki
 
Nimefuatilia mijadala inayoendelea bungeni kuhusu Mpango wa Taifa wa Maendeleo nikamsikia Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina akizungumzia namna Serikali inavyoshindwa kukusanya fedha nyingi kutokana na kutokuwepo usimamizi madhubuti.

“Mhe. Mwenyekiti tulisema hapa wabunge tunazo Trilioni 360 zimeshikiliwa na Mahakama, uamuzi haujatoka nilitegemea kwenye mpango hapa isemwe kwamba hizo Trilioni 360 ziko wapi leo hapa Bunge zima linapiga makofi kwa Trilioni 1.3 tulizopewa na IMF fedha ndogo Trilioni 1.3 tunapiga makofi mpaka mikono inauma na kwakweli tunashukuru kwa hilo"

Mpina alisema asilimia 10 Trilioni 360 ni Trilioni 36 lakini bado hilo halijawauma, Bunge halijaumia, Serikali haijaumia lakini fedha zimeshikiliwa tu kinachosubiriwa ni maamuzi tu ya Mahakama.

“Kama tatizo ni hizo bodi zetu za rufaa za kodi zinashida ya wataalamu si tuajiri hata wataalamu wa kutoka nje kama tatizo ni wataalamu nini kinachosababisha mpango haujazungumza suala hilo?” amehoji

Ni vizuri Wabunge wangeungana kuzidai hizo fedha zingeleka ahueni kubwa na Maendeleo makubwa kwa Taifa letu.
 
Atakachoambulia ndugu Mpina ni kuambiwa mtetea legacy! Watanzania baadhi yetu hatujui tunachokitaka ama bila kujua ama kwa makusudi mbali na uelewa na nafasi tulizonazo.
====
Tunaomba ufafanuzi hizo tri 360 tunamdai nani?
 
Kiukweli wengi wetu tunahitaji uelewa na ufupisho makini huo mzigo mkubwa. Na Kama zipo kwanini kiongozi wa maamuzi Magumu JPM alipotezea??
 
Mpina yuko kwenye ndoto, nadhani hayuko sawa. Ana natural arrogance ya kisukuma, si alikuwa Waziri, kwanini hakuishauri serikali wakati alikuwa na nafasi nzuri mwaka mmoja tu hata haujapita, mnafiki sana huyu jamaa, appearance tu he looks arrogant.
 
Mpina yuko kwenye ndoto, nadhani hayuko sawa. Ana natural arrogance ya kisukuma, si alikuwa Waziri, kwanini hakuishauri serikali wakati alikuwa na nafasi nzuri mwaka mmoja tu hata haujapita, mnafiki sana huyu jamaa, appearance tu he looks arrogant.
Kwahiyo maana yako ni ipi? Hizo pesa hazipo, kwamba ameongea uongo..?
 
Mpina na muanzisha mada wote ma zuzu..

Dollar milioni 400 inakuwaje trilioni 360?

Mnaijua trilion 360? Ni uchumi wote wa south Africa au Nigeria

Pathetic
 
Nimefuatilia mijadala inayoendelea bungeni kuhusu Mpango wa Taifa wa Maendeleo nikamsikia Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina akizungumzia namna Serikali inavyoshindwa kukusanya fedha nyingi kutokana na kutokuwepo usimamizi madhubuti.

“Mhe. Mwenyekiti tulisema hapa wabunge tunazo Trilioni 360 zimeshikiliwa na Mahakama, uamuzi haujatoka nilitegemea kwenye mpango hapa isemwe kwamba hizo Trilioni 360 ziko wapi leo hapa Bunge zima linapiga makofi kwa Trilioni 1.3 tulizopewa na IMF fedha ndogo Trilioni 1.3 tunapiga makofi mpaka mikono inauma na kwakweli tunashukuru kwa hilo"

Mpina alisema asilimia 10 Trilioni 360 ni Trilioni 36 lakini bado hilo halijawauma, Bunge halijaumia, Serikali haijaumia lakini fedha zimeshikiliwa tu kinachosubiriwa ni maamuzi tu ya Mahakama.

“Kama tatizo ni hizo bodi zetu za rufaa za kodi zinashida ya wataalamu si tuajiri hata wataalamu wa kutoka nje kama tatizo ni wataalamu nini kinachosababisha mpango haujazungumza suala hilo?” amehoji

Ni vizuri Wabunge wangeungana kuzidai hizo fedha zingeleka ahueni kubwa na Maendeleo makubwa kwa Taifa letu.
Huyu Luhaga Mpina naye si Mwendazake alisemaga ni kichaa kichaa kama yeye! Hivi trilioni 360 anazijua ! Kusoma ukubwani na kwa kuungaunga ni shida sana!
 
Wana Bodi hili suala la Tranfer Pricing alilogusia Mh. Luhaga Mpina Bungeni limekaaje.

Nimemsikia Mpina akizungumzia suala la ‘transfer pricing’ ambalo wabunge walishauri Serikali wakati wa Bunge la Bajeti mwaka huu kwamba kuna makampuni ya kimataifa 504 yenye miamala zaidi ya Trilioni 105 kwa mwaka na uwezo wa TRA kuyakagua makampuni hayo ni asilimia 1, TRA haina wataalamu, haina fedha na haiwezi kukagua miamala hiyo ya TP na hivyo Serikali haiwezi kupata kodi katika maeneo hayo fedha nyingi za watanzania zinapotea.

“Mhe. Mwenyekiti haya yote kwetu sisi mipango yetu hatuoni kama ni shida lakini tukiletewa hata bilioni 5 tunafurahi kweli kweli lakini fedha zetu zimeshikiliwa na watu hatupati hasira katika hili”

Sasa nini hatma ya Taifa letu katika suala hili la la Makampuni hayo 504 ambayo tunapoteza Trilioni 105 kwa mwaka.
 
Back
Top Bottom