Tetesi: Mbunge wa Kibamba ( CHADEMA) , Mheshimiwa John Mnyika kuongea na wanahabari Jijini Dsm

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,552
Habari ambazo zimenifikia mimi Hivi Punde kutoka kwa Mnyetishaji wangu ndani ya CHADEMA ni kwamba, Mh John Mnyika , Mbunge wa Kibamba ( CHADEMA ) ataongea na waandishi wa habari wakati wowote kuanzia jumatatu ya October 15,2018.

Atakuwa na Mh. Joshua Nassari na Joseph Haule, wote kutoka CHADEMA.

Mbowe atakula nyama zake.

Muda utaongea.
 
Fyekelea mbali ni balaa, Chadema atabaki mwenyekiti wa kudumu na Salary slip. Chadema ina laana ya Dr. Slaa. Karma inafanya kazi.
 
Kwanza ninashangaa mtu mwenye akili zako kamili unashabikia kuingia garama za kurudia uchaguzi majimbo ambayo yana wabunge na ni wabunge hao hao watakao kwenda kugombea tena, hivi ni nani aliwaloga watanzania mbona wenzetu hapa Kenya tu jirani na sisi wako tofauti kabisa kimawazo tunatatizo gani sisi? Sasa kwanini tusiwe masikini milele kama ndo vitu tunavyoona vya kushabikia hivyo. Mtanzania tena mlipa kodi unanufaika vipi mbunge akiacha jimbo lake na kuchaguliwa tena katika jimbo hilohilo. Mbona mi siyo mwanasiasa lakini naumia sana kodi ninayolipa halafu inatumika kwenye hayo mambo. Sijui tunapata wapi ujasiri wa kushabikia mambo yanayotutia umaskini mi binafisi hivyo vitendo sioni tofauti na uhujumu uchumi kwakweli. Kama Mbunge anajihuzulu aache huo ubunge asigombee tena lakini leo anaacha kesho anaomba kuchaguliwa awe Mbunge wa jimbo hilohilo, hapana kwakweli huko ni kutuletea umaskini kwa makusudi. Hata kujitegemea nchi haijaweza inategemea misaada halafu kidogo tunachopata kinachezewa kwenye hizo chaguzi za marudio. Mungu iokoe nchi yangu isiangamie.
 
Back
Top Bottom