mjoli wa kweli
JF-Expert Member
- Jan 26, 2017
- 630
- 381
Hivi mtu hawezi kuwa kuunga mkono jitihada za serikali kuleta maendeleo akiwa upinzani ? Kiazi
Na si kulogwa tu bali pia na yeye KANUNULIWA na wenye chamaWa kumlaumu Nyalandu yeye ndie alianza mchezo wa kujivua ubunge na kwenda chama kingine na alipofanya hivyo hatukusikia kelele zote hizo bali alionekana shujaa,ila wengine wakitumia haki yao wale wavuka mto Mara huja na kejeli na matusi kibao,basi hata Nyalandu atakuwa amerogwa
"CHADEMA wekeni STRATEGIES (mikakati) MPYA ili kuwa-ATTRACT WANACHAMA (waliopo na wapya)" ..... Kaushauri muafaka ... but sidhani kama katapewa uzito katika nyakati hizi za SINGO MPYA inayo-hit isemayo KUNUNULIWA WAPINZANI ... ninapita nitarudi baadaenyie mliohama wote ni wasaliti,
Kama CCM inavutia,ndio mlitakiwa mpigane ndani ya chama chenu, muweke strategies mpya kuwaatract wanachama wapya,sio kuhama,
Nawashangaa sana,mnataka turudi kwenye serikali ya chama kimoja,sidhani kama lipo duniani?????????????!!!!!!!!!!,
Tanzania haitawasamehe kwa hili,
wapinzani wapo kucreate balance,at least serikali inawork within boundaries,sasa mkicreate chama kimoja huoni kama mnmapa Rais afanye anavyotaka?????? akifanya lolote la hovyo mtakua na audacity ya kumkosoa ???demokresia ndio bye bye kulinda matumbo yenu!
Hivi katika hao WAHAMAJI si Nyalandu pia yumo ama mie niko nyuma ya PAZIA ... na mbona nae haitwi MSALITI kwa walompigia kula kule jimboni kwake? au kwa kuwa kavaa GWANDA ....Ila Nyarandu namuaminia ana maakili akipewa nafasi na wengine yeye pamoja na Lowasa,Tundu lisu akipona,wakikaa pamoja na kuweka mkakati wa chama chao,watafanikiwa tu,......wasipanick
Una akili sana. Sasa uchaguzi ujao wa jimbo hilo, waambie cdm wawaeke jiwe au mbuzi ili tu prove point yako.This guy is too NAIVE ........... Nafikiri wana Siha walichagua chama. Hawakuchagua mtu!!
Inawezekana kabisa kufanya hivyo (kupongeza juhudi) ... tatizo ni pale ambapo yule aisifuye serikali anaposhambuliwa kama mpira wa kona na kuanza kuitwa MSALITI na kukaliwa na vikao ... rejea sakata la Mh. Nasari aliposhambuliwa na kusakamwa humu SOCIAL MEDIA kisa kaipongeza serikali ya awamu ya tano chini ya JPMHivi mtu hawezi kuwa kuunga mkono jitihada za serikali kuleta maendeleo akiwa upinzani ? Kiazi
Swadakta.Siasa ni kama safar,ukiona basi linatoka Dsm kuelekea Mwanza na abiria akashukia Moro,Dom,Singida,Tabora au Shinyanga usimlaumu kwa kuwa safar yake inaishia hapo!
Mbunge wa Jimbo la Siha kwa tiketi ya CHADEMA, Godwin Ole Mollel ajiuzulu nafasi hiyo pamoja na uanachama wa CHADEMA kuanzia leo Disemba 14, 2017.
Mwanasiasa huyo amesema kuwa ameshindwa kuukataa ukweli huu kuwa hivi sasa uongozi wa nchi yetu chini ya Chama cha Mapinduzi (CCM) umedhihirisha wazi kupigania rasilimali za nchi na kwa kuwa niliomba ridhaa ya Ubunge kwa ahadi ya kupigania rasilimali za nchi nimejikuta sina namna nyingine zaidi ya kujivua uanachama wa CHADEMA na kujiuzulu Ubunge wangu ili niungane na CCM katika jukumu hili muhimu kwa Taifa.
Nimefanikiwa kuipata barua yake ya kujiuzulu na kujivua uanachama wa CHADEMA;
Video
Huu mchezo hauhitaji hasira. Mbona hukutoa povu walivyohama nyala? Hukuona hasara kwa taifa wala ccm? Ccm hawakukatishwa tamaa? Kwanini hutaki kuongea ukweli? Kwanini unakuwa kipofu na kiziwi kiasi unajitoa ufahamu? Tunafanya makosa kuwaona hawa wanaohamia ccm ni wasaliti na wanaohamia cdm ni makamanda. Cdm ni kuwambia ukweli tu, viongozi wetu wajitathmini, na wawe na mikakati vitendo hivi visijirudie. Sio kuwapa moyo wa kijinga kabisa. Ila nakupongeza kuwa tahadharisha hao ccm.Kama ilivyo katika mapenzi, kuwa si kila mmoja huwa ni mpenzi bali wengine huwa ni wapenzi watazamaji!!!
Mniwie radhi kwa kauli hii kuwa nchi yetu bado haijatunukiwa wanasiasa wakomavu na wenye kusimamia nia njema ya chama chao, wengi wapo ku struggle ili wapate chochote. Mtu anapoacha ubunge kwa kigezo cha kumuunga mkono rais huyo ni muongo kwasababu kufanya uchaguzi ni gharama kuliko hata kumuunga mkono rais!!!
Watu wa namna hii nashauri hata utendaji wa kata wasipewe, maana ni wanafiki wanadhani wanakisaliti chama na wakati wanawasaliti wananchi walio wachagua.
Nyerere na wapigania uhuru wetu wangekuwa na fikra mbovu Kama hizi za kutamani tamani nadhani mpaka Leo tungekuwa colony la mwingereza, wazee wetu hawa hawakuikimbia TANU kwenda kumuunga mkono gavana Richard Turnbull. Walisimamia Nia yao moja na wakaridhika na kidogo walichokuwa nacho hatimaye tukafanikiwa kupeperusha bendera yetu na kutambulika kama Taifa.
*ANGALIZO KWA CCM*
Kuweni makini sana na wanademokrasia uchwara kama hawa.
Chama kisijivune kurusha vyavu katika dimbwi kubwa la samaki. Kumbukeni si vyote vinavyokuja ni samaki, kuna vyura na kenge pia.
Watu hawa wasio na misimamo wala uchungu na Taifa maskini kama hili, wanaoacha majimbo yao ili hela ambayo ingefanya shughuli zingine za maendeleo ikafanye uchaguzi wa marudio ktk majimbo yao ni wa kuogopa kama ukoma!!
Nashauri CDM wasikatishwe tamaa na hawa wanaharakati hewa.
*Ni maoni tu wapendwa *
Unakimbilia wapi? Tulia aandike vizuriDuh!!!!
Aiseeee!!!
Hapa kazi tu naona inautia wengi.
CHADEMAHuyo mbunge wa Siha ni chama gani?
Correct. Watafakali upya siasa za ndani ya chama kabla hawajotoka nje. Lowassa ndio sumu kuuChadema wafanyie marekebisho sera zao na Mwenendo wao haiwezekani kila Mbunge awe amenunuliwa
Huyo aliamua kuachana na wajinga wasioweza kujibu hoja kwa hoja badala yake kutumia maguvu na vitishoHahaahaaa...muasisi was kampeni hii anajulikana mkuu ni Lazaro Nyalandu, alidhani wengine watamfuata huko alikokimbilia bahati mbaya upepo umegeuka. Muwe wapole ndo makali ya msumeno yalivyo