Mbunge wa Jimbo la Siha, Godwin Aloyce Mollel(CHADEMA) ajivua wadhifa huo na kuhamia CCM

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Mbunge wa Jimbo la Siha kwa tiketi ya CHADEMA, Godwin Ole Mollel ajiuzulu nafasi hiyo pamoja na uanachama wa CHADEMA kuanzia leo Disemba 14, 2017.

Mwanasiasa huyo amesema kuwa ameshindwa kuukataa ukweli huu kuwa hivi sasa uongozi wa nchi yetu chini ya Chama cha Mapinduzi (CCM) umedhihirisha wazi kupigania rasilimali za nchi na kwa kuwa niliomba ridhaa ya Ubunge kwa ahadi ya kupigania rasilimali za nchi nimejikuta sina namna nyingine zaidi ya kujivua uanachama wa CHADEMA na kujiuzulu Ubunge wangu ili niungane na CCM katika jukumu hili muhimu kwa Taifa.

Nimefanikiwa kuipata barua yake ya kujiuzulu na kujivua uanachama wa CHADEMA;

Video




24c9272f-29ec-44f8-b0f7-95ef6f7c33d2.jpeg
 
Back
Top Bottom