Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,087
- 6,568
Nimemsikiliza mbunge wa Geita mjini ndugu Costantine Kanyasu kwa kweli anashangaza sana. Nini kimemfanya akurupuke kuanza kutoa maoni kama haya kabla ya uchunguzi?
Nilimsikiliza waziri Jaffo alipopewa kazi yake ya kwanza kuunda tume kuchunguza ubadhilifu halimashauri ya Geita,alisema pesa mil 400 zilizotumika hazikupitishwa na baraza la madiwani.
Nashangaa nimemsikiliza mbunge wa Geita anaongea na media na kudai kuwa amepitia document hapo halmashauri na amebaini kuwa pesa hizo zilipitishwa na baraza la madiwani,pia anasisitiza Gpsa walitumiwa kununua hilo gari la mil 400,kwa hiyo taratibu zote zilifuatwa maana Gpsa ndie wakala wa manunuzi wa serikali.
Mbali na hayo anasema mkurugenzi aliyesimamishwa ni muadilifu na amekuwa akipambana na ufisadi kwa muda mrefu. Je ina maana Mbunge wa Geita vijijini ni muongo? Anaropoka hovyo na kumdanganya rais,maana huyu ndie aliyemlipua mkurugenzi kuwa alifanya ubadhirifu wa mil 400.
Nilimsikiliza waziri Jaffo alipopewa kazi yake ya kwanza kuunda tume kuchunguza ubadhilifu halimashauri ya Geita,alisema pesa mil 400 zilizotumika hazikupitishwa na baraza la madiwani.
Nashangaa nimemsikiliza mbunge wa Geita anaongea na media na kudai kuwa amepitia document hapo halmashauri na amebaini kuwa pesa hizo zilipitishwa na baraza la madiwani,pia anasisitiza Gpsa walitumiwa kununua hilo gari la mil 400,kwa hiyo taratibu zote zilifuatwa maana Gpsa ndie wakala wa manunuzi wa serikali.
Mbali na hayo anasema mkurugenzi aliyesimamishwa ni muadilifu na amekuwa akipambana na ufisadi kwa muda mrefu. Je ina maana Mbunge wa Geita vijijini ni muongo? Anaropoka hovyo na kumdanganya rais,maana huyu ndie aliyemlipua mkurugenzi kuwa alifanya ubadhirifu wa mil 400.