Mbunge wa Dodoma Mjini, Anthony Mavunde ashiriki zoezi la ufunguzi wa barabara zilizokuwa hazipitiki kwa muda mrefu

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Jan 5, 2013
658
821
Mbunge wa Dodoma Mjini Mhe. Anthony Mavunde ashiriki zoezi la ufunguzi wa barabara zilizokuwa hazipitiki kwa Muda mrefu

Mbunge wa Dodoma Mjini Mhe. Anthony Mavunde leo ameshiriki na viongozi wa Kata ya Chigongwe kukagua zoezi la kufungua barabara yenye urefu wa kilomita 5.2 kutoka eneo la Chigongwe-Ngh’ambala ikiwa ni sehemu wa utekelezaji wa Ahadi za Mbunge huyo za kufungua barabara hiyo ambayo imekuwa kero ya muda mrefu kwa wananchi wa eneo hilo.

Kukamilika kwa barabara hiyo kutapunguza adha ya matumizi ya muda mrefu ya kusafiri kutoka eneo moja kwenda eneo lingine ndani ya kata ambapo awali wananchi walikuwa wakipata tabu kupita maeneo yasiyo rasmi kwasababu ya kukosekana kwa barabara inayounganisha mitaa husika.

"Tumeanza sasa ukarabati na kuboresha miundombinu ya barabara mbalimbali za ndani ya Jiji na pembezoni ya Jiji ili kuwapunguzia adha wananchi kutokana na kutopitika kwa urahisi kwa baadhi ya barabara katika maeneo mbalimbali" alisema Mhe. Mavunde

Nitaendelea kushirikiana na TARURA kuhakikisha tunayafikia maeneo mengi zaidi yenye barabara korofi kadri bajeti itakavyoruhusu.

Ora et Labora”Sala na Kazi”

De Populo servorum “Mtumishi wa Watu”

FB_IMG_1620401484497.jpg


FB_IMG_1620401482083.jpg


FB_IMG_1620401470878.jpg


FB_IMG_1620401466215.jpg


FB_IMG_1620401468513.jpg
 
Zamani sana... narudia, kitambo sana wakati nipo bwa mdogo tu!!

Basi bhana... ikawa nipo ground floor na mdada fulani hivi! Huyu mdada alikuwa mshikaji wangu sana ingawaje alikua mkubwa sana kwangu... Tom Boy fulani hivi!

Baada ya kupiga stori mbili tatu mara akaja binti mmoja ambae alikuwa dada wa kazi wa jirani yao! Swali lake la kwanza kwa huyu Housegirl lilikuwa "...mbona umechelewa, ulikuwa unafanya nini?"!

"Samahani dada, nilikuwa naoga..." Ndo jibu alilotoa yule binti, nami nilipoinua macho kumtazama, nikakuta kweli alikuwa na maji maji mwilini!

"Yaani hapo ndo umetoka kuoga? Kabla hujaoga ulikuaje?" Rafiki yangu huyu akamuuliza swali lingine la kijeuri yule housegirl!

Kwa mara nyingine, na bila kutarajia, nikajikuta nainua tena shingo kumtazama yule binti aliyedai anatoka kuoga!! Ingawaje sikukusudia lakini nikajikuta tu nikijiuliza swali lile lile lakini kimoyomoyo!!!

Anyway, hata sijui ni kwanini nimeukumbuka huo mkasa...

Hongera sana Mheshimiwa Mavunde kwa kuanza ukarabati na uboreshaji wa miundombinu Jijini Dodoma!!
 
Yaani wagogo mna tabu,....kabisa ukarabati wa barabara tena ukiwa ni bado mnabaki na vumbi mnauita ukarabati?ndo maana watu kama Ndugai wanawatawala kiwepesi kutokana na nyie ni watu wakuridhika hovyo kama hivi.

Tanzania kuna maeneo matukio kama haya yakifanyika wala hawapigi picha kurusha mitandaoni.
 
kukagua zoezi la kufungua barabara yenye urefu wa kilomita 5.2 kutoka eneo la Chigongwe-Ngh’ambala ikiwa ni sehemu wa utekelezaji wa Ahadi za Mbunge huyo za kufungua barabara hiyo ambayo imekuwa kero ya muda mrefu kwa wananchi wa eneo hilo.
Nadhani hili jimbo lilikua likiongozwa na Upinzani ndio maana zilikua hazipitiki na zimekua kero kwa muda mrefu!!
 
Huyu hakuna Mbunge hapo ni kibaka fulani tu ambaye mwendazake kwa ushamba wake alidhani ni vijana wa maana kumbe ni chawa wa kila mtoa pipi
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom