FairPlayer
JF-Expert Member
- Feb 27, 2006
- 4,145
- 716
Hongera wananchi kwa kuonyesha yanayowasibu!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hongera wananchi kwa kuonyesha yanayowasibu!
Siku zote wanaopinga kuhusu uzomeaji,naona leo wameamka na kukubali kuwa kuna uzomeaji.Huyo mbunge kama alienda kinyume na hao wananchi,alistahili kuzomewa,kwani yeye ni nani?Upinzani sio malaika,wana makosa pia,kuna wenye jazba pia.Sio wote waliopo upinzani kuwa wanafaa,hapana wapo wasiofaa pia.
Ila tutazidi kuzomea mafisadi ndani ya ccm kwa nguvu zote,hayo ya mwenyekiti wa kijiji ni minor case tu,wale wanaoiba billions of money ndio tunapambana nao.
Ila tutazidi kuzomea mafisadi ndani ya ccm kwa nguvu zote,hayo ya mwenyekiti wa kijiji ni minor case tu,wale wanaoiba billions of money ndio tunapambana nao.
Kama kuna mafisadi ambao hawako ndani ya CCM hawatazomewa? au ni mafisadi ambao ni wa nndani ya CCM tuu? au tuseme ufisadi unazomewa kutegemea na chama? Inawezekana fisadi akitoka CCM akijiunga na upinzani yeye jina lake litabadiliaka na kuwa malaika sio? Mimi nadhani tutawazomea mafisadi wote siku zote hata kama wako makanisani, misikitini, na vyamani.
Kama kuna mafisadi ambao hawako ndani ya CCM hawatazomewa? au ni mafisadi ambao ni wa nndani ya CCM tuu? au tuseme ufisadi unazomewa kutegemea na chama? Inawezekana fisadi akitoka CCM akijiunga na upinzani yeye jina lake litabadiliaka na kuwa malaika sio? Mimi nadhani tutawazomea mafisadi wote siku zote hata kama wako makanisani, misikitini, na vyamani.
Mtoto wa mkulima, nadhani humu ndani nimepiga sana kelele kuhusu haya mambo ya vyama na watu/watu na vyama lakini watu hawasikii ! kilichobaki sasa ni ushabiki tu, nikishabikia chama changu nitaambiwa mie mwendawazimu kwa sababu kule kuna mafisadi, sasa hao mafisadi ndio ccm jamani au they happen to come from ccm ? kwingine kwenye upinzani hakuna mafisadi ? haijalishi fisadi mdogo, fisadi mkubwa wote ni fisadi !
Watu wapo wazi sana kuona failures za serikali lakini sio success, na wengi huchukia wakiona JK anafanya vizuri, wao wanataka kila siku JK aboronge tu ili waanze kupiga zogo !
Kama kuna fisadi ndani ya ccm, hao ni wao mafisadi lakini sio chama, chama kipo pale na watu nenda rudi huamia pale na sio chama kuhama na kuwafuata watu !
Njoo taratibu,CCM ndio imejaa mafisadi,hata na upinzani kama kuna mafisadi nao watazomewa kwa kwenda mbele.Soma barua ya Butiku,ujionee mambo ndani ya ccm,naona watanzania wengi bado mpo usingizini.Ufisadi ndani ya CCM ni 97% labda 3% ndio wasafi,upinzani wanaweza kuwa na ufisadi 5%, wengi ni wasafi 95%,nao wakiingia madarakani wakishindwa kazi tutawachambua kama karanga,huoni Kibaki wanavyomchambua.Amkeni usingizini.
DC, mbunge chupuchupu kutwangana hadharani
2007-10-18 09:44:56
Na Bigambo Jeje, PST Tarime
Mkuu wa Wilaya ya Tarime mkoani Mara, Bw. Stanley Kolimba na mbunge wa Tarime (CHADEMA), Bw. Chacha Wangwe, nusura watwangane makonde mbele ya wananchi wakati wa mkutano wa kusuluhisha mgogoro wa ardhi baina ya wanakijiji wa Nyakunguru na wawekezaji wa mgodi wa dhahabu wa North Mara ulioko wilayani hapa.
Pamoja na kwamba `hawakuzipiga` Mkuu wa Wilaya kwa jazba alivunja mkutano huo na kuuahirisha hadi wakati mwingine baada ya kuzuka makundi mawili ya wananchi waliotofautiana juu ya suala la viongozi halali wa kijiji hicho na kusababisha vurugu za hapa na pale, licha ya ulinzi mkali wa askari wapatao 15 waliokuwa na silaha kuwepo kwenye mkutano huo.
Tafrani hiyo ilizuka kufuatia mzozo mkubwa uliojitokeza baina yao mara baada ya Bw. Kolimba aliyekuwa ameitisha mkutano huo kutaka mwenyekiti wa kijiji hicho, Bw. Abel Maginga ambaye amekataliwa na wananchi mara kadhaa mbele ya viongozi, kufungua mkutano huo.
Baada ya Bw. Kolimba kumtaka Bw. Maginga kusimama kufungua mkutano huo, mamia ya wananchi waliokuwepo walilipuka kwa mayowe wakipaza sauti kuwa hawamtaki kwa sababu wameshamkataa mbele ya viongozi mbalimbali, akiwemo Bw. Kolimba.
Alipotaka kupuuza matakwa ya wananchi, Mbunge Wangwe alimcharukia mkuu huyo wa wilaya aliyekuwa wamekaa naye meza moja akimtaka asikilize madai ya wananchi badala ya kutumia madaraka, jambo lililozua mzozo mkubwa baina ya viongozi hao.
Mzozo huo uliwafanya viongozi hao kila mtu kumpandishia jazba mwenzake na kusababisha wananchi kubaki midomo wazi huku wakiona viongozi wao wakitoleana maneno makali kwenye mkutano huo wa kujadili na kupata ufumbuzi wa mgogoro wa ardhi uliodumu kwa zaidi ya mwaka moja.
Ugomvi huo kati ya viongozi hao wawili wa ngazi ya juu ulitulizwa na Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Tarime, Bw. Bandola aliyeingilia kati kuwataka washushe jazba ili waendelee na mkutano na wananchi wanaodai wananyang`anywa ardhi yao kinyemela na uongozi wa mgodi wa North Mara unaotaka kuwalipa fidia ndogo.
Wakiongelea chanzo cha mzozo huo, Mkuu wa Wilaya alidai Bw. Wangwe alitaka afuate matakwa yake ya namna ya kuongoza mkutano huo, jambo ambalo alipinga na hivyo kuzua mzozo.
Kwa upande wake, Bw. Wangwe alisema mzozo huo ulizuka baada ya Bw. Kolimba kukataa kuwasikiliza wananchi ambao wana haki ya kuamua kile wanachotaka.
Akizungumza mara baada ya mkutano huo kuvunjika, Bw. Wangwe alisema joto la mgogoro wa ardhi wa Nyakunguru linazidi kupanda kila siku kutokana na serikali ya CCM kuwakumbatia viongozi wa mgodi huo na kuwasahau wananchi ambao wana haki yao ya kisheria.
Bw. Kolimba alikanusha madai yaliyotolewa na mbunge huyo ya kuwakumbatia viongozi wa North Mara katika mgogoro huo ambapo alidai yeye si kibaraka wa mgodi huku akitoa kauli ya mshangao kwamba hajawahi kupokea orodha ya wananchi waliodhulumiwa ardhi yao na mgodi huo katika vijiji vya Kewanja, Nyangoto na Matongo.
SOURCE: Nipashe
Mkuu heshima kwako, mimi nakukubali sana kwani siku zote huwa tupo pamoja. Yeah report nilishaisoma vizuri sana na kuielewa. My point is mafisadi ni mafisadi tuu hata wawe wapi na hilo mkuu bila hiyana umekubaliana nalo. Sasa ningependa pia tuungane wote il tupambane nao woete 100% hiyo 97% ya CCM na hiyo 3% zote bila kujali itikadi za chama. Mkuu nashukuru kabisa kwenye thread zako za siku za nyuma uliwahi kusema mimi msimamo wangu sio wa SISIEM na nafurahi kwa wewe kujua hilo mkuu sasa lets kanyaga twende kwa manufaa ya taifa zaidi kuliko ya kichama.