Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,898
MBUNGE wa Bunda Mjini, Ester Bulaya (CHADEMA) ameshikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam (Central) kwa madai amebakishwa kwa ajili ya upelelezi.
Bulaya aliripoti leo kituoni hapo baada ya kutakiwa kufanya hivyo, akiongozana na Viongozi wengine wa CHADEMA akiwemo Mwenyekiti, Freeman Mbowe ikiwa ni moja ya sharti la dhamana yao katika kesi inayowakabiri.
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Vincent Mashinji amesema kuwa baada ya kuripoti kituoni hapo viongozi wote waliruhusiwa kuondoka lakini Bulaya alitakiwa kubaki kwa sababu ya upelelezi.
“Mbunge Bulaya amebaki mahabusu kwa sababu za kiupelelezi lakini tumeambiwa ataunganishwa katika shauri letu lililokuwa mahakamani Kisutu,” amesema Mashinji.
Hata hivyo ameeleza kuwa upelelezi utakapokamilika Bulaya atafikishwa mahakamani na kuunganishwa katika shauri la viongozi wengine ambao walishafikishwa mahakamani.
Kuripoti kwa viongozi hao ni moja ya sharti la dhamana katika kesi yao namba 112/2018 katika mahakama ya Kisutu Dar es Salaam.