Elections 2010 Mbunge wa Arusha apigwa hadi kuzirai na jeshi la polisi

Kwa niliyoyasikia toka Arusha kwa mkereketwa wa CDM Mheshimiwa LEMA ALIOMBA KICHAPO KILE YEYE MWENYEWE!!
  1. Wao CDM walishagoma kwenda kwenye uchaguzi, wenzao wakaendelea! Kama sheria ilikiukwa (na CCM) basi CDM wangesubiri kupinga hilo kwa kufuata sheria!!
  2. Kuingia ukumbini wakati kikao cha uchaguzi (walichokigomea CDM) kimemalizika na kuanzisha vurugu ya kupinga matokeo ilitafsiriwa kama "kuvuruga amani"...na mbaya zaidi...
  3. Sheria ya nchi (Under the Criminal Procedures Act ikisomwa pamoja na Law of Evidence na Katiba yetu) inawaruhusu Polisi (au mtu yeyote aliyepewa dhamana ya kulinda usalama) kutumia "nguvu ya kiasi" wakati wa kumkamata (Arrest) na kumdhibiti (restrain) mhalifu/mtuhumiwa asilete madhara!! Bwana Lema alitoa BASTOLA, ni dhahiri endapo asingedhibitiwa angeweza kumdhuru mtu (Kwa kuwa kisheria huwezi kuelewa state of mind ya mtu wakati anafanya tendo lolote lile)....Kwa hiyo ilikuwa ni halali kwa polisi kumkamata na kumnyong'onyeza maana akkuwa anaendelea kutishia na hakujisalimisha kwa polisi!! Isitoshe polisi hawajatumia bastola au silaha nyingine, wametumia Judo na virungu...which so far was reasonable force!!
SOMO
Tunaipenda CDM lakini mbinu zake sasa zinatuchosha, watapigwa sana kama hawatakaa chini na kujadili mbinu mbadala! Wote tunajua kwa nini RPC Arusha alibadilishwa, yule jamaa na watu wake wako kwa kazi maalumu, wanasubiri kuwa "tuned" tu, sasa kama adui umeshamuelewa anakupaje kazi kupambana naye? Hebu CDM wafuate sheria, wapambane KISAYANSI siyo kwa kutumia nguvu "ZA KIJINGA"....Kamwe hatutaweza kushindana na dola....TUWE MAKINI

Kaka au sijui ni dada tafadhali tuambie nini maana ya kupambana KISAYASI???? Hivi polisi anaruhusiwa kutoa hukumu kwa mtuhumiwa au ni mahakama? unamaanisha wale polisi walivyotoa ile adhabu kwa bwana Lema walitumia nguvu ya KISAYANSI SIO???
 
Well:

Ukiangalia ile "fracas" kati ya Lemma (MP) na Police Detectives utaona kuwa Lemma alikataa kutii "order" ya kumtaka asilete vurugu mahali pale (uhalali wa order is questionable though), halafu yeye in return akachomoa "pistol" (as self defence?) ndipo Police Detectives (seems kule Arusha kuna special forces wa kutosha) waka-hit the most sensitive parts/mishipa ya fahamu kujaribu kum-subdue in very quickest possible way!

Lini wewe pia umekuwa ****?
 
Mimi nilikuwa natazama TV nikaona kipigo hiki cha Godbless Lema na Polisi walivyokuwa wanamchapa.

Inaonekana kwamba viongozi walioteuliwa na Serikali ya CCM wamesahau Katiba na Sheria ya Uchaguzi. Kilichotokea katika jimbo la Arusha Mjini ni kwamba wananchi wapiga kura walimchagua Godbless Lema kuwa Mbunge wao. Mbunge huyu amekwisha apizwa na ni Mbunge halali. Huyu ni MHESHIMIWA sasa na msamiati wetu unatambua hivyo.

Mbunge yeyote ana haki na uhuru kuhutubia waliompigia kura na kuwa na vikao na wananchi wa jimbo lake, kujadili nao jinsi ya kutatua matatizo yao. Polisi sio tu wamheshimu, bali wanatakiwa wampe ulinzi ili atekeleze wajibu na majukumu yake.

IGP Mwema anatakiwa atoe mwongozo kwa RPCs wote wazingatie kuwaheshimu Wabunge wa vyama vyote vya siasa. Polisi wakiheshimu Wabunge watakuwa wanaheshimu na kuenzi maamuzi ya wananchi. Polisi wa cheo chochote asiyeheshimu Mbunge, na hasa anayempiga au kumdhalilisha hafai. Afukuzwe.

Watumishi wa Serikali kama Mkurugenzi wa Manispaa wanatakiwa wakubali maamuzi ya wananchi wapiga kura. Kujaribu kuibeba CCM na kupindisha taratibu ili wawakilishi waliochaguliwa wasishiriki ni kubaka demokrasia na ni kinyume cha Katiba na sheria. Kuita Polisi katika mikutano ya madiwani, eti wawadhibiti ndio kuchochea fujo na kuweka vitisho visivyo na msingi. Madiwani wa vyama vyote vya siasa wawezeshwe kujadili na kushiriki katika vikao vyao, na ndivyo wananchi walivyotaka walipowachagua.
 
Nasubiri kusikia huyu bwana andengenya na yule mnali(aliyewacharaza mboko walimu) wanapandishwa vyeo,maana waapuz kama lema lazima wafundishwe adabu.

Mawazo yako ni finyu hata mtoto wa darasa la kwanza anakushinda, anyway, ni CCM ndio inakupa kiburi, lakini kumbuka machafuko yakitokea hayakuchagui. Hata wewe na uzao wako utaathirika.
 
"Mawazo yako ni finyu hata mtoto wa darasa la kwanza anakushinda, anyway, ni CCM ndio inakupa kiburi, lakini kumbuka machafuko yakitokea hayakuchagui. Hata wewe na uzao wako utaathirika."


jaribu kumwelewesha huyo asione walimu wamekaa kimya akadhani wamefurahi kwani me ni mwanafunzi wa shahada hiyo ya ualimu niliudhika sana. Halafu hii Tz yetu imekuwa kama nchi ya kusadikika wajumbe wema na wapenda maendeleo wamekuwa wakipigwa vta wakionekana ni wazushi. Me naanza kuamini wakina Shaaban Robert walikuwa wanaona mbali na ni manabii ambao hawakukubalika kwao.
 
Kwenye magazeti ya leo tunaona kauli za CCM zinavyojipinga zenyewe............................

Kwenye gazeti la majira lina kichwa cha habari Chadema watoa masharti ya mgogoro wa Mameya..........................

Uhuru lasema...................Makamba amjibu Lowassa.....................Asema CCM haitaongea na Chadema.....CCM isihusishwe na vurugu za Arusha.....wengi wamshangaa..................

The CItizen ..........Chadema tells Tendwa to call urgent meeting...............................

Daily News................CCM speaks on Arusha violence........defends Lowassa........................................

Yote haya yaashiria ya kuwa busara bado siyo sera ya CCM ila ni mabavu tu.........na hili haliisaidi taifa hata chembe..............................

Mtanzania.........................Makmba amrulka Lowassa..................................
 
watatiwa adabu mpaka wakome. wao si walisema asiyefunzwa na mamake afunzwe na ulimwengu? hiyo ndiyo habari
 
Back
Top Bottom