Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Mbunge wa Arumeru mashariki Mhe.Joshua Nassari tarehe 17/02/2019 alikutana na Askofu Paul Erickson katika jimbo la Wisconsin Marekani kupata chakula cha mchana.
Pamoja na mambo mengine walijadiliana mambo mabali mbali ya kuendeleza mradi wa Maji ambao waliufadhili kupeleka maji kutoka Tengeru hadi Kikwe ambapo kwa mujibu wa Mhe.Nassari wafadhili hao wanajipanga ili kuufikisha mradi huo hadi msitu wa mbogo na Shambarai Burka.
Mhe.Nassari yupo Marekani kwenye programu ya mafunzo ya viongozi kupitia taasisi ya Obama Foundation kwenye Jimbo la Chicago
Ikumbukwe mnamo mwezi wa nane mwaka jana 2018 Mhe Nassari alimkabidhi Askofu Erickson na timu yake vyeti vya shukrani baada ya kukamilika kwa mradi huu wa maji sehemu ya kwanza uliogharimu takribani tshs 120M chini ya ufadhili wa dayosisi anayoiongoza. Ashukuriwe Mungu.
Pamoja na mambo mengine walijadiliana mambo mabali mbali ya kuendeleza mradi wa Maji ambao waliufadhili kupeleka maji kutoka Tengeru hadi Kikwe ambapo kwa mujibu wa Mhe.Nassari wafadhili hao wanajipanga ili kuufikisha mradi huo hadi msitu wa mbogo na Shambarai Burka.
Mhe.Nassari yupo Marekani kwenye programu ya mafunzo ya viongozi kupitia taasisi ya Obama Foundation kwenye Jimbo la Chicago
Ikumbukwe mnamo mwezi wa nane mwaka jana 2018 Mhe Nassari alimkabidhi Askofu Erickson na timu yake vyeti vya shukrani baada ya kukamilika kwa mradi huu wa maji sehemu ya kwanza uliogharimu takribani tshs 120M chini ya ufadhili wa dayosisi anayoiongoza. Ashukuriwe Mungu.