Mbunge Tarimba apendekeza TANESCO kufumuliwa na kuwepo kampuni 3 kwa ajili ya Uzalishaji, Usafirishaji na Ugawaji umeme

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
Mbunge wa Kinondoni, Tarimba Gulam Abbas amehoji ikiwa Serikali haioni ni muda mwafaka wa kulifumua Shirika la Umeme (TANESCO) ili kuwe na Kampuni tatu kwa ajili ya kufanya Generation Uzalishaji, Usafirishaji na Usambazaji kama ilivyo Nchi nyingine.

Akimjibu, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kukatwa na kutolewa kwa maeneo hayo kwa watu tofauti kunaweza kuleta athari kwenye Usalama wa Nchi pale Umeme unapohitajika wakati wote na mmoja ya waliopewa jukumu awe anaenda kinyume na mipango, hivyo malengo kushindwa kufikiwa.

Amesema kwa Hali iliyopo Nchini, maeneo yote ya Uzalishaji umeme yanaendelea kufanya hivyo lakini changamoto ni miundombinu ambayo hata sasa inapeleka baadhi ya maeneo kukatiwa Umeme.
 
Mbunge wa Kinondoni, Tarimba Gulam Abbas amehoji ikiwa Serikali haioni ni muda mwafaka wa kulifumua Shirika la Umeme (TANESCO) ili kuwe na Kampuni tatu kwa ajili ya kufanya Generation Uzalishaji, Usafirishaji na Usambazaji kama ilivyo Nchi nyingine.
....
TANESCO inaenda kuwa sehemu mahsusi ya kufisadi. Matrilioni yaliyolipwa tangu miaka ya tisini bado tu hawataki kuiacha ipumue!
 
Nini hoja yako mkuu, TANESCO isigawanywe kwa sababu tu ikigawanywa kutakua na CEO watatu ?
Kwaiyo wewe hofu yako ni kwenye "vyeo" tu !
Kama inashindwa kuperform leo ikiwa chini ya komandi moja hiyo ya sauti tatu unaona itakuwa na tija? Suala la vyeo ni tatizo kwani vyeo siyo majina zina gharama Kama hilo hulijari basi kuna tatizo mahali.
 
Kama inashindwa kuperform leo ikiwa chini ya komandi moja hiyo ya sauti tatu unaona itakuwa na tija? Suala la vyeo ni tatizo kwani vyeo siyo majina zina gharama Kama hilo hulijari basi kuna tatizo mahali.
What if kwa maono yake mtoa pendekezo kuigawanya TANESCO makampuni matatu tofauti itaongeza tija na ufanisi?
Uzalishaji - Shirika lake
Usafirishaji - Shirika lake
Usambazaji - Shirika lake.

Tukiachana na ubishani ambao tunaweza kuufanya hapa, kwa maoni yangu TANESCO kwa sasa wanafanya kazi nyingi mno.
Ili kuongeza tija, hata kama litabaki kuwa Shirika moja, liongezewe uwezo kwa kiwango kikubwa sana kwa maana ya rasilimali watu, teknolojia, miundombinu, fedha n.k

Vinginevyo tuligawe ili tupate mashirika matatu yatakayoshugulika na maeneo madogo madogo kwa ufanisi mkubwa.

Kwa hali ilivyo sasa hii TANESCO sidhani kama itaweza kui'accommodate Tanzania ya kweli ya viwanda na mradi wa treni ya umeme.

Muda utaongea.
 
Wazee wa kuchungulia michongo hao usikute katumwa huyu kila kitu kimeshapangwa.

Haya mambo tuliyasema humu kipindi Kuwa huo ndio mkakati wenyewe na sasa ndio yanaanza kutimia!! huyu Tarimba Abass ni kibaraka wao tu anatumiwa kufanikisaha ufedhuli wao!!

Sasa utasikia hao wabunge wa ccm nao wanaimba wimbo huo huo. ; wenzao wa ANC kule bondeni walisimama kidete TANESCO yao [ ESKOM] ilipotaka kuuzwa kwa mtindo huo!!
 
Mbunge wa Kinondoni, Tarimba Gulam Abbas amehoji ikiwa Serikali haioni ni muda mwafaka wa kulifumua Shirika la Umeme (TANESCO) ili kuwe na Kampuni tatu kwa ajili ya kufanya Generation Uzalishaji, Usafirishaji na Usambazaji kama ilivyo Nchi nyingine....
South Africa wamepitisha mpango wa kugawa shirika lao hivyo ila hadi sasa miaka kadhaa imepita wameshikwa na kigugumizi kutekeleza. Tusirukie matawi kama nyani tutaanguka.

Kuna risk kwenye utaratibu kama huo hasa kama tutaruhusu yawe makampuni binafsi ya wageni. Nia yetu kuwaletea wananchi maendeleo inaweza pata kikwazo.
 
What if kwa maono yake mtoa pendekezo kuigawanya TANESCO makampuni matatu tofauti itaongeza tija na ufanisi...
Tatizo la tanesco kwa sasa siyo kusambaza umeme bali hakuna umeme wa kutosha. Hivyo hata ukiigawa tanesco katika mashirika matatu utapata wapi umeme wa kusambaza?

Jitihada ielekezwe katika kutafuta vyanzo vipya na vingi zaidi vya umeme, usambazaji hauna tatizo kubwa!
 
Moja imewashinda tatu mtaweza?

TANESCO walipaswa wapate mshindani mmoja tu kutoka nje ya nchi awafunze adabu.

Wangeoneshwa namna ya kutoa huduma sio ujinga walionao sasa.
Huyo mshindani atapata umeme kutoka wapi?
 
Mbunge wa Kinondoni, Tarimba Gulam Abbas amehoji ikiwa Serikali haioni ni muda mwafaka wa kulifumua Shirika la Umeme (TANESCO) ili kuwe na Kampuni tatu kwa ajili ya kufanya Generation Uzalishaji, Usafirishaji na Usambazaji kama ilivyo Nchi nyingine...
Wabunge aina ya Abbas Tarimba ni wabunge walioingia bungeni kusaka maslahi zaidi kuliko kuwakilisha wapiga kura.

Ukiona hivyo ujuwe kabisa kuna maslahi binafsi anawakilisha kutoka genge la kipigaji,ambalo linaiona kama fursa.

Binafsi hawa wabunge wafanyabiashara sampuli ya Tarimba,Musukuma,Abood nk,huwa nawachukulia kama wametafuta ubunge ili kujiweka karibu na michongo ya kibiashara zaidi.
 
Vinginevyo tuligawe ili tupate mashirika matatu yatakayoshugulika na maeneo madogo madogo kwa ufanisi mkubwa.

Ukubwa wa shirika unahusiana vipi na ufanisi wake ? Hata ukiligawa kuwa mashirika matatu kama utendaji wake katika hayo mashirika matatu utabaki hivyo hivyo, hakutakuwa na ufanisi wowote!! Inaelekea mbinu ya kuligawa shirika sio kulipatia ufanisi bali kutaka kuliuza kwa private operator.!! Huu ni mchongo wa Msoga Gang! Ndio maana wamemuweka Omar Issa kama Mwenyekiti wa TANESCO!!!

Remember Tanesco is very crucial to the success of other investments like the STANDAD GAUGE RAILWAY such that to put it into the hands of private operators can easily compromise national security!!

Argument kama hii ilitumika kuuza National Bank of Commerce kuwa ilikuwa inapata hasara kwasababu ilikuwa kubwa na watu wakapiga Pesa pale na Kaburu akachukua benki na assets zake kwa bei ya bure!!! We Shule learn from our past mistakes. KUFANYA KOSA SIO KOSA, KOSA KURUDIA KOSA.
 
Hofu yake ni kuongeza mzigo kwa wa gharama kwa mteja wa TANESCO. Kwa nini, vitengo vya uzalishaji, usambazaji, na uuzaji kwa mteja visiimarishwe?
TANESCO ya sasa kwa namna ilivyo haitatufikisha mbali kama taifa.

Zipo options mbili za kuiboresha.

1. Kuboresha utendaji wa vitengo vyake vya uzalishaji, usafirishaji na usambazi wa umeme kama ulivyoeleza hapo.

2. Kuligawa shirika ili tupate mashirika mawili au matatu yatakayoshughulikia kikamilifu kazi hizo tatu.

In both two cases maboresho yanahitajika ili kuleta tija na ufanisi zaidi.
Mwenzetu Tarimba Abbas kaona approach ya pili ndio inafaa zaidi na kashauri hivyo.

Yote kwa yote, nyakati zijazo zinazihaji huduma ya kuaminika ya umeme (umeme uwe mwingi, usambazaji uwe wa uhakika).

Kwa muundo wa sasa TANESCO inabeba risks and responsibilities nyingi mno.

1. Maji yamekauka Kidatu - TANESCO
2. Visima vya gesi vinahitaji matengenezo - TANESCO
3. Nguzo zimeanguka Mafinga - TANESCO
4. Mfumo wa kununua LUKU una shida - TANESCO
5. Bibi Chausiku amelipia umeme hajaunganishwa - TANESCO
6. Kutengeneza nguzo za zege, kukata miti chini ya nguzo - TANESCO
7. Kubadili tariffs kwenda kwenye matumizi madogo - TANESCO.
8. Tunataka kuwauzia Malawi umeme - TANESCO
This is so much to do.

Tuiboreshe TANESCO kwa kweli, whatever the means, vinginevyo tutazidi kumlalamikia tu J. Makamba kila kunapokucha.
 
Back
Top Bottom