Mbunge Saashisha Mafue adaiwa kuwalipa vijana walioajiriwa kazi ya muda ya Postkodi Tsh. 15,000 kwa siku mkataba wa siku 15

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
12,809
21,411
Mbunge wa CCM Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro, Mh. Saashisha Mafue anadaiwa kuwalipa vijana walioajiriwa ajira ya muda ya Postikodi Tsh 15,000 kwa siku badala ya Tsh 30,000 kwa siku kama ilivyopangwa nss as Serikali ya Rais Samia.

Pili, Mbunge huyo anadaiwa amewaambia vijana hao kuwa ajira hiyo ni ya muda wa siku 15 badala ya siku 45 kama ilivyoainishwa na serikali ili zoezi lifanyike kwa Uangalifu na kwa umakini mkubwa.

Vijana hao wameamua kufanya kazi hiyo bila ufanisi kutokana na kulipwa malipo tofauti na mpango wa serikali, ila siku ya jumamosi tarehe 19.3.2022 wataandamana kumpokea mwenyekiti wa chadema Taifa ambaye atahutubia Jimbo la Hai mjini ikiwa ni mara ya kwanza tangu atoke gerezani na watafikisha kilio hicho mbele yake kwa mabango.

Mkuu wa Wilaya ya Hai alivyotafutwa kuzungimzia malipo hayo na siku za kufanya kazi hakutaka kusema chochote bali alisema hausiki na zoezi hilo na hakushirikishwa.

Mkurugenzi Mtendaji wa wilaya ya Hai , Dionis Myinga alivyotwafutwa ofisini kwake palikuwa pamefungwa.

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Stephen Kagaigai, tulivyompigia simu ,kumuuliza kuhusu stahiki ya malipo kwa hao vijana wanaofanya kazi kwa mkataba, kwa kila siku na muda wa kazi hadi kumalizika alisema yuko kwenye kikao.

Vijana hao wanakiomba Chama cha mapinduzi ngazi ya wilaya, mkoa, Taifa kuingilia kati hatima ya malipo yao na siku za kufanya kazi hiyo kama ilivyopangwa na serikali ya CCM. Vijana wamekata tamaa iliyosababishwa na mtu mmoja au kikundi cha watu.
 
Mbunge wa CCM Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro, Mh. Saashisha Mague ,amefanya maajabu kwenye serikali ya awamu ya sita kwa kuwalipa vijana walioajiriwa ajira ya muda ya Postikodi Tsh 15,000 kwa siku badala ya Tsh 30,000 kwa siku kama ilivyopangwa nss as Serikali ya mama Samia...

Mkuu huyo mbunge unamuonea tuu hizi kazi hazitolewi na mbunge bali ni Halmashauri husika?

Mbunge unamuonea tuu
 
Mbunge wa CCM Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro, Mh. Saashisha Mague ,amefanya maajabu kwenye serikali ya awamu ya sita kwa kuwalipa vijana walioajiriwa ajira ya muda ya Postikodi Tsh 15,000 kwa siku badala ya Tsh 30,000 kwa siku kama ilivyopangwa nss as Serikali ya mama Samia...
Ebu twende taratibu.

1. Ajira zilitangazwa na nani!?

2. Pesa za malipo zinatoka kweny source gani?

3. Taarifa za postcode zinapelekwa kwa nani zikikamilika.

4. Hao vijana wanalipoti kwa nani!??
 
Ebu twende taratibu..
1. Ajira zilitangazwa na nani!?
2. Pesa za malipo zinatoka kweny source gani?
3. Taarifa za postcode zinapelekwa kwa nani zikikamilika
4. Hao vijana wanalipoti kwa nani!??
 

Attachments

  • temmeke usail.pdf
    245 KB · Views: 16
Mbunge wa CCM Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro, Mh. Saashisha Mague ,amefanya maajabu kwenye serikali ya awamu ya sita kwa kuwalipa vijana walioajiriwa ajira ya muda ya Postikodi Tsh 15,000 kwa siku badala ya Tsh 30,000 kwa siku kama ilivyopangwa nss as Serikali ya mama Samia...
1647450346716.png
 
Mbunge wa CCM Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro, Mh. Saashisha Mague ,amefanya maajabu kwenye serikali ya awamu ya sita kwa kuwalipa vijana walioajiriwa ajira ya muda ya Postikodi Tsh 15,000 kwa siku badala ya Tsh 30,000 kwa siku kama ilivyopangwa nss as Serikali ya mama Samia...
Kwani wabunge ndio wanaoajiri hao vijana?....acheni propaganda za kuchafuana.
 
Vijana ajira ya muda postikodi badala ya kulipwa Tsh 1,350,000 kwa siku 45 baada ya kumaliza kazi , sasa watalipwa Tsh 225,000 kwa siku 15 na kazi itakuwa haijamalizika .

Ni nini ukweli halisi wa malipo haya kwa nchi nzima?
Kuna upigaji wa hizi fedha setiksli ifuatilie kila Jimbo itaona maajabu .
 
Mbunge wa CCM Jimbo la Hai Mkoani Kilimanjaro, Mh. Saashisha Mague ,amefanya maajabu kwenye serikali ya awamu ya sita kwa kuwalipa vijana walioajiriwa ajira ya muda ya Postikodi Tsh 15,000 kwa siku badala ya Tsh 30,000 kwa siku kama ilivyopangwa nss as Serikali ya mama Samia...
Palipo na ccm hakuwezi kutendeka haki.
 
Kwani wabunge ndio wanaoajiri hao vijana?....acheni propaganda za kuchafuana.
Ili kupata ukweli wa jambo hili piga namba hii 0621-955-483 au 0623-988-579 au 0767-844-191 Jf sio mtandao wa Baddoo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom